Mume kufuliwa nguo za ndani na mkewe

Da Pretty

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
3,059
Reaction score
1,152
Najiuliza na nimeona niulize na wengine hasa wenye ndoa.
Mke kufua nguo za ndani za mumewe ni hiari,lazima au makubaliano?
Hiyari: namaanisha mke anaweza kufua atakapojisikia kumfulia au anaweza akaamua siku hiyo asifue akaacha mume afue mwenyewe.
Lazima: kwamba hata iweje mume HATAFUA nguo yake hata kama mkewe kasafiri akirudi atazikuta, zikiisha mume atanunua zingine lakini kamwe hatafua lazima afue mke.
Makubaliano: Mume anaweza kuamua kua atakua anajifulia mwenyewe au wakakubaliana kua yeyote anaweza kufua nguo za ndani za wote wawili.
Naomba mnisaidia hapa....
Kwa uzoefu na utashi wako
HASA WANAUME (sijabagua wanawake)
 
He! Kwamba hili swali linaulizwa na mwanamke ngoja waje wakujibu
 
Kwangu huwa Bibi DC anafua tu.....Sijui kama ni lazima au la!!


Kwani wewe umewekewa mtutu wa AK47 ili uzifue haraka??

Ila nakushauri ufue mdogo wangu, kwani wale walioikosa hiyo bahati (MEMKWA) huwa wanaililia sana!!

Babu DC!!
 
Kwangu huwa Bibi DC anafua tu.....Sijui kama ni lazima au la!!


Kwani wewe umewekewa mtutu wa AK47 ili uzifue haraka??

Ila nakushauri ufue mdogo wangu, kwani wale walioikosa hiyo bahati (MEMKWA) huwa wanaililia sana!!

Babu DC!!

Kwahiyo bibi akisafiri inakuaje babu?
 
mimi kwa maoni yangu nitamwambia mama watoto tuchangishe hela hapa tununue washing machine na huzo kufuli zitadumbukizwa na nguo nyingine ndani ya washing mashine so hapo hamna anayefua bali mashine
 
Hakuna kanuni kwa kweli ila kama nilivyosema, imeshakuwa kama kazi yake vile.....

Mbona hutaki kusema yaliyokukuta??

Babu DC!!

Kwahiyo kwako ni lazima afue yeye...
Duh!
 
mimi kwa maoni yangu nitamwambia mama watoto tuchangishe hela hapa tununue washing machine na huzo kufuli zitadumbukizwa na nguo nyingine ndani ya washing mashine so hapo hamna anayefua bali mashine


Kama unaishi uswahilini maji utayapata wapi na umeme je??


Au wewe hizo shida ndogo ndogo hazikuhusu!

Babu DC!!
 
Wapi nimesema hivyo??

Babu DC!!

Hujasema nimekusingizia...
Nisamehe
Lakini sa mbona sikuelewi unaposema imekua ni kazi yake? Ni kama vile wewe haikuhusu...au?
Usinikimbize nieleweshe mjukuu wako mambo yananitatiza haya
 
mimi kwa maoni yangu nitamwambia mama watoto tuchangishe hela hapa tununue washing machine na huzo kufuli zitadumbukizwa na nguo nyingine ndani ya washing mashine so hapo hamna anayefua bali mashine
usinunue hiyo mashine siku zote uje ununue sababu ya pichu?
 
ni wajibu wa mwnamke kumfulia nguo mumewe.

wajibu ni jukumu ambalo huwa si lazima au hiyari lakini huwa imekaa kwamba huwa inatakiwa iwe hivyo kama ilivyo!

wajibu huu hauwezi kuwa applied kama mtu hayupo au anaumwa.
 
Kama unaishi uswahilini maji utayapata wapi na umeme je??


Au wewe hizo shida ndogo ndogo hazikuhusu!

Babu DC!!

mie kama nipo kijijini basi tunapena zamu alafu unajua mie napenda ile smell ya kufuli ya demu so nashangaa watu wanaona tabu kufua kwa nini?
 
Mi nafua lakini sijawahi hata kujiuliza hayo maswali kama ni "lazima, hiari au wajibu"

Ila naona raha sana kufua boxer za hubby...na yeye naona anaona raha kuona always boxers ni safi yeye anachagua tu avae ipi.

Suala la kusafiri na kuchanganya kuwa mfuaji hayupo...nadhani linaongeza sababu za yeye kuni miss. Lol. Maana hajazoea ati kufua mwenyewe na inabidi afue sasa. Utasikia 'naona shida sana kuwa mbali na wewe' kumbe ni mchanganyiko wa mengi kuanzia mambo ya 6X6 na 'other services'
 
ni wajibu wa mwnamke kumfulia nguo mumewe.

wajibu ni jukumu amabalo huwa si lazima au hiyari lakini huwa imekaa kwamba huwa inatakiwa iwe hivyo kama ilivyo!

wajibu huu hauwezi kuwa applied kama mtu hayupo au anaumwa.

Ina maana mume akijifulia au akinifulia na mimi anakua amekiuka????
 
ni wajibu wa mwnamke kumfulia nguo mumewe.

wajibu ni jukumu ambalo huwa si lazima au hiyari lakini huwa imekaa kwamba huwa inatakiwa iwe hivyo kama ilivyo!

wajibu huu hauwezi kuwa applied kama mtu hayupo au anaumwa.

Mdugu yangu mathematics,

Nilitaka kusema mengi ili kueleza jinsi ambavyo umeniokoa kwenye kiaango cha Da Pretty,

Ila jina lako linajitosheleza.....

Wapo watu wachache sana wasioogopa mathematics...sina hakika kama mimi ni mmoja wao!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
@da pretty hizi wajibu zipo kama ilivyo yaani automatikale mwanamke akiolewa inabidi amsaide mume wake kazi fulan fulani kama kumfulia, kumpikia, etc

mwisho utakuja kujiuliza je ni wajibu kwa mke kumuwekea mume maji ya kuoga bafuni ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…