Mtoto Kumeza Uchafu wa Mama Wakati wa Kuzaliwa

OCC Doctors

Senior Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
113
Reaction score
172
Kwa Lugha nyepesi
Kinyesi cha mtoto akiwa kwenye tumbo la uzazi hufahamika kama [Meconium] Mara nyingi wafanyakazi wa hospitali watamwambia mama kwamba mtoto wake "alikula" au "alimeza" uchafu, kabla au wakati wa kuzaliwa, mtoto ana hatari kubwa ya kuingiza [meconiam] ndani ya mapafu yake au kumeza, Kabla au wakati wa maumivu ya leba, mtoto aliye tumboni mara nyingine huweza kutokwa na kinyesi cha [meconium] ambapo huwenda kuchanganyikana na maji ya uzazi ya mama yake [amniotic fluid]., Inaweza ikawa ni tukio la kawaida, lakini pia inaweza kuleta madhara kwa mtoto wakati kinyesi chake kinapochanganyikana na maji ya uzazi kunaweza kupelekea mtoto akayameza au yakamuingia kwenye mfumo wa hewa, au yakampalia sehemu ya uvutaji wa hewa na kwenda kuathiri mapafu. Hali amabayo hufahamika kama [meconium aspiration syndrome] (MAS).
Tuna Karibisha MaswaliView attachment 1063821
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…