Mtuhumiwa anaweza kupata dhamana kwa makosa mawili yanayofanana?

Mr Kiroboto

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2008
Posts
350
Reaction score
90
Habari wana JF

Mimi nataka kufahamu sheria inasemaje. Kuna mtuhumiwa alifikishwa polisi kwa kosa la utapeli, upelelezi haukukamilika, mtuhumiwa alitimiza masharti ya dhamana akawa nje, baada ya siku mbili akakamatwa tena kwa kosa lingine la utapeli.

Je mtuhumiwa huyu anaweza kupata dhamana nyingine au sheria inasemaje??
 
Sheria ya kuhusu dhamana imetaja kosa mojamoja. Haijasema kwa sababu mtuhumiwa anatenda kosa mara kwa mara basi dhamana yake ifungwe.

Hebu aje mwanasheria Janjaweed atakuelezea vizuri.
 
Sheria ya kuhusu dhamana imetaja kosa mojamoja. Haijasema kwa sababu mtuhumiwa anatenda kosa mara kwa mara basi dhamana yake ifungwe. Hebu aje mwanasheria Janjaweed atakuelezea vizuri.
Shukran,malyenge.Ngoja aje huyo Janjaweed.
 
Dhamana ni haki ya mshtakiwa hata hivyo yapo makosa yasiyo na dhamana kama murder, money loundering, treason n.k

Hata hivyo zipo sababu zinazo weza kusababisha mtuhumiwa akanyimwa dhamana mfano kama mtuhumiwa anaweza kuharibu ushahidi, kama usalama wake uko hatiani, au anaweza kuhatarisha usalama kama ataachiwa.

Pia DPP amepewa mamlaka ya kuzuia dhamana ya mtuhumiwa kama ataeleza sababu mbele ya hakimu.
 
My learned brothers,

Ppamoja na sababu nyingi zilizotajwa hpo juu. mtuhumiwa anabaki kuwa mtuhumiwa hata kama atatuhumiwa kwa makosa mia.

Haki ya dhamana ipo palepale isipokuwa tu mtu huyu atakuwa amefanya kosa hilo hilo kwa kujirudirudia basi mtuhumiwa huyo anaweza kutiliwa shaka kuwa asipate dhamana.

Hilo linatokea pale ambapo upande wa mashtaka anona mtu huyu kutoka na makosa mengi anayokabiliwa anaweza kuwatoka au kujiua basi watiomba mahakama kuwa mtuhumiwa au mshtakiwa asipewe dhamana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…