Muhoozi Kainerugaba (Mtoto wa Rais Museveni) atangaza kustaafu Jeshi. Je, ni maandalizi ya kurithi kiti cha Urais?

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938

Picha: Baba(Rais), Mtoto (Luteni Jenerali), Mama (Waziri wa Elimu)

Jenerali Muhoozi Kainerugaba ni nani?​

Muhoozi Kainerugaba ni mtoto wa Rais Yoweri Museveni wa Uganda na mama Janet Museveni, ambaye ni waziri wa elimu na michezo tangu mwaka 2016.

Ni mume wa Charlotte Nankunda Kutesa aliyemuoa mwaka 1999 na mtoto wa kwanza wa Rais Museveni. Alizaliwa tarehe 24 mwezi Aprili 1974 mjini Dar es Salaam Tanzania. Akapata elimu yake ya shahada ya sayansi ya siasa kutoka chuo kikuu cha Nottingham University nchini Uingereza.

Mwaka 1999 alijiunga na jeshi la Uganda UPDF akiwa afisa kadeti na kuhitimu shahada kutoka chuo cha mafuzo ya jeshi cha Royal Military Academy Sandhurst, mwaka 2000 ambacho hutumika kwa mafunzo ya wanajeshi wa uingereza .

Kainerugaba ni miongoni mwa wanajeshi wa Uganda walipanda vyeo harakahara. Lakini kufika ngazi za juu za jeshi amepitia pakubwa. Dalili zilianza kumuendea vyema baada ya kupandishwa cheo na kuwa kapteni wa jeshi Novemba 2001, mwaka uliofuata (2002) akahudhuria mafunzo ya kuwa kamanda wa kitengo cha Jeshi (Battalion) huko nchini Misri.

Safari yake ndani ya jeshi​

Mwaka 2003 alipandishwa cheo cha kuwa Meja na kuteuliwa kuwa kamanda wa kitengo cha jeshi cha Motorised Infantry batallion, na mwanachama wa baraza kuu la ulinzi nchini Uganda.

2005: Vilevile alihudhuria mafunzo ya ngazi za juu za usimamizi wa kitengo cha jeshi katika chuo cha kaisenyi magharibi mwa Uganda.

2006: Alisimamia mafunzo na mipango ya kitengo kipya cha jeshi kwa jina 1 Command katika eneo la Barlege, kaunti ya Otuke , wilayani Lira kaskazini mwa Uganda.

2008: Julai alikuwa mganda wa kwanza kufuzu mafunzo ya kushambulia kwa kutumia parachute katika jeshi la Uganda la UPDF baada a kumaliza mafunzo yake huko Marekani. Mwaka huo huo akapandishwa cheo na kuwa Luteni kanali na kuteuliwa kuwa kamanda wa kikosi maalumu chini ya UPDF.

2010: Akateuliwa kuwa kamanda wa Kikosi maalumu ambacho sasa kinajumuisha kikosi cha ulinzi wa rais ambacho awali kilitenganishwa.

2011: Septemba akapandishwa cheo na kuwa kanali kabla ya kuwa Brigedia Jenerali.
Kuandaliwa kurithi kiti cha urais cha baba yake Museveni
Kutokana na kupandishwa vyeo harakaraka, kukazuka maneno ya kwamba anaandaliwa kuja kuwa mrithi wa Museven aliyetawala Uganda kwa zaidi ya miaka 30.

Mwezi Juni 2013 alijitokeza na kupinga tetesi hizo na kusema: "Uganda sio nchi ya kifalme ambao uongozi unarithishwa kutoka kwa baba kwenda kwa mtoto. Hili linalosemwa ni [Muhoozi] ni mradi ni maneno tu yakutungwa na watu."
Alikuja kurejea hilo la kupinga kuandaliwa kumrithi baba yake mwaka 2016 alipoteuliwa kuwa meja jenerali. Katika sherehe za uapisho wake alisema mradi wa "Muhoozi haupoi na ni maneno tu".
Kumlinda baba yake 'Rais' na nguvu 'tata' za kimamlaka alizokuwa nazo
Ni Luteni wa pili kuhudumu katika kikosi cha kumlinda rais (PPU).

