mimi sijaelewa tatizo bado; kama yote anayokuambia tena hadharani, bila kuuma maneno na mbele ya mke wake akimaanisha kuwa ni kweli kwamba:
a. Kaka una miguu ya CCM
b. Macho ya chama
c. Umbo la kibalozi
d. Ngozi laini ya kifisadi fisadi
Mpe hizo sifa mbele ya mke wake halafu tuone mtaishia wapi, inawezekana ndio mtakuwa mnaheshimiana zaidi. DON'T take it too serious...
On the other hand.. itakuwaje kama hizo ni preview ya kukupigia mahesabu?
Nadhani unamuendekeza, posibly kwa sababu zako binafsi!
- Wewe ni single, married, divorced, widowed?
- Wewe unapomuona unahisi vipi? I mean kuna hisia yoyote uliyonayo juu yake?
- Umeshaongea na mke wake kuhusu kutopendezwa na tabia ya mumewe?
- Kwani njia yao ya kwenda kazini inapitia barazani kwako?
Hapo kwenye red.....Natamani kukuona ili niongeze exposure:bounce:!
Kwa vile bado hujamfahamu vizuri huyo bwana, inawezekana ni mapema mno kufanya conclusion yoyote hasa ukizingatia mambo hayo anafanya mbvele ya mekewe (hayafanyi mafichoni). Kwa mfano suala la ku'hug' kwa baadhi ya watu sio ishu kihivyo. Na hilo la kusifia, kuna watu wana tabia ya mzaha sana hata kwa watu wageni.
Lakini kama walivyosema wengine kama ukaribu huo unakukera ni vema ukamueleza wazi huyo bwana bila kuuma maneno na hasa body language yako ioneshe kweli hupendi/hutaki!
hhehehehe!hapa nilijua tu hommie langu lazima lichangie tu!Kuