Msanii nyota wa filamu nchini Sherry Charles Magali ambaye ni mtoto wa mzee Magari amefariki dunia akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro wodi namba 8.
Msanii huyo, amefariki leo saa nne asubuhi baada ya kuugua kwa muda mrefu. Kwa mujibu wa familia, taarifa zaidi za mazishi zitatolewa baadae. Fichuo Tz inatoa pole kwa wafiwa na kumtakia marehemu alale pema- ameen!