Muda wa kumuonesha trafiki leseni ni mpaka siku tatu kama umesimamishwa na huna

Usip
Usipotoshe watu kwa uanasheria uchwara, kama leseni ni ya kuendesha gari, kila uendeshapo unapaswa kuwa nayo. Kama kila dereva ataacha leseni yake nyumbani ili aipeleke traffic ndani ya siku tatu, traffic atatofautishaje dereva mwenye leseni na asiye nayo?, Asiye na leseni sukuma ndani, aliyeisahau, sukuma ndani pia
 
Naomba hio sheria ya barabarani natamani sana kwa kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante sana
 
ukikataa kulipa faini unaenda kupaki gari yako kituo cha polisi, wanakuambia mpaka muende mahakamani ukishinda hiyo kesi ndo hutolipa faini na hapo ndo utaruhusiwa kuchukua gari yako. wengine hatupendi huo usumbufu, unaweza kushinda hiyo kesi yako lakini ukija kuchukua gari yako kituoni unakuta imegeuka screpa, wameshanyofoa betri n.k
 
Asante, ila kuna vipengele kidekede vya sheria za barabarani kwa waendesha vyombo vya moto trafiki wetu wanatuonea, ni vingi mno, mpaka wajihisi wanajiona mitu miungu, wanadhalilisha, kuonea, na kutudharau sana kwa kweli..
 
Tupe ukweli au uwongo wa kifungu alichotoa cha 71, tujue unachosema kama nikweli au laa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tupe ukweli au uwongo wa kifungu alichotoa cha 71, tujue unachosema kama nikweli au laa

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe kama una leseni hai ya udereva na una gari, hakikisha unakuwa nayo kabla ya kuingia barabarani ili uionyeshe pale itakapohitajika. Hii ligi ya mchangani unayotaka kuanzisha haitakusaidia kwa kuwa wewe na mimi hatutungi sheria, ama kama wewe ni mwanasheria,katafute tafsiri yake mahakamani.
 

Hizo siku tatu mnakua mpo na huyo polisi hapo alipokumatia au mnaenda naye nyumbani kwako?
 
Pia unachotakiwa ni kumwonyesha leseni. Siyo yeye kuichukua. Aione tu na si kuishika. Unaweza kumwonyesha hata bila kushusha kioo!
 
Tatizo mnapangaje kuonana ndani ya hizo siku tatu?
Tatizo mnapangaje kuonana ndani ya hizo siku tatu?

Polisi atachukua taarifa zako na za gari yako unaloendesha na atakupa notification kuku - notify kuwa una tuhuma za kudraivu chombo cha moto bila leseni na hivyo kukutaka uthibitishe kuwa you are licensed ila umeisahau tu leseni yako....

Tuchukulie mfano umekamatiwa Mbeya nawe unaishi Mwanza na kwa wakati huo ndo uko safarini njiani kuelekea Mwanza nyumbani kwako iliko leseni unayodai umeisahau...

Utakachotakiwa kufanya ni mara ufikapo nyumbani, chukua leseni yako na ripoti kituo cha polisi kilicho karibu nawe waoneshe notification uliyopewa Mbeya na leseni yako ikiwa valid, kosa litajifuta mara hiyo...

Nadhani ni rahisi tu kwa jinsi hiyo.

Lakini tatizo ninaloliona mimi ni uelewa wa pande zote mbili na hususani upande wa polisi na hasa polisi wetu hawa wa leo na kwa tabia yao hiyo wamewafanya hata raia nao kuwa kichwa ngumu kiasi ambacho mnapokutana barabarani ni kutunishiana misuri tu...
 
Sect 87 RTA...."A police officer may after stopping any motor vehicle or trailer which he reasonably suspects of being or having been (driving without having d/licence) or used or involved in the commission of an offence , whether under this act or any other written law, order the driver thereof to drive it to the nearest convenient police station in order that....."

Sect 87 (d) RTA...."statement relevant to the suspected offence (failing to produce a d/licence for inspection as per sect 77 RTA) may be obtained and such vehicle may be detained until all necessary inquiries have been made in relation to the case ( kuileta leseni yake baada ya masaa 72 ( siku 3).

Sect 88 RTA....."No person shall make any statement when required to do so under this part which to his knowledge is false or in any respect misleading ..." utakuwa umetenda kosa kwa maana kwamba umepewa siku 3 kuleta/ kuonesha leseni yako ukijuwa kabisa huna/unadanganya na inapofika siku hizo unashindwa kutoa/ kuonesha leseni yako utaadhibiwa kwa kutoa taarifa ya uongo....

