Mtwara: Wananchi watamkumbuka Byakanwa kwa kusimamia usafi wa fukwe

Mtwara: Wananchi watamkumbuka Byakanwa kwa kusimamia usafi wa fukwe

DustBin

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2021
Posts
609
Reaction score
604
Mimi niliwahi kusoma ktk moja ya shule za huko mkoani Mtwara. Hivyo naijua kiasi hasa pale Mtwara mjini. Enzi zile bahari na ufukwe ulikua mchafu sana. Yaani ilikua unaenda pale kivukoni (kivuko cha msanga mkuu) au huku beach unakuta matakataka tu yamezagaa. Pamoja nabupepo wote wa baharini lakini ufukwe ulikua unatoa harufu mbaya.

Sasa mwaka jana mwishoni nikabahatika kutembelea Mtwara mjini, nikastaajabu sana na hali ya ufukwe ilivyo safi, kuanzia pale Mikindan. Ikanilazimu niende kule kwenye soko la samaki nikajiridhishe nikakuta hali ya mazingiza ni safi tena safi sana, hamna uchafu uliokua unazagaa zagaa kwenye fukwe za Mtwara. Moja kwa moja nikasema haya ni matokeo ya kazi ya RC hapa. Itakua hili suala amelivalia njuga na hakika amefanikiwa.

Kwa hili, nasema wana Mtwara watamkumbuka sana Byakanwa..!!
 
Una bahati hukusomea Simiyu au Dodoma mpya ya Mtaka...usingepata ata huo muda wa kwenda Fukweni..we ungekua unaamkia Darasani mpaka Giza ndio utoke😂😂
 
Ulijaribu kutafiti kama hicho unachokisema ni matokeo ya usimamizi makini wa Byakanwa, au ndo mwendelezo wa kuimba mapambio...
 
Una bahati hukusomea Simiyu au Dodoma mpya ya Mtaka...usingepata ata huo muda wa kwenda Fukweni..we ungekua unaamkia Darasani mpaka Giza ndio utoke😂😂
Hhahahhhahaaa...! Wewe una jambo na kina Anthony sio bure
 
Ulijaribu kutafiti kama hicho unachokisema ni matokeo ya usimamizi makini wa Byakanwa, au ndo mwendelezo wa kuimba mapambio...
Yeye ana mkono wake kwenye hilo. Nyumba ikipendeza anasifiwa mwenye nyumba hata kama wanaofanya usafi ni wapangaji
 
Kama kakutuma huyo Byakanwa mwambie imebuma , kimsingi yule alikua RC bogus kupitiliza kuliko wote waliowahi kupita mkoa ule , yaani mtu alikua siju DC anapandishwa cheo tu kwasababu kavuruga shamba la mpinzani na kuharibu mali zake, tunasemaga malipo ni hapahapa duniani na huo ndio ukweli
 
Yeye ana mkono wake kwenye hilo. Nyumba ikipendeza anasifiwa mwenye nyumba hata kama wanaofanya usafi ni wapangaji
Vipi kama ni jitihada za wizara ya uvuvi na mambo ya mazingira, umeshawasifia mawaziri kwenye wizara hizo.......au hii ngoma ni mahsusi kwa Byakanwa.....
 
Kama kakutuma huyo Byakanwa mwambie imebuma , kimsingi yule alikua RC bogus kupitiliza kuliko wote waliowahi kupita mkoa ule , yaani mtu alikua siju DC anapandishwa cheo tu kwasababu kavuruga shamba la mpinzani na kuharibu mali zake, tunasemaga malipo ni hapahapa duniani na huo ndio ukweli
Hajanituma na sijawahi kuonana nae zaidi ya kumuona videoni. Lakini alichojitahidi kukisimamia vizuri sio dhambi kusifu..!!
 
Vipi kama ni jitihada za wizara ya uvuvi na mambo ya mazingira, umeshawasifia mawaziri kwenye wizara hizo.......au hii ngoma ni mahsusi kwa Byakanwa.....
Nikibainikiwa kuwa hili nililolisema yeye hakuhusika ktk kulisimamia nitaomba radhi kwa walionielewa vibaya. Kama walivyifanya watangulizi wangu kina anton. Hahahhhh
 
Back
Top Bottom