Mume wa mtu nomaah!

bahaticaro

Senior Member
Joined
Jul 20, 2012
Posts
100
Reaction score
31
dah! inaniuma sana nilipata boyfriend na nikampenda sana kumbe ana mke na mtoto mara ya kwanza aliniambia kuwa ana mtoto ila haishi na huyu aliyezaa naye nikamuuliza sababu akasema kuwa huyo mwanamke alimdharau na pia hakutaka kumuoa alikuwa anataka mtoto tu.. baada ya muda nikagundua kuwa dada aliyezaa naye anampenda na kuna muda anaenda kwake juz kati tena huyu boyfriend ananiambia et baba yake mzaz huyu boyfriend kamleta huyo dada aishi kwake kwa kumlazimish mim nikamwambia ni vizuri bas tuachane ili yeye aishi vizuri na mke wake et ananiambia kuwa anaish naye nyumba moja ila hamna communication yoyote na huyo dada na kila mtu analala kwake.....inaniuma kwasababu mimi ndiyo ninaye sababisha huyo dada kufanyiwa vituko na nikimwambia tuachane ananitishia.naombeni ushauri jaman nifanyeje?
 

Unaogopa kutishiwa tu au una lako jambo?
 
Tafuta njia ya kutokea(kimbia)
 
Fanya maamuzi magumu ya kuachana nae, atakua anampenda huyo msichana huku akikutamani na wewe, kama angekua ni mwanaume mwenye maamuzi yake asingesema eti babake mzazi kamleta huyo mdada aliezaa nae ili waishi wote, bila ridhaa yake, ni muongo na atakupotezea muda.
 
Kwa kuwa anakutishia mwache kimyakimya, hatua kwa hatua. Usimpe tena keki, punguza mawasiliano ya simu na pia ya kukutana ana kwa ana. Akikuuliza mbona hivi? Sema poa tu hakuna lolote. Mbona hujibu msg? Niko bize. Tukutane .... Sema sawa lakini usiende. Zima simu. Mbona hukuja na simu ulizima? Nilipata safari ya ghafla, samahani halafu simu nilisahau nyumbani au iliisha chaji. Fanya tu vitimbi hadi akate tamaa. Usimwache gafla.
 
Hapo kwenye bold hapo...kinachokufanya umuamini huyo muhongo ni nini? Hivi kweli unategemea akuambie nikitoka kuku do naenda kum-do na mwenzio???

Huyo ni mkewe na anampenda...usikubali cheap lies za eti wazazi wameniletea mke..utashangaa wanaongeza mtoto wa pili na wa tatu endelea na uamuzi wako wa kusonga mbele...acha kuonea huruma watu wasiostahili.

Maana hata mkiendelea mwisho wenu ni upi? Utakuwa kimada maisha yako yote?

Afu tembela blog moja ya mwanamke na nyumba uone stori za wadada waliofanyiziwa kwa kutembea na waume za watu.

Sawa hukujua ...sasa umejua...hakuna excuse tena.

 
Kumbe ndio mnavyotutosa wanaume kwa njia hizi from now sitomuamini tena demu akitoa visingizio kama ulivyovitaja.
 
nʇɐʍ ɐz әɯnɐʍ ɐu ɐuɐႡɔɐ'әʍәʍ oz!Ⴁ ɐႡɔɐ'ɐ!snʞnႡ !u!uɐʍʞ !Ⴈәʍʞn ɐ!qɯɐnʞ!Ⴈɐ
 
aisee, kuna wanaume ni wataalamu wa kufunga kamba si masihara, yaani binti anapigwa fix mpaka anakosa njia ya kutokea
 
aisee, kuna wanaume ni wataalamu wa kufunga kamba si masihara, yaani binti anapigwa fix mpaka anakosa njia ya kutokea

huyu dem mwenyewe anampenda msela..anatuzuga tu,.
 

Dadaangu kwani wewe hujihisabu kuwa una haki ya kuwa na mume? Na akuowe mbanane hapo hapo uone kama hatakuwa mumeo hata kama unashare.
 

red- So my dear in other words you are not matured enough to make firm decisions?
Hata nyepesi kiasi hiki? Sasa kwa nini usisubiri ukue ndo uingie kwenye mahusiano?

green - Really inakuuma? Just wait ukae upande wa huyo dada ndo utajua maana halisi ya maneno hayo. U should've walked away the minute you realised that. Wadada kama nyie ndo mnapenda sana kupangishwa foleni...
 
hapo sasa unataka ushauri gai wakati kila kitu unakiona???? kama unapenda kuwa mtazamaji sawa lakin maamuzi ya msingi unayo naamin ulishayafanya..
 

Pole shost,lakini mbona kwa maelezo yako inaonyesha wazi unafurahia yanao mkuta mwenzio? kwanza jamaa muongo,kama mie ningesha malizana nae zamani sana,anakutisha inamaana anakubaka humpi Chali kwa ridha yako?
ebu shosti jikaze kike na kama mwanamke kweli tafuta wako peke yako huto furahi ukijakusikia mumeo anamwanamke mwengine njee,sasa basi kabla hujafanyiwa hayo acha kumfanyia mwezio......
 
Mie hata sijakuelewa unasaka Ushuaia juu ya nini? Kutishiwa, kufanyiwa vituko Hugo dada mwingine AMA kabaka 'the other woman'?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…