Sect 89 RTA , ADHABU
(a) failing to comply with or contravenes any requirement , direction or order made under this part ( kushindwa kuproduce d/licence baada ya siku 3).

(c) contravenes the provision of sect 77 RTA (kushindwa kutoa leseni kwa ukaguzi) or sect 88 RTA (kuonekana kutoa taarifa ya uongo baada ya kushindwa kuleta leseni yako baada ya masaa 3)

Adhabu yake ni kifungo kisichozidi miaka miwili jela au kulipa faini au vyote kwa pamoja

Kwa hivyo sasa .......

1. Hayo masaa 72 (siku 3) utapewa endapo utaacha gari kituoni au udhaminiwe na mtu anayefahamika katika eneo ulilokamatiwa ili uweze kwenda hizo siku 3 kuleta leseni yako (sect 87 RTA)

2. Kushindwa kutoa/kuleta na kuonesha leseni yko ndani ya siku 3 ni kuonekana umetoa taarifa ya uongo na kumletea usumbufu afisa wa polisi walipokuwa anasimamia utekelezaji wa kifungu 77 (sect 88 RTA)

3. Kosa la namna hilo adhamu yake ni kifungo miaka isiyozidi miaka 2 jela, au kulipa faini au vyote kwa pamoja ( sect 89 RTA)

TUSIKIZARAU KIFUNGU CHA 77 RTA KINA MADHARA/UKAKASI MKUBWA ENDAPO KITAVUNJWA TEMBEA NA LESENI YAKO HAI (sect 19 RTA muda wote uendeshapo chombo cha moto)



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa umemaliza kila kitu maana kuna watu wanatoa kifungu kimoja na maelezo ambayo yanaweza kuwaletea wenzao matatizo, kifungo cha miaka miwili sio mchezo na sikuizi ukionekana ulifanya makusudi alafu unajua kabisa na Nguvu unazo ukikutwa na hatia lazima faini na kifungo ili ukasaidie shughuli za kijamii au ukalime mashamba huko magereza ya kilimo

Mkorintho wa 6
 
Safi
 
Hujatembea na leseni gari unaipeleka kituoni mpaka ulete leseni, tena utawekwa na mahabusu. Sent using Jamii Forums mobile app
umesema kweli kabisa mleta Mada si DEREVA ila ni bush lawyer
km huna leseni huruhusiwi kuendesha gari na akikukuta barabarani ana haki Sheria na Wajibu wa kukuweka ndani na safari usiendelee na hata kubadili dereva hauruhusiwi km kakukamata.
Nilikamatwa Mdaula Moro -Dar nikasingiziwa Speed 52 katika eneo linaloitwa 50 ndefu nikataka nikaoneshwe mpiga picha, nikajibiwa utaenda na Askari kituoni ukalale ukisubiri kesi yako Mahakamani, hao abiria (familia yangu) watatafuta pa kulala nililipa 30,000/
vivyo hivyo Haneti Njia ya Dom Kondoa nilikuwa na 51 nikagomea leseni kuwa sina nikaambiwa acha gari upelekwe Mahakamani mbona niliitoa maana hawataki hata kueleimisha.
Madereva hawa Traffic si wa kuwafundisha huu uongo wao wameshaambiwa Poilisi akiua yupo kazini yeyote awekwe ndani
chonde chonde tembeeni na leseni kwani faini haiwezi kuandikwa bila ya jina la kwenye lessni
 
Hatari hii! Verified Member asante kwa taarifa. Ila polisi habari hii hawatapenda kusikia. Ndugu andkia Makala kwenye Gazeti mmojawapo Bongo iliwalaji /madereva waokoe 30,000/= zao maana muda mwingine mtu anasahu tu kubebea leseni lakini Jamaa hawajui hilo.
 
Ila polisi habari hii hawatapenda kusikia. Ndugu andkia Makala kwenye Gazeti mmojawapo Bongo iliwalaji /madereva waokoe 30,000/= .
ndugu yangu achana na hao wanasheria uchwara, Akwilina kapigwa risasi, Tundu Lissu na watu wamelala ndani hadi mwezi ujao ww unadanganywa na Wanasheria ambao hata Vyuo vya udereva hawajapitia au kuendesha safari ndefu wao ni kuamrisha dereva pita hapa
Mwanasheria km Bashir Yakub yeye kafukua kifungu 77 tu bila ya kukitaja kifungu 87 anavyojua ila ndani (POLISI) utalala wewe na gari yako
fuatilia post No 135 ya Mwaki Pesile vifungu hivyo vinajieleza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…