Muda Mfupi Watanzania Huenda wamemsahau Warioba na Tume Yake

Muda Mfupi Watanzania Huenda wamemsahau Warioba na Tume Yake

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
14,242
Reaction score
34,903
Rasimu ya warioba ingejibu kero nyingi

Ni muda mfupi,watanzania huenda wamemsahau Warioba na tume yake.

Lakini ili ujue ubora wa timu hii, jaribu kupitia Randama ya katiba na katiba pendekezwa ni tofauti kabisa,Rasimu ya warioba ilijibu kero nyingi.

Mfano baadhi ya mambo mazito yaliyojadiliwa humo nihaya;

ZAWADI
Mtumishi wa umma hataruhusiwa kupokea zawadi,akiwa kwenye shughuli za serikali akapewa zawadi,zawadi hiyo itakuwa mali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo itakabidhiwa kwa katibu Mkuu kiongozi au wa wizara husika.ibara ya 15

Kufungua akaunti nje

Kiongozi wa umma,hataruhusiwa kumiliki au kuweka fedha kwenye akaunti nje ya nchi,isipokuwa sheria itakavyoelekeza

Ibara ya 88(1)
Rais anaweza kushitakiwa iwapo tu atapuuz au kukataa kutekeleza uamuzi au amei ya mahakama.
Au amepokea rushwa.


Wajumbe wa bunge la Muungano

Kutakuwa na wabunge sabini wa kuchaguliwa,na wabunge watano wenye ulemavu,katika kila jimbo wabunge watagombea wawili mwanaume na mwanamke.

Mamlaka ya kukopa
Serikali itaweza kukopa,lakini kifungu ( b),kinasema itaweka ukomo wa deni la Taifa na madhumuni ya kukopa.

Vyombo vya usalama

Viliwekwa wazi kuwa kutakuwa na vyombo vya usalama,vyombo hivi ni jwtz,jeshi la polisi,usalama wa Taifa na wajibu wao,katika shughuli zao hawataruhusiwa;
Kuwa na upendeleo,
Kuendeleza maslahi ya kisiasa ya chama chichote,

Kuhujumu maslahi ya kisiasa au mpango wa kisiasa ambao ni halali kwa mujibu wa katiba hii.


Kutishia,kudhulumu au kuwatendea ukatili raia na wengine.

Mamlaka ya kuwajibisha mbunge
Ibara ya 129(1), inawapa mamlaka wananchi kumwajibisha mbunge wao,endapo tu,atafanya haya,
Kuunga mkono sera ambazo zinaenda kinyume na maslahi ya wapigakura au kinyume na maslahi ya Taifa,au
Kushindwa kuwasilisha au kutetea kwa dhati,hoja zinazorokana na kero za wapigakura au kuacha kuishi au kuhama eneo lake la kazi.

Yapo mengi ambayo ni wazi kuwa Taifa kupitia pendekezo hayo ni dhahiri Taifa hili lilikuwa mfano wa kuigwa

Mwanahabari Huru
 
Rasimu ya warioba ingejibu kero nyingi

Ni muda mfupi,watanzania huenda wamemsahau Warioba na tume yake.

Lakini ili ujue ubora wa timu hii, jaribu kupitia Randama ya katiba na katiba pendekezwa ni tofauti kabisa,Rasimu ya warioba ilijibu kero nyingi.

Mfano baadhi ya mambo mazito yaliyojadiliwa humo nihaya;

ZAWADI
Mtumishi wa umma hataruhusiwa kupokea zawadi,akiwa kwenye shughuli za serikali akapewa zawadi,zawadi hiyo itakuwa mali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo itakabidhiwa kwa katibu Mkuu kiongozi au wa wizara husika.ibara ya 15

Kufungua akaunti nje

Kiongozi wa umma,hataruhusiwa kumiliki au kuweka fedha kwenye akaunti nje ya nchi,isipokuwa sheria itakavyoelekeza

Ibara ya 88(1)
Rais anaweza kushitakiwa iwapo tu atapuuz au kukataa kutekeleza uamuzi au amei ya mahakama.
Au amepokea rushwa.


Wajumbe wa bunge la Muungano

Kutakuwa na wabunge sabini wa kuchaguliwa,na wabunge watano wenye ulemavu,katika kila jimbo wabunge watagombea wawili mwanaume na mwanamke.

Mamlaka ya kukopa
Serikali itaweza kukopa,lakini kifungu ( b),kinasema itaweka ukomo wa deni la Taifa na madhumuni ya kukopa.

