Ulirchdov
JF-Expert Member
- Apr 4, 2019
- 356
- 258
Naomba kuelewesha sababu zinazofanya mjamzito kuzidisha miezi ya kujifungua nikiwa na maana kwamba kawaida mtoto hukaa tumboni kwa miezi tisa lakini nimekuwa nikishuhudia wajawazito wengi wakilalamika juu ya ujauzito wao kwamba siku za kujifungua zimefika na zikavuka pasipo dalili ya uchungu wa kujifungua, wengine hupitisha wiki au mwezi.
Mfano, kuna mama fulani tarehe yake ya kujifungua ilifika kwa mujibu wa hesabu zake lakini hakupata uchungu hatimaye wiki ikaisha, mwezi mmoja baadae ndo akajifungua na alijifungua salama kabisa.
Naomba kuuliza nini hasa kinasababisha mtoto/kichanga kukaa tumboni zaidi ya miezi tisa au zaidi ya tarehe ya kuzaliwa tofauti na tarehe ambazo mama zao wanazipigia hesabu?
Mfano, kuna mama fulani tarehe yake ya kujifungua ilifika kwa mujibu wa hesabu zake lakini hakupata uchungu hatimaye wiki ikaisha, mwezi mmoja baadae ndo akajifungua na alijifungua salama kabisa.
Naomba kuuliza nini hasa kinasababisha mtoto/kichanga kukaa tumboni zaidi ya miezi tisa au zaidi ya tarehe ya kuzaliwa tofauti na tarehe ambazo mama zao wanazipigia hesabu?