habari zenu wadau, nina mtoto wa mwaka mmoja na miezi saba lakini ni mbishi wa kula chochote, ana ratiba ya milo sita kwa siku lakini sijawahi kumuona akila kwa raha ni kilio tu nifanyeje? Uzito wake hauridhishi ana 11kgs sasa hivi. Natanguliza shukran kwa msaada!
milo sita ina maana kuwa saa 12asubuhi maziwa fresh, saa 2 chakula, saa 5 maziwa fresh, saa 8mchana chakula, saa 10 uji, anakaa free akinywa juice au tunda mpaka saa 2usiku chakula.