Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
- Anthony Murimi alikamatwa 2015 kwa madai ya wizi wa kimabavu
- Alikaa rumande kwa miezi 24 kabla ya kesi hiyo kutupiliwa mbali baada ya kukosekana kwa ushahidi
Jamaa kutoka Kayole amepokea KSh.4.5 milioni kama fidia na nyongeza nyingine ya KSh.500,000 baada ya kukamatwa na kufungwa kimakosa.
Jaji wa mahakama kuu James Makau alitoa uamuzi huo Ijumaa, Juni 5 na kusema afisi ya DPP ilikiuka haki ya Anthony Murimi Waigwe kwa kumshtaki kwa kosa la wizi wa kimabavu bila ushahidi wowote 2015.
Jaji Makau aligundua kwamba shtaka hilo halikuwa na uzito wowote kwani mshukiwa hakupatikana na bidhaa zozote za wizi kulingana na ripoti ya Citizen TV.
Waigwe, ambaye alikuwa akihudumu katika duka moja la jumla mtaani Donholm, alikutana na maafisa wa polisi akirejea nyumbani jioni.
Murimi alikamatwa na kupelekwa kituo cha Polisi Kayole ambapo alikaa zaidi ya wiki moja kabla ya kufikishwa mbele ya mahakama kujibu mashtaka hayo ya uongo dhidi yake.
Baadaye alishtakiwa kwa wizi wa kimabavu baada ya gwaride la kiwatambua washukiwa kuandaliwa.
Jaji Makau alisema Waigwe alidhulumiwa na kufungwa bila hatia.
- Alikaa rumande kwa miezi 24 kabla ya kesi hiyo kutupiliwa mbali baada ya kukosekana kwa ushahidi
Jamaa kutoka Kayole amepokea KSh.4.5 milioni kama fidia na nyongeza nyingine ya KSh.500,000 baada ya kukamatwa na kufungwa kimakosa.
Jaji wa mahakama kuu James Makau alitoa uamuzi huo Ijumaa, Juni 5 na kusema afisi ya DPP ilikiuka haki ya Anthony Murimi Waigwe kwa kumshtaki kwa kosa la wizi wa kimabavu bila ushahidi wowote 2015.
Jaji Makau aligundua kwamba shtaka hilo halikuwa na uzito wowote kwani mshukiwa hakupatikana na bidhaa zozote za wizi kulingana na ripoti ya Citizen TV.
Waigwe, ambaye alikuwa akihudumu katika duka moja la jumla mtaani Donholm, alikutana na maafisa wa polisi akirejea nyumbani jioni.
Murimi alikamatwa na kupelekwa kituo cha Polisi Kayole ambapo alikaa zaidi ya wiki moja kabla ya kufikishwa mbele ya mahakama kujibu mashtaka hayo ya uongo dhidi yake.
Baadaye alishtakiwa kwa wizi wa kimabavu baada ya gwaride la kiwatambua washukiwa kuandaliwa.
Jaji Makau alisema Waigwe alidhulumiwa na kufungwa bila hatia.