Mtwara: Rais Samia awaleta Essa Group wa Indonesia kujenga Kiwanda cha mbolea kwa Trilioni 3.2

Mtwara: Rais Samia awaleta Essa Group wa Indonesia kujenga Kiwanda cha mbolea kwa Trilioni 3.2

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Matunda ya ziara ya Rais Samia Nchini Indonesia na Yale ya Rais wa Indonesia hapa Tanzania yamezaa matunda Kwa Wana Mtwara.

Ambapo kampuni ya kutoka Indonesia ya Essa Group of Industries imesaini MoU na Tanzania Kupitia TIC tayari kuanza uwekezaji wa Ujenzi wa kiwanda kikubwa Cha Mbolea Afrika chenye thamani ya $1.2 Bilioni( sawa na Shilingi Trilioni 3.2) ambacho Kitakuwa na uwezo wa Kuzalisha zaidi ya Tani Milioni 1 za mbolea ya Urea Kwa kutumia gesi ya Mtwara.👇👇

----
Ziara ya Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Nchini Indonesia yazaa matunda, Waziri Mhe. Prof. Kitila Mkumbo ashuhudia utiaji saini makubaliano ya ujenzi kiwanda kikubwa cha Mbolea Nchini

"Kuanzishwa kwa kiwanda hichi (kiwanda cha kuzalisha mbolea kitakachotumia gesi ambacho kinatarajiwa kujengwa mkoani Mtwara na wamiliki wake ni kampuni ya Essa group kutoka nchini Indonesia) ambacho tunatarajia kinaweza kikaanza rasmi kufanya production mwaka 2029 au kabla ya hapo, tunategemea sasa tutakuwa na uwezo wa uzalishaji wa mbolea ambazo zinaweza kusaidia kukidhi mahitaji ya ndani na kufikia ile azma yetu ya ajenda 10/30" -Joel

Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa mbolea Tanzania (TFRA) Joel Laurent amezungumza hayo mbele ya wanahabari leo, Jumatano Julai 31.2024 muda mfupi baada ya kushudiwa kwa utiaji saini wa uwekezaji wa mradi wa ujenzi wa kiwanda cha mbolea mkoani Mtwara, hafla iliyofanyika Regency Hotel, jijini Dar es Salaam

Imeelezwa kuwa kukamilika kwa mradi wa kiwanda cha kuzalisha mbolea kinachotarajiwa kujengwa mkoani Mtwara na kampuni ya Essa group kutoka nchini Indonesia kutapelekea kuzalisha tani za mbolea takribani milioni moja kwa mwaka, jambo ambalo litatengeneza ziada ya kuuza nje ya nchi kwa kuwa mahitaji ya nchi ni tani laki nane na elfu hamsini

Hayo yameelezwa na Abdallah Saad Kitete ambaye ni Mwakilishi mkazi wa kampuni ya Essa group alipozungumza na wanahabari leo, Jumatano Julai 31.2024, muda mfupi baada ya kushuhudiwa utiaji saini wa kiwanda hicho kitakachotumia gesi, hafla hiyo imefanyika Regency Hotel, jijini Dar es Salaam

Chanzo: Jambo online

My Take
Alifanya JK Kwa Ajili ya Wana mtwara kwa.kumleta Dangote na Sasa anafanya Rais Samia.

Ikumbukwe hiki Kitakuwa kiwanda Cha pili Cha Mbolea ambacho kina Ushawishi wa Moja kwa Moja wa Rais Samia, kingine ni intracom fertilizer company ltd Dodoma ambacho Rais Samia aliwashawishi Kampuni ya Burundi kujenga kiwanda Dodoma.

Hongera sana Rais Samia, juhudi zako huko kwenye ziara zinaonekana wazi.

