Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,903
Kwa hali inayoendelea sasa nchini na ndani ya CCM, sio tu kunaua upinzani lakini pia inadhohofisha vyama vyote mpaka CCM yenyewe na hilo halina ubishi.
JPM na Polepole hawaamini katika siasa za ushindani, wao wanaamini katika siasa za ushindi wa mezani ambazo katika ulimwengu wa sasa hazina nafasi kwa kuwa maisha ya siasa hizo huwa sio ya muda mrefu.
JPM na Polepole wanaamini zaidi katika wao na hawaamini katika kutengeneza mfumo ili wanachokifanya kiwe na muendelezo, wao wapo tayari kufanya hata lisilo na faida mradi wapate umaarufu wa muda lakini wanasahau kuwa ukweli ni kama jua hivyo huna uwezo wa kulifunika, lazima litaonekana tu.
Mfano: shambulio la lisu, ununuzi wa madiwani, ujenzi wa uwanja 2a ndege Chato, manunuzi ya ndege, skendo ya vitambulisho vya utaifa, swala la makinikia, upotevu wa trillion 1.5 na mengine mengi, ipo siku haya mambo yatakuwa hadharani na watu watawadharau sana.
Ccm kimekuwa chama cha waoga, watu wote wanaendeshwa na watu wawili, na wao hawana chochote cha kuongea ingawa wanakufa kisabuni, wakati umefika sasa kwa CCM nchi nzima kuazimia kuwafuta uanachama JPM na Polepole kuliko kukiua chama kama wanavyofanya.
Pia, ndani ya CCM walikuwa na hazina kubwa ya watu waliofanya kazi 2015 kama kina Shaka wa UVCCM, lakini ukuu wa wilaya anakuja kupata katambi wa chadema, hii ni aibu kubwa kwa chama tawala, hasa kwa kutowathamini watu wao kwa sifa za watu wachache ambao wanaendekeza maslahi yao binafsi.
JPM na Polepole hawaamini katika siasa za ushindani, wao wanaamini katika siasa za ushindi wa mezani ambazo katika ulimwengu wa sasa hazina nafasi kwa kuwa maisha ya siasa hizo huwa sio ya muda mrefu.
JPM na Polepole wanaamini zaidi katika wao na hawaamini katika kutengeneza mfumo ili wanachokifanya kiwe na muendelezo, wao wapo tayari kufanya hata lisilo na faida mradi wapate umaarufu wa muda lakini wanasahau kuwa ukweli ni kama jua hivyo huna uwezo wa kulifunika, lazima litaonekana tu.
Mfano: shambulio la lisu, ununuzi wa madiwani, ujenzi wa uwanja 2a ndege Chato, manunuzi ya ndege, skendo ya vitambulisho vya utaifa, swala la makinikia, upotevu wa trillion 1.5 na mengine mengi, ipo siku haya mambo yatakuwa hadharani na watu watawadharau sana.
Ccm kimekuwa chama cha waoga, watu wote wanaendeshwa na watu wawili, na wao hawana chochote cha kuongea ingawa wanakufa kisabuni, wakati umefika sasa kwa CCM nchi nzima kuazimia kuwafuta uanachama JPM na Polepole kuliko kukiua chama kama wanavyofanya.
Pia, ndani ya CCM walikuwa na hazina kubwa ya watu waliofanya kazi 2015 kama kina Shaka wa UVCCM, lakini ukuu wa wilaya anakuja kupata katambi wa chadema, hii ni aibu kubwa kwa chama tawala, hasa kwa kutowathamini watu wao kwa sifa za watu wachache ambao wanaendekeza maslahi yao binafsi.