Mtwara: Atupwa jela miaka 30 kwa kukutwa na bangi nyumbani

Mtwara: Atupwa jela miaka 30 kwa kukutwa na bangi nyumbani

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mahakama ya Wilaya ya Mtwara imemhukumu kwenda jela miaka 30, Salum Shamte (35), Mkazi wa Libobe wilayani hapa kwa kosa la kusafirisha dawa za kulevya aina ya bangi.

Hukumu hiyo imetolewa siku ya Alhamisi Machi 23, 2023 (jioni) na Hakimu wa Mahakama hiyo, Lucas Jang'andu baada ya kuridhishwa na maelezo ya mashahidi watano waliotoa ushuhuda wao mbele ya mahakama.

Kesi hiyo namba 21 ya mwaka 2021 ilifikishwa mbele ya Hakimu Jang'andu kwa mara ya kwanza Februari 18, 2022 na Mwendesha Mashtaka wa kesi hiyo alikuwa Wakili wa Serikali Gedion Magesa.

Awali ilielezwa mahakamani hapo kuwa Shamte alikamatwa baada ya polisi waliokuwa doria eneo la Libobe kufika na kufanya upekuzi nyumbani kwa mshtakiwa huyo kufuatia taarifa za kiintelijensia walizozipata na kukuta kiroba cha kilo 12 za dawa hizo aina ya bangi.

MWANANCHI
 
Upumbavu mfu!hata Hakimu aliyetoa hukumu apimwe akili,bangi siyo sehemu ya matatizo ambayo ni tangible Kwa ustawi wa nchi.Hukumu zitolewe kulingana na vihatarishi vya uharifu,mnamkosea Sana kuanzia utungaji wa Sheria Hadi utekelezaji wa Sheria,dunia imebadilika Sana,bangi haipo tena kwenye category ya madawa ya kulevya...Mytake:Huyu kijana Yuko na familia inayomtegemea,anavuta bangi Kwa starehe zake,leo anaibuka Hakimu anampangia mahala pa kuishi Maisha yake yote..Hakimu naye ni binadamu ,ufike mahala tuheshimu utu kuliko vyeo tulivyonavyo na mamlaka ya kupita,nimeumia Sana Kwa hii hukumu..🙏🙏🙏
 
Hivi vichwa vya habari bana,Kuna habari Moja ilisomeka matumdu mawili ya choo watoto 400 alafu picha ya mweheshimiwa akichungulia Tundu la choo
 
Wamemuonea tu bangi haina hatari kama rushwa, dunia imebadilika wao wanalazimisha mrungi na bangi bado ionekane ni madawa ya kulevya hapana sio sawa
 
Back
Top Bottom