Januari 2017, Muhoozi aliteuliwa kuwa mshauri wa rais wa shughuli maalumu. Kupandishwa kwake cheo na kusogezwa Ikulu, kukaongeza maneno zaidi kwenye vyombo vya habari vya Uganda kwamba Kainerugaba ni kama andaaliwa kuwa rais ajaye wa Uganda kumrithi baba yake.

2020: Rais Museveni akamteua tena kuwa kamanda wa kikosi maalumu (SFC) kumrithi Meja jenerali James Birungi. Akiendelea kuwa mshauri mwandamizi wa rais kwenye shughuli maalumu.

2021: Kabla ya June 24, kuteuliwa kuwa Kamanda wa vikosi vya ardhini akichukua nafasi ya lutein jenerali Peter Elwelu ambaye aliteuliwa kuwa mkuu wa majeshi msaidizi.

2021: Desemba alimtaka baba yake Rais Museveni kumwachia huru Inspekta wa zamani wa Polisi Jenerali Kale Kayihura. Alitumia tu mtandao wake wa twitter kufikisha ujumbe huo na miezi miwili baadaye Inspekta mstaafu huyo aliachiwa huru.
Jenerali Kayihura alikuwa ndani akiruhumiwa kwa makosa matatu: kushindwa kulinda vifaa vya vita, kusaidia na kuchochea utekaji nyara na urejeshwaji wa wakimbizi wa Rwanda nchini Uganda. Alifikishwa mahakamani Agosti mwaka 2018.

Mtoto huyu wa Rais alichapisha ujumbe kwenye mtandao wake wa twitter kuonyesha kuunga mkono uvamizi wa Urusi nchini Ukraine akiandika: "Watu wengi (ambao sio wazungu) wanaunga mkono msimamo wa Urusi nchini Ukraine. Putin yuko sahihi! Wakati USSR ilipopeleka makombora ya nyuklia nchini Cuba mwaka 1962, mataifa ya magharibi yalikuwa tayari kuilipua dunia. Wakati huu Nato inafanya hivyo hivyo wanatarajia Urusi kufanya tofauti?"


----------

President Yoweri Museveni's son and Uganda People's Defence Force's (UPDF) Commander of Land Forces Lt Gen Muhoozi Kainerugaba , has on Tuesday March 8, announced that he is retiring from the army after more than two decades of service.

Muhoozi 47 made the announcement via his tweeter handle.



"After 28 years of service in my glorious military, the greatest military in the world, I am happy to announce my retirement," the powerful Ugandan First Son wrote on Twitter, a platform that has recently become his major tool of public communication.

Muhoozi who rapidly but vertically rose through the ranks of the army March 8 said "he and his soldiers have achieved so much."

Available records indicate that Muhoozi, who if released from the army could become one of the youngest people at his rank to be granted retirement from the army, became a serviceman in 1999 as a cadet officer.

"I have only love and respect for all those great men and women that achieve greatness for Uganda everyday," the man elevated to the rank of a Major General in 2016 observed.

Mainstream social media services including Twitter and Facebook- remain dominated by messages touting First Son Muhoozi as the next Ugandan president although the 47-year-old has not publicly declared interests.

Meantime, his intent to retire remains a subject of the army's approval under the UPDF Act, 2005.

“An officer may in writing tender the resignation of his or her commission to the board but shall not, unless otherwise ordered by the Chief of Defence Forces, be relieved of the duties of his or her appointment until he or she has received notification, in writing, of the approval of his or her resignation by the board,” reads section 66 (1) of the Act.

In Uganda, top military officials including the country's former spy chief, Gen David Sejusa, have previously had their requests for release from the army either delayed or even denied.
 
Sawa

Pictures Zifuatie Ili Nikirudi Nichangie

Habari Hii Imekanuswa Hajajiuzuru Bado Yupo Jeshini
 
This is strategic his presidency is more than closer and ready now. I submit now for future reference.
 
Ndio shida yetu, umakini zero! Kweli kabisa huyo ni graduate wa Nottingham University? Kweli?
Ulimbukeni na ushamba!
 
Amekanusha vikali sana, amesema mtakuwa mmetype kwenye ukurasa wake akiwa hayupo. Ahahahaaa...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…