View: https://www.instagram.com/reel/C-ID4MoO5gE/?igsh=MXMzeTVvcThqM3M3Ng==

Pia soma Rais Samia anatafsiri Tanzania ya viwanda kwa vitendo

Zaidi soma Mafanikio ya Rais Samia katika kujenga Tanzania ya Viwanda yaanza kuzaa matunda
 
Hivi kiwanda cha mijingu na kile cha Dodoma si wanzalisha mbolea?mbona wanauza nhmje kwa sbb soko la ndani hakuna? Na je Hawa watafanyaje kupata soko la uhakika kama waliopo wanapata changamato ya kuuza mbolea
Hakuna kilichoharibika,in fact tunahitaji wauze Nje zaidi kuliko hata ndani.
 
Hivi kiwanda cha mijingu na kile cha Dodoma si wanzalisha mbolea?mbona wanauza nhmje kwa sbb soko la ndani hakuna? Na je Hawa watafanyaje kupata soko la uhakika kama waliopo wanapata changamato ya kuuza mbolea
Mbolea ziko aina mingi mkuu.
 
Nakumbuka ilikuwa wakati wa utawala wa magufuli wananchi walishatoa ardhi yao bure ili kijengwe kiwanda cha mbolea nadhani ndio hawa
Toa ujinga wako hapa,unapozungumzia biashara na uwekezaji usimtaje huyo mtu wako unakimbusha maumivu Kwa wengi.

Huyo alitaka kufanya Dangote afunge kiwanda kama sio busara za JK kumsihi avumilie.
 
Toa ujinga wako hapa,unapozungumzia biashara na uwekezaji usimtaje huyo mtu wako unakimbusha maumivu Kwa wengi.

Huyo alitaka kufanya Dangote afunge kiwanda kama sio busara za JK kumsihi avumilie.
Mimi sio chawa kama wewe na mimi ni mtu timamu na sivizii teuzi wala siongozwi na hisia za kidini kama wewe...ninachokueleza ni jambo ambalo kila mwana mtwara analijua tangu utawala uliopita kuhusu ujenzi wa kiwanda cha mbolea...ni wakati upi wananchi hawajawahi kupitia maumivu? Korosho msimu uliopita watu wamelipwa 900 kwa kilo sasa mwananchi kama huyu anaamini tatizo ni raisi aliyopo
 
Mimi sio chawa kama wewe na mimi ni mtu timamu na sivizii teuzi wala siongozwi na hisia za kidini kama wewe...ninachokueleza ni jambo ambalo kila mwana mtwara analijua tangu utawala uliopita kuhusu ujenzi wa kiwanda cha mbolea...ni wakati upi wananchi hawajawahi kupitia maumivu? Korosho msimu uliopita watu wamelipwa 900 kwa kilo sasa mwananchi kama huyu anaamini tatizo ni raisi aliyopo
Kiwanda kipi? Toka 2016 ni hizo Hadithi tuu.

Mwekezaji wa kwanza ambae ilikuwa ajenge alishindwana na Mwendazake,huyu ni mwingine na sio kwamba Wananchi wametia sijui eneo Bure Bali wamelipwa fidia kuposha hiyo ni kongani ya viwanda hapo Mtwara.

Vingine vingi hasa vya korosho vinakuja.

Mengine ukiyoandika ni upuuzi tuu.Mwisho mipango sio matumizi na maneno matupu hayajengi ghorofa
 
Kiwanda kipi? Toka 2016 ni hizo Hadithi tuu.

Mwekezaji wa kwanza ambae ilikuwa ajenge alishindwana na Mwendazake,huyu ni mwingine na sio kwamba Wananchi wametia sijui eneo Bure Bali wamelipwa fidia kuposha hiyo ni kongani ya viwanda hapo Mtwara.

Vingine vingi hasa vya korosho vinakuja.

Mengine ukiyoandika ni upuuzi tuu.Mwisho mipango sio matumizi na maneno matupu hayajengi ghorofa
Kumbe unakiri kuwa kuna mipango ya kwenye makaratasi na kuna utekelezaji kwa vitendo?
 
