Mtwara: TAKUKURU Yamfikisha Mahakamani Hakimu Mkazi, Mussa Esanju kwa Tuhuma za Kupokea Rushwa

Mtwara: TAKUKURU Yamfikisha Mahakamani Hakimu Mkazi, Mussa Esanju kwa Tuhuma za Kupokea Rushwa

Boss la DP World

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2021
Posts
2,318
Reaction score
8,464
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mtwara, imemfikisha Mahakamani, Hakimu Mkazi wa Mtwara, Mussa Esanju kwa tuhuma za kupokea rushwa ya kiasi cha Sh. 50,000 kutoka kwa Mtuhumiwa mmoja aliyefikishwa mbele yake.

Hakimu Mussa amefikishwa Mahakamani na kusomewa makosa mawili ambayo ni kushawishi kuomba fedha Tsh. 200,000 na kupokea Tsh. 50,000, amesomewa makosa hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mtwara, Lucas Jang’andu.

Kwa upande wake Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Mtwara, Enock Ngailo amesema Mtuhumiwa alikamatwa Aprili 5, mwaka huu eneo la Mangamba Tanki la Maji majira ya saa mbili usiku, akiwa na fedha ambazo ziliandaliwa maalum na mamlaka hiyo, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mlalamikaji.

Mshtakiwa baada ya kusomewa mashtaka amekana na kuachiwa kwa dhamana na kesi hiyo itatajwa tena May 18, mwaka huu.
 
Kesi zao nyingi ni za wizi wa vidonge kumi vya panadol na rushwa kwa Mahakimu report ya CAG wanaiangalia kama vile haiwahusu wangekuwa wanafanya kazi kwa weredi hizo kesi za bamia tusingezisikia leo hii tungeona wapo busy na hao wezi waliopeleka hela USA kutunza vyura..
IMG-20230408-WA0002.jpg
 
Hii taasisi ivunjwe..hakuba cha msingi inachofanya, ufisadi na rushwa nzito nzito inakuwa kimya..hizi za wananchi wadogowadogo..ndo iko mbele..
 
Hii taasisi ivunjwe..hakuba cha msingi inachofanya, ufisadi na rushwa nzito nzito inakuwa kimya..hizi za wananchi wadogowadogo..ndo iko mbele..

Inawezekana rushwa za mabilioni hazimo kwenye JDs zao
 
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mtwara, imemfikisha Mahakamani, Hakimu Mkazi wa Mtwara, Mussa Esanju kwa tuhuma za kupokea rushwa ya kiasi cha Sh. 50,000 kutoka kwa Mtuhumiwa mmoja aliyefikishwa mbele yake.

Hakimu Mussa amefikishwa Mahakamani na kusomewa makosa mawili ambayo ni kushawishi kuomba fedha Tsh. 200,000 na kupokea Tsh. 50,000, amesomewa makosa hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mtwara, Lucas Jang’andu.

Kwa upande wake Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Mtwara, Enock Ngailo amesema Mtuhumiwa alikamatwa Aprili 5, mwaka huu eneo la Mangamba Tanki la Maji majira ya saa mbili usiku, akiwa na fedha ambazo ziliandaliwa maalum na mamlaka hiyo, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mlalamikaji.

Mshtakiwa baada ya kusomewa mashtaka amekana na kuachiwa kwa dhamana na kesi hiyo itatajwa tena May 18, mwaka huu.
🤣🤣🤣
 
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mtwara, imemfikisha Mahakamani, Hakimu Mkazi wa Mtwara, Mussa Esanju kwa tuhuma za kupokea rushwa ya kiasi cha Sh. 50,000 kutoka kwa Mtuhumiwa mmoja aliyefikishwa mbele yake.

Hakimu Mussa amefikishwa Mahakamani na kusomewa makosa mawili ambayo ni kushawishi kuomba fedha Tsh. 200,000 na kupokea Tsh. 50,000, amesomewa makosa hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mtwara, Lucas Jang’andu.

Kwa upande wake Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Mtwara, Enock Ngailo amesema Mtuhumiwa alikamatwa Aprili 5, mwaka huu eneo la Mangamba Tanki la Maji majira ya saa mbili usiku, akiwa na fedha ambazo ziliandaliwa maalum na mamlaka hiyo, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mlalamikaji.

Mshtakiwa baada ya kusomewa mashtaka amekana na kuachiwa kwa dhamana na kesi hiyo itatajwa tena May 18, mwaka huu.
Kuna ka TAKUKURU ka kike mkoa fulani kalikua kanamchunguza mtu, jamaa akaishia kukapiga mimba na kukaoa kabisa na kesi yenyewe ikaishia hapo
 
Bila kusahau watendaji wa vijiji na kata na mambo ya Poss machine. Ati mtu anashtakiwa kwa uhujumu uchumi kwa loss ya Tsh. 300000/= kwenye poss!
 
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mtwara, imemfikisha Mahakamani, Hakimu Mkazi wa Mtwara, Mussa Esanju kwa tuhuma za kupokea rushwa ya kiasi cha Sh. 50,000 kutoka kwa Mtuhumiwa mmoja aliyefikishwa mbele yake.

Hakimu Mussa amefikishwa Mahakamani na kusomewa makosa mawili ambayo ni kushawishi kuomba fedha Tsh. 200,000 na kupokea Tsh. 50,000, amesomewa makosa hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mtwara, Lucas Jang’andu.

Kwa upande wake Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Mtwara, Enock Ngailo amesema Mtuhumiwa alikamatwa Aprili 5, mwaka huu eneo la Mangamba Tanki la Maji majira ya saa mbili usiku, akiwa na fedha ambazo ziliandaliwa maalum na mamlaka hiyo, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mlalamikaji.

Mshtakiwa baada ya kusomewa mashtaka amekana na kuachiwa kwa dhamana na kesi hiyo itatajwa tena May 18, mwaka huu.
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mtwara, imemfikisha Mahakamani, Hakimu Mkazi wa Mtwara, Mussa Esanju kwa tuhuma za kupokea rushwa ya kiasi cha Sh. 50,000 kutoka kwa Mtuhumiwa mmoja aliyefikishwa mbele yake.

Hakimu Mussa amefikishwa Mahakamani na kusomewa makosa mawili ambayo ni kushawishi kuomba fedha Tsh. 200,000 na kupokea Tsh. 50,000, amesomewa makosa hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mtwara, Lucas Jang’andu.

Kwa upande wake Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Mtwara, Enock Ngailo amesema Mtuhumiwa alikamatwa Aprili 5, mwaka huu eneo la Mangamba Tanki la Maji majira ya saa mbili usiku, akiwa na fedha ambazo ziliandaliwa maalum na mamlaka hiyo, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mlalamikaji.

Mshtakiwa baada ya kusomewa mashtaka amekana na kuachiwa kwa dhamana na kesi hiyo itatajwa tena May 18, mwaka huu.

 
Taasisi nyingi za serikali nchini, hazijitambui.
 
Back
Top Bottom