Vyombo vya usalama

Viliwekwa wazi kuwa kutakuwa na vyombo vya usalama,vyombo hivi ni jwtz,jeshi la polisi,usalama wa Taifa na wajibu wao,katika shughuli zao hawataruhusiwa;
Kuwa na upendeleo,
Kuendeleza maslahi ya kisiasa ya chama chichote,

Kuhujumu maslahi ya kisiasa au mpango wa kisiasa ambao ni halali kwa mujibu wa katiba hii.


Kutishia,kudhulumu au kuwatendea ukatili raia na wengine.

Mamlaka ya kuwajibisha mbunge
Ibara ya 129(1), inawapa mamlaka wananchi kumwajibisha mbunge wao,endapo tu,atafanya haya,
Kuunga mkono sera ambazo zinaenda kinyume na maslahi ya wapigakura au kinyume na maslahi ya Taifa,au
Kushindwa kuwasilisha au kutetea kwa dhati,hoja zinazorokana na kero za wapigakura au kuacha kuishi au kuhama eneo lake la kazi.

Yapo mengi ambayo ni wazi kuwa Taifa kupitia pendekezo hayo ni dhahiri Taifa hili lilikuwa mfano wa kuigwa

Mwanahabari Huru

Nitaipata wapi hiyo randama ?
 
Mwanahabari Huru,hivi bado unaamini katika Katiba mpya?Maana naona kila anayepewa nakala hizi anatusomea kama vile tunasikiliza HADITHI za SHIGONGO!

Hakuna mwanasheria mwelekezaji anayezielezea maana ya kilichoandikwa,hakuna wakutupa nafasi kujua tofauti za hivi vitabu viwili,basi ni shida tu,nafuu ile ya mwaka 1947 iendelee.
 
yaani seriously umeamua kuchukua kijisehemu tu cha hiyo katiba ili uwapotoshe watu.......fikiria mazuri yako mangapi na mabaya yako mangapi na effect za mazuri na mabaya hayo....sio unaongea ongea tu kuchochea watu wasiwe na amani.......
 
Kwa kiasi fulani hata yeye Warioba mwenyewe ameisahau.
 
Wakuu
Mngetegemea Chenge awalete katiba itakayo mkaba koo?
Tunachotakiwa kukifanya ni kuuelimisha umma kuhusu mapungufu tunayoyaona kabla ya kura ya maoni.
Wananchi wengi hawajui chochote na hao ndo wanalegwa wabuluzwe kupiga kura ya ndiyo, lakini elimishwa hawatabuluzwa tena. Tumeona mwamko wao hasa kwenye chaguzi zilizopita.
 
yaani seriously umeamua kuchukua kijisehemu tu cha hiyo katiba ili uwapotoshe watu.......fikiria mazuri yako mangapi na mabaya yako mangapi na effect za mazuri na mabaya hayo....sio unaongea ongea tu kuchochea watu wasiwe na amani.......

Hoja ipo hapo,wewe tuletee yale ambayo yanachochea watu,wasiwe na amani tutakuletea yote hata usiyopenda maskio yao kuyasikia na ukisyasikia maskio yanakuwasha
 
yaani seriously umeamua kuchukua kijisehemu tu cha hiyo katiba ili uwapotoshe watu.......fikiria mazuri yako mangapi na mabaya yako mangapi na effect za mazuri na mabaya hayo....sio unaongea ongea tu kuchochea watu wasiwe na amani.......

We tuletee sehemu ya ubaya wa hiyo randama tuuone hapa. Sio Maneno bila mfano.
 
Afadhali umelijua hili na bora watazame jambo lililombele yao, tume ya Warioba ilimaliza kazi yake na kuliachia Bunge Maalum la Katiba (BMK) iliyoletwa ndio hiyo sasa unataka nini tena? mie nasubiri tarehe ya kupiga kula nikapige zangu.
 
yaani seriously umeamua kuchukua kijisehemu tu cha hiyo katiba ili uwapotoshe watu.......fikiria mazuri yako mangapi na mabaya yako mangapi na effect za mazuri na mabaya hayo....sio unaongea ongea tu kuchochea watu wasiwe na amani.......

Hakuna hata chembe ya upotoshaji hapa ndugu, kasema ukweli mtupu! Jibu hoja zake acha siasa! Katiba ni moyo wa taifa letu sote, itikadi yako ya kifisadi inakufanya ujenge hofu ya rasimu ya Warioba kwa sababu inabana wewe na team yako na kuiba hutaki kuacha umefanya jadi ya chama chako.
 
Back
Top Bottom