Muda wa kumuonesha trafiki leseni ni mpaka siku tatu kama umesimamishwa na huna

Mkuu unachosema ni sahihi na sheria inakutaka iwe hivyo shida ni pale utakapo pelekwa kituo cha polisi jamaa wanakuweka ndani...kwa makusudi..
 
Inategemea na u smart wa askari mwenyewe. Mi nilishakamatwa sina leseni, gari imevunjika kioo nyuma kuna nylon tu nimezibia. Akaniuliza tu una mpango gani na hiki kioo nikamwambia nimeshaagiza nakifunga soon. Leseni nikasema nimeisahau home kuna mtoto kazidiwa ndio namfuata nimuwahishe KCMC. Akanielewa sikumpa hata sh.100
 
Hapo ni sawa ila kama ametenda kosa na hajabeba leseni na taskari ameamua kukuadhibu hapo lazima atakutaka leseni ukiwa huna atakuomba namba ya leseni na kama kichwani huna hapo utaambiwa upeleke gari kituoni na ulete leseni yako kwa ajili ya taratibu zingine (ndio hizo siku tatu zinazosemwa)...kama uivyosema inatokana na u smart wa askari pia na u smart wa dereva kwa mawasiliano ya pande mbili hivyo hata kama alikuwa ana nia ya kukuadhibu alafu umesahau leseni nyumbani na jinsi mlivyowasiliana kwa nidhamu anajikuta anakuachia (kwa sababu sasa hivi leseni ni digitally hata usipoibeba wanaweza wakai-access kupitia mtandaoni)
 
Somo zuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…