Habari....
Mtoto wangu wa kiume ana miezi 2 toka azaliwe....anasumbuliwa sana na tumbo....wengine wanasema ngiri, wengine wanasena chango....kitovu chake ni kikubwa kiasi (kama golori) lakini ikitokea chango likambana ndo inakuwa kama kinavyoonekana katika picha...na analia sana kwa maumivu makali......naomba msaada/ushauri
View attachment 147804
Hiyo ni umbilical hernia.
Tatizo hilo linasababishwa na ukuta wa tumbo kuwa haujafunga vizuri na hivyo sehemu ya utumbo unapenya na kuja mpaka chini ya ngozi. Hatari yake ni kwamba utumbo unaweza kuziba na kusababisha maumivu makali au hata mtoto kupoteza maisha iwapo hali ya namna hiyo haitatatuliwa mapema.
Kwa kawaida hizi hernia za watoto huwa zinapotea zenyewe kadri mtoto anavyokua, hata hivyo ushauri wangu kwako ni kuwa kwa vile huduma za afya za dharura nchini sio za uhakika. Hakikisha mtoto anafanyiwa operation mapema bila kungoja dharura. Huu ni ushauri wa kiujumlajumla, lakini iwapo mazingira yako yana uhakika wa kupata huduma ya dhararu iwapo itatokea hernia kuwa incarcerated basi unaweza kumuacha tu mtoto bila operation mpaka kuwe na emergency kwa matumaini kwamba itajifunga yenyewe kadri mtoto anavyokua.
asante sana ZeMarcopolo
ushauri wako ni mzuri sana....sikuwaza hata kidogo juu ya hernia, nilijua ni chango / ngiri
THANX
Habari....
Mtoto wangu wa kiume ana miezi 2 toka azaliwe....anasumbuliwa sana na tumbo....wengine wanasema ngiri, wengine wanasena chango....kitovu chake ni kikubwa kiasi (kama golori) lakini ikitokea chango likambana ndo inakuwa kama kinavyoonekana katika picha...na analia sana kwa maumivu makali......naomba msaada/ushauri
View attachment 147804
Kwa kawaida hernia kubwa kama hiyo sio hatari sana uwezo wa kubana ni mdogo sana kwa hiyo usiwe na wasiwasi sana. Kusema itaziba yenyewe akikua sina uhakika sana lakini inaweza tokea. Cha msingi ni observation tu kama ikitokea kikabanwa ndio akimbizwe hosp kwa ajili ya operation kama madaktari wataona inafaaa. Kumuwahisha hosp kwa ajili ya op kama alivyoshauri marcopolo mimi nisingeshauri mpaka walau akue kue kidogo.