MY LOVE
Senior Member
- Oct 17, 2012
- 161
- 68
An entrepreneur is born or made? Naomba mnisaidie ndugu zangu kwani maisha ya kusubiri ajira yamenishinda sasa. Nafikiria kuwa mfanyabiashara au mkulima lakini sina hata moja ninalolijua juu ya biashara wala kilimo jinsi ya kuanza mpaka kufanikiwa, nasikia kuna makabila Fulani wao niwafanyabiashara kuanzia babu mpaka kitukuu hata kama hajasoma lakini anauwezo wakufanya biashara na ikafanikiwa kuliko msomi mwenye degree kadhaa, ktk hili kuna siri gani? mimi sijazaliwa ktk hiyo jamii na elimu ya Bongo niliyopata haikuniandaa kuwa mjasiriamali wala mkulima tunadanganyana ukimaliza tu unapata ajira. Sasa nitajifunzia wapi kuwa mfanyabiashara mzuri au mkulima mzuri bila kupata hasara kubwa? kwani nimeona baadhi ya watu walioingia kichwa kichwa kwenye biashara au kilimo na wakafilisika hata kile kidogo walichokuwa nacho.