Mtoto kupiga chafya wakati akinyonya, kweli kunasababisha ziwa(titi) kuvimba?

Mtoto kupiga chafya wakati akinyonya, kweli kunasababisha ziwa(titi) kuvimba?

Ziroseventytwo

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
8,581
Reaction score
15,618
Leo, Muda huu naandika huu uzi, kuna dada huwa anatuuzia chai kila ahsubuhi. Kaja ofisini kwake, lakini anadai anasikia homa kali, nilipomwambia aende kufanya vipimo akasema tatizo analijua. Eti mtoto wake aliyekuwa akinyonya kampigia chafya ziwa lake. Na akaendelea kusema ikiwa mtoto atapiga chafya au kucheua wakati akinyonya, hupelekea mama kupata homa kali na ziwa kuvimba. Hii nimewahi kuisikia kwa mama wengi wanaonyonyesha.

Sasa kitaalamu, hii dhana ipo? Na kama ipo kitaalamu inaitwaje? Kuna connection gani hapo inayopelekea mama kupata homa wakati mtoto ni wake na maziwa ni yake?
 
Hata miminiliwah kusikia na sio kuvimba tu hufanya jipu na mm nasubiri majibu
 
Back
Top Bottom