mtoto hataki kunyonya

mtoto hataki kunyonya

cjui mimi

Member
Joined
Jul 7, 2013
Posts
67
Reaction score
8
heshima zenu wakuu,
nina mtoto wa miezi mitano na nusu leo ni siku ya tatu ziwa la mams yake halitaki kabisa ila ukimpa ile chupa ya kunyonyea watoto ananyonya vizuri tu! msaada wenye utaalam inaweza kuwa ni tatizo?
niko mbali kidogo na family napewa maelekezo kwa njia ya simu tu
 
Acha usimnyonyeshe! endelea kumpa maziwa ya ng'ombe yaliyochemshwa vizuri kwasasa na kisha fanya jitihada za kumuona daktari wa magonjwa ya akina mama na watoto haraka.
 
Muone daktari wa watoto akueleze shida nini? kwasababu kwa umri huo kasi ya kunyonya huwa ni kubwa sana na ukizingatia bado hajafika umri wa kupewa chakula.
 
Huyo mtoto alikuwa anapewa maziwa ya chupa kabla hajagoma kunyonya ziwa?
Inatokeaga kwamba mtoto anakaatga kunyonya kwasababu anaprefer ladha ya maziwa ya chupa kuliko ya ziwa la mama na haswa kama huna maziwa ya kutosha kwenye maziwa...
 
Huwa inatokea wakwangu alikataa akiwa na miezi 3;ikabidi anywe ya ng'ombe kwa chupa;nilienda kwa dr wa watoto ikashindikana;kamwone dr.wa watoto;chaajabu mdogo zake wamenyonya mpaka 3 yrs.usiogope
 
Muone daktari wa watoto akueleze shida nini? kwasababu kwa umri huo kasi ya kunyonya huwa ni kubwa sana na ukizingatia bado hajafika umri wa kupewa chakula.

ni kweli kaka mimi mwenyewe nashangaa
 
Huyo mtoto alikuwa anapewa maziwa ya chupa kabla hajagoma kunyonya ziwa?
Inatokeaga kwamba mtoto anakaatga kunyonya kwasababu anaprefer ladha ya maziwa ya chupa kuliko ya ziwa la mama na haswa kama huna maziwa ya kutosha kwenye maziwa...

hajawahi kupewa maziwz ya ngombe kabla, mama yake ana maziwa ya kutosha tu na hivi sasa yanamsumbua kwani yanajaa sana maziwa na dogo ndo kagoma
 
Huwa inatokea wakwangu alikataa akiwa na miezi 3;ikabidi anywe ya ng'ombe kwa chupa;nilienda kwa dr wa watoto ikashindikana;kamwone dr.wa watoto;chaajabu mdogo zake wamenyonya mpaka 3 yrs.usiogope

wamekwe da kwa daktari hakuna shida yoyote ila dogo tu ndo hataki akipewa cerelac anakula, maziwa kwa chupa ananyonya na na naabiwa anashikilia chupa mwenyewe
 
Hana shida huyo, atafutiwe maziwa ya ngombe mazuri,yachemshwe vizuri na kwamuda wa dk kama 10,ila yaweyanatolewa ile crimu ya juu kama mara tatu hivi alafu ndo apewe mtoto ,na iyo cerelac siyo mbaya ,ila muhimu juice fresh,
 
Na baadae atarudia kunyonya japo siku za mwanzo ataharisha nk.
 
shukran wakuu dogo yuko vzr ingawa hataki kunyonya ziwa ila ndo tumehamia plan b maziwa kwa chupa, cerelac, juice, na uji mchanganyiko naambiwa anakula vzr
 
Mama kama anaweza ajaribu kumkamulia maziwa yake, lakini inatakiwa kazi hiyo ifanywe kwa usafi wa hali ya juu na pia kuna vyombo vya kukamulia na si ghali sana au ajaribu kumdanganya mtoto kwa kumpa maziwa ya chupa akianza kunyonya mama aondoe chupa na kujaribu kumpa maziwa yake. Kila la heri.
 
Kama mtoto akiendelea kugoma mpe mtumzima, ospitali yake ipo mwembe yanga, uliza kwa mtu mzima utaelekezwa
 
Back
Top Bottom