Muigizaji wa maisha ya mzanzibari Freddie Mercury ashinda Oscar

Muigizaji wa maisha ya mzanzibari Freddie Mercury ashinda Oscar

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1551156599231.png


Muigizaji Rami Malek ameshinda Oscar kwa kucheza nafasi ya Freddie Mercury katika filamu inayoitwa, "Bohemian Rhapsody."

Nashangaa si watu wengi wameguswa na ushindi huu unaohusu filamu hii ya Freddie Mercury aliyezaliwa Zanzibar na kwa aina yake kaifanya Zanzibar izidi kufahamika.

Leo nyumba alimozaliwa Freddie Mercury na sehemu nyingine zinazomuhusu vimekuwa sehemu za kuvutia watalii wanaofika Zanzibar.

Siwezi kuwalaumu watu wasiomjua Freddie Mecury kwani mimi pia sikuwa namjua hadi siku moja usiku kiasi miaka 30 ishapita niko chumbani kwangu najitayarisha kulala mwanafunzi mwenzangu jina lake Panothiakis akawa anaupiga mlango wangu kama vile nyumba inaungua moto na anataka nitoke nje nisalimishe maisha yangu yangu.

''Mohamed Freddie Mercury is dead...'' nasikia akiniambia kutoka nje ya mlango wangu.

Kwa haraka nikafungua mlango, Panos kama tulivyomzoea kumwita amesimama anatweta, ''Mohamed Freddie Mercury is dead," karudia kusema.

Kwa kweli mimi simjui Freddie Mercury. ''Panos who is Freddie Mercury."

You don't know Freddie Mercury?''

Mshangao wa rafiki yangu Panos ulikuwa mkuwa na niliona sura yake ilivyokuwa na mfadhaiko.

Alitingisha kichwa na kwanza kabisa akaanza kwa kunifahamisha kuwa Freddie Mercury ni mwanamuziki mkubwa wa kikundi kinachoitwa Queen na kazaliwa Zanzibar akisisitiza neno, ''Zanzibar.''

Panos akajiondokea zake kurudi chumbani kwake.

Nikafungua TV na hapo ndipo nilipojua umaarufu wa Freddie Mercury kwa zile rambirambi zilivyokuwa zikiingia na watangazaji kueleza maisha yake na muziki wake.

Lakini nilikuja kumjua Freddie Mercury vizuri nikiwa Zanzibar na rafiki yangu Dr. Harith Ghassany.

Dr. Ghassany alinipa historia ya Freddie Mercury kwa utulivu na kunipitisha kwenye nyumba ambayo aliishi akiwa mtoto kabla hawajahama Zanzibar.

Turejee kwa Panos.

Siku nyingine tena akanigongea kunipa taarifa muhimu.

Kagonga mlango wangu na nilipomfungulia akaniambia kuwa kuna taarifa kwenye TV kuwa Magic Johnson amegundulikana kuwa ameathirika na AIDS.

Nilikuwa kimya namwangalia Panos sahib wangu. Nadhani aliona kuwa sura yangu ilikuwa, ''tupu,'' yaani blank.

Simjui Magic Johnson.

Panos kwa upande wake alikuwa kimya akiniangalia.

Nilipotulia kutoka katika ule mshagao wangu nikamuuliza sahib yangu mleta habari muhimu kwangu Panos, ''Who is Magic Johnson?''

Habari za filamu kuhusu maisha ya Freddie Mercury na kuwa filamu hii muigizaji wake amepatatuzo ya Oscar nimeiona kwenye post moja aliyoweka Dr. Ghassany mtandaoni.

Lakini naamini sote tunaijua nyimbo ya Queen, "We Will Rock You."

Huyo ndiye Mzanzibari Freddie Mercury.

Panos alipatapo kuniuliza kama namjua muigizaji Anthony Queen nikamjibu ndiyo.

Kisha akaniuliza kama namjua George Foundas.
Nakamjibu namjua.

Panos akaniambia kuwa huyo ndiye baba yake.
 
Born in Tanzania, Farrokh Bulsara a.k.a Freddie Mercury, would move to England and take the rock world by storm. In the end he would be considered the greatest rock singer of all time.



 
Are you Serious?!...alikuwa anatoa
Alianza mwaka 76 huko hadi Kifo chake kinamkuta na alikufwa kwa ngoma tena ile HIV ya mwanzoni kama uliwahi shuhudia, yani unakongoroka hadi vidole.
 
Nafikiri sababu kubwa ya kutotaka kum claim Fred Mercury kama mwenzetu hata kwa sisi tuliokuwa tunajua wakati huo ilikuwa kujisikia aibu ya tabia yake ya ushoga!!! Alikuwa shoga wa kupindukia. Naona tuishie hapo.
 
Freddy Mercury alikufa kabla ya advance technology ya ARV’s sasa hivi angekuwa anavuta pension yake safi
 
yaani kama alikuwa shoga vipi wazanzibar walikemea kuwakilishwa tabia zao na maisha yao na jitu shoga shoga,walisemaje wazanzibari katika hilo?
 
Nafikiri sababu kubwa ya kutotaka kum claim Fred Mercury kama mwenzetu hata kwa sisi tuliokuwa tunajua wakati huo ilikuwa kujisikia aibu ya tabia yake ya ushoga!!! Alikuwa shoga wa kupindukia. Naona tuishie hapo.

Kitu muhimu cha kukumbuka ni kuwa Freddie Mercury alizaliwa Zanzibar lakini hakuwa mzanzibari ndo maana wazanzibari wasingeweza kumclaim

Wazazi wa Freddie walihamia kutoka India ili babake kuja kuendelea na kazi yake ya ukeshia katika serikali ya ukoloni wa muingereza Zanzibar na wakapewa uraia wa Uingereza sababu waliishi katika serikali ya Uingereza japo ilikuwa ni Zanzibar, hivyo Freddie alipozaliwa mwaka 1946 alizaliwa kama raia wa Uingereza mwenye asili ya Uhindi aliezaliwa Zanzibar na ni hivyo kuwa alikuwa considered kama Muingereza tangu kuzaliwa kwake. Hata Freddie mwenyewe alikuwa akijichukulia kama Muingereza,alikuwa obsessed na westerners na alipenda sana kusikiliza miziki ya westerns kama vile Rock music na ndipo alipoamua kujibadili jina lake kutoka Faroukh Bulsara na kuwa Freddie Mercury na ndipo alipokuwa inspired kuwa anaandika nyimbo

Freddie pia hajaishi sana Zanzibar, ameishi miaka nane ya mwanzo na baada ya hapo akiwa na miaka minane alipelekwa kusoma boarding school nchini India, amesoma boarding takliban miaka nane na aliporudi Zanzibar hakukaa sana kwani mapinduzi ya Zanzibar yalitokea na ndipo yeye na familia yake walikimbia kwenda Uingereza
 
Back
Top Bottom