Habari zenu waungwana,kuna mtoto wa dada yangu anaumri wa karibia miaka 3,tatizo lake mtoto hawezi kuongea...je atakuwa na matatizo gani kiutaalamu
Mi wa kwangu ana miaka minne lakini anasumbuka sana kuongea hasa kuwasiliana, ni kwamba anaweza kuongea lakini si kwa ajili ya kuwasiliana anatamka tu maneno. Nimeenda hospital Dr wanasema ni Autism.
Alisema kama kuna tiba yake au mtoto asaidiwaje?
Hauna tiba na ni ugonjwa ambao upo kwenye range nyingi so kila mtoto anatakiwa aangaliwe kipekee kutokana intensity ya ugonjwa wenyewe, thanks God kwamba wa kwangu hayupo kwenye upande mbaya sana lakini hawezi kabisa kuwasiliana, kwa mfano akimaliza kujisaidia huwa hawezi kusema nimemaliza wakati mdogo wa miaka miwilli anaweza. akitaka kitu atakushika mkono kukuonyesha. ila hayo maneno ya tayali au kusoma sehem anaweza lkn si kwa ajili ya kuwasiliana anatamka tu hasa akisikia mtu anayasema.
Habari zenu waungwana,kuna mtoto wa dada yangu anaumri wa karibia miaka 3,tatizo lake mtoto hawezi kuongea...je atakuwa na matatizo gani kiutaalamu