Mtoto kulia sana wakati wa usiku

Mtoto kulia sana wakati wa usiku

gileun

Member
Joined
Nov 8, 2017
Posts
85
Reaction score
74
Habari wakuu!
Nina mtoto wangu wa kiume kwa sasa yuko na umri wa mwezi mmoja na wiki moja. Dogo huwa analia sana wakati wa usiku hasa kuanzia mida ya saa nne usiku hivi. Siku kadhaa ilikua kulia kwake ni afadhali lakini jana ikawa ni zaidi ya siku zote,yaani kalia tangu saa nne mpaka saa nane kasoro usiku. Tungeweza sema anamaumivu ya tumbo lakini hapana maana hajikunji kunji wakati analia na zaidi ni kwamba kwa jana tulimnywesha na Sheladol kwa ajili ya maumivu maana tulihisi pengine kuna mahali panamuuma na hatuezi jua maana hawezi kutuambia. Swala la njaa tuliweka pembeni sababu alikua hata maziwa hataki kunyonya kabisa. Leo tumeenda kwa daktari kamcheki lakini dogo yuko sawa, daktari akashauri yawezekana huwa anapata mshtuko na pia wakati mwingine huwa sababu ana kiu ya maji.
Nashea uzi huu ili kujaribu kupata mwanga toka kwenu wataalam na wadau wengine juu ya nini tunaweza kufanya ili kwa kiasi kikubwa kuondokana na hili tatizo.
Natanguliza shukurani zangu za dhati kwenu!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mvumilie kwa sasa, watoto wengi hupitia hiyo hali na huchukua mda kutulia vile vile hutofautiana mda.
Chamuhimu ale ashibe bila kusahau msimfunike sana pengine joto.

Msiache kwenda hospitali mkiwa na wasiwasi au hali ikibadilika.

Poleni na Hongereni kwa kuwa Wazazi.

Ndiyo,zote anapata bila shida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Isije kuwa ni wewe unae mmalizia chakula yake! (maziwa)
Habari wakuu!
Nina mtoto wangu wa kiume kwa sasa yuko na umri wa mwezi mmoja na wiki moja. Dogo huwa analia sana wakati wa usiku hasa kuanzia mida ya saa nne usiku hivi. Siku kadhaa ilikua kulia kwake ni afadhali lakini jana ikawa ni zaidi ya siku zote,yaani kalia tangu saa nne mpaka saa nane kasoro usiku. Tungeweza sema anamaumivu ya tumbo lakini hapana maana hajikunji kunji wakati analia na zaidi ni kwamba kwa jana tulimnywesha na Sheladol kwa ajili ya maumivu maana tulihisi pengine kuna mahali panamuuma na hatuezi jua maana hawezi kutuambia. Swala la njaa tuliweka pembeni sababu alikua hata maziwa hataki kunyonya kabisa. Leo tumeenda kwa daktari kamcheki lakini dogo yuko sawa, daktari akashauri yawezekana huwa anapata mshtuko na pia wakati mwingine huwa sababu ana kiu ya maji.
Nashea uzi huu ili kujaribu kupata mwanga toka kwenu wataalam na wadau wengine juu ya nini tunaweza kufanya ili kwa kiasi kikubwa kuondokana na hili tatizo.
Natanguliza shukurani zangu za dhati kwenu!


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante sana ndugu...[emoji120]
Mvumilie kwa sasa, watoto wengi hupitia hiyo hali na huchukua mda kutulia vile vile hutofautiana mda.
Chamuhimu ale ashibe bila kusahau msimfunike sana pengine joto.

Msiache kwenda hospitali mkiwa na wasiwasi au hali ikibadilika.

Poleni na Hongereni kwa kuwa Wazazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza nikupe pole kwa tatizo hilo ndugu yangu,mie siyo daktari ila nakushauri kama mzazi usizoee kumpa dawa mtoto mchanga bila ushauri wa doctor tena doctor makini atakuruhusu umpe mtoto dawa pale anapoona imebidi.

Kingine ni ugeni wa malezi,sijui kama wewe na mkeo huu ni uzazi wa ngapi ila inawezekana mtoto hapati maziwa ya kutosha kwa wakati anaohitaji na nyie hili hamjaling'amua so anapolia sana huwa ni hasira na anakataa ziwa kutokana na ameshapewa akanyonya zaidi ya mara nne tano hakuna kitu anabaki akilia njaa.