Matunda ya ziara ya Rais Samia Nchini Indonesia na Yale ya Rais wa Indonesia hapa Tanzania yamezaa matunda Kwa Wana Mtwara.

Ambapo kampuni ya kutoka Indonesia ya Essa Group of Industries imesaini MoU na Tanzania Kupitia TIC tayari kuanza uwekezaji wa Ujenzi wa kiwanda kikubwa Cha Mbolea Afrika chenye thamani ya $1.2 Bilioni( sawa na Shilingi Trilioni 3.2) ambacho Kitakuwa na uwezo wa Kuzalisha zaidi ya Tani Milioni 1 za mbolea ya Urea Kwa kutumia gesi ya Mtwara.👇👇

----
Ziara ya Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Nchini Indonesia yazaa matunda, Waziri Mhe. Prof. Kitila Mkumbo ashuhudia utiaji saini makubaliano ya ujenzi kiwanda kikubwa cha Mbolea Nchini

"Kuanzishwa kwa kiwanda hichi (kiwanda cha kuzalisha mbolea kitakachotumia gesi ambacho kinatarajiwa kujengwa mkoani Mtwara na wamiliki wake ni kampuni ya Essa group kutoka nchini Indonesia) ambacho tunatarajia kinaweza kikaanza rasmi kufanya production mwaka 2029 au kabla ya hapo, tunategemea sasa tutakuwa na uwezo wa uzalishaji wa mbolea ambazo zinaweza kusaidia kukidhi mahitaji ya ndani na kufikia ile azma yetu ya ajenda 10/30" -Joel

Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa mbolea Tanzania (TFRA) Joel Laurent amezungumza hayo mbele ya wanahabari leo, Jumatano Julai 31.2024 muda mfupi baada ya kushudiwa kwa utiaji saini wa uwekezaji wa mradi wa ujenzi wa kiwanda cha mbolea mkoani Mtwara, hafla iliyofanyika Regency Hotel, jijini Dar es Salaam

Imeelezwa kuwa kukamilika kwa mradi wa kiwanda cha kuzalisha mbolea kinachotarajiwa kujengwa mkoani Mtwara na kampuni ya Essa group kutoka nchini Indonesia kutapelekea kuzalisha tani za mbolea takribani milioni moja kwa mwaka, jambo ambalo litatengeneza ziada ya kuuza nje ya nchi kwa kuwa mahitaji ya nchi ni tani laki nane na elfu hamsini

Hayo yameelezwa na Abdallah Saad Kitete ambaye ni Mwakilishi mkazi wa kampuni ya Essa group alipozungumza na wanahabari leo, Jumatano Julai 31.2024, muda mfupi baada ya kushuhudiwa utiaji saini wa kiwanda hicho kitakachotumia gesi, hafla hiyo imefanyika Regency Hotel, jijini Dar es Salaam

Chanzo: Jambo online

My Take
Alifanya JK Kwa Ajili ya Wana mtwara kwa.kumleta Dangote na Sasa anafanya Rais Samia.

Ikumbukwe hiki Kitakuwa kiwanda Cha pili Cha Mbolea ambacho kina Ushawishi wa Moja kwa Moja wa Rais Samia, kingine ni intracom fertilizer company ltd Dodoma ambacho Rais Samia aliwashawishi Kampuni ya Burundi kujenga kiwanda Dodoma.

Hongera sana Rais Samia, juhudi zako huko kwenye ziara zinaonekana wazi.

Pia soma Rais Samia anatafsiri Tanzania ya viwanda kwa vitendo

Zaidi soma Mafanikio ya Rais Samia katika kujenga Tanzania ya Viwanda yaanza kuzaa matunda
Uwekezaji wa awamu ya sita uliofanikiwa ni do world tu na kwasababu hawajawekeza pesa yoyote zaidi ya kuleta management yao na kuanza kuvuna pesa
 
Back
Top Bottom