Pia elewa unaweza kuona maziwa yanatoka vizuri ila je yana uzito unaotakikana? sometimes yanakuwa maji tu watoto wengine huzaliwa na uzito ambao unahitaji mlo mkubwa kumridhisha.chakufanya mama yake kama Mungu alimjaalia kujifungua bila upasuaji mwambie ktk milo yake ya siku awe anakula ugali wa dona mboga za majani na matunda hii itamsaidia kutengeneza maziwa mazito yatakayomtosha mtoto.

Pia kama ni mtu wa kufanya kazi nyingi mtafutie msaidizi kama uwezo hauruhusu mwambie ajipangie ratiba zake vizuri apate muda walau masaa manne ya kupumzika kwa siku na asikae kae juani ili awe anatulia maana anaweza akawa anakula vizuri ila kutokana na mizunguko yake chakula chote kinajikuta kimemsaidia yeye nguvu wakati lengo ni mtoto.

Imani yangu mtoto hana tatizo wala haumwi popote fanyeni hivi atakaa sawa,nna experience kidogo na haya mambo ila epuka kumpa madawa mtoto bila ushauri wa kitaalam wala maji wala chochote kwa muda wa miezi 6 toka azaliwe kama ni kiu maji atayapata kwenye maziwa ya mama yake,muhimu mama yake anywe maji mengi.

Mimi siyo doctor ila ushauri wangu utaweza kusaidia japo kidogo.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Ahsante ndugu yangu, kwetu ndo uzazi wa kwanza kiukwel, na kama wengi wasemavyo yaweza kuwa ishu ipo zaidi kwny maziwa ya mama...kwakua alijifungua kwa njia ya kawaida basi ttajitahid kubadili aina ya vyakula pia! Shukuran[emoji120]
Kwanza nikupe pole kwa tatizo hilo ndugu yangu,mie siyo daktari ila nakushauri kama mzazi usizoee kumpa dawa mtoto mchanga bila ushauri wa doctor tena doctor makini atakuruhusu umpe mtoto dawa pale anapoona imebidi.

Kingine ni ugeni wa malezi,sijui kama wewe na mkeo huu ni uzazi wa ngapi ila inawezekana mtoto hapati maziwa ya kutosha kwa wakati anaohitaji na nyie hili hamjaling'amua so anapolia sana huwa ni hasira na anakataa ziwa kutokana na ameshapewa akanyonya zaidi ya mara nne tano hakuna kitu anabaki akilia njaa.

Pia elewa unaweza kuona maziwa yanatoka vizuri ila je yana uzito unaotakikana yanakuwa maji tu watoto wengine huzaliwa na uzito ambao unahitaji mlo mkubwa kumridhisha?chakufanya mama yake kama Mungu alimjaalia kujifungua bila upasuaji mwambie ktk milo yake ya siku awe anakula ugali wa dona mboga za majani na matunda hii itamsaidia kutengeneza maziwa mazito yatakayomtosha mtoto.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante ndugu yangu, kwetu ndo uzazi wa kwanza kiukwel, na kama wengi wasemavyo yaweza kuwa ishu ipo zaidi kwny maziwa ya mama...kwakua alijifungua kwa njia ya kawaida basi ttajitahid kubadili aina ya vyakula pia! Shukuran[emoji120]

Sent using Jamii Forums mobile app
Rudi kwenye post yangu kuna kitu nimeongeza!

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Aisee,ni shughuli pevu sana na hutia sana stress...ikiisha hii hali ntaomba na likizo kazin[emoji28][emoji28]
Hyo ni kawaida kwa watoto wachanga japo sio wote akifikisha miezi mitatu hiyo itaisha yenyewe.
Bora wewe analia hadi sanane mimi nilikuwa nalala sakumi alfajiri dogo ndio ananyamaza

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee,ni shughuli pevu sana na hutia sana stress...ikiisha hii hali ntaomba na likizo kazin[emoji28][emoji28]

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha acha kabisa hadi mnanuniana na wife maana hanyonyi ni kulia tu wife anabembeleza anachoka ananipa narukaruka namrudishia mnamuweka kitandani analiaa mnaanza tena mpaka sa10 ndio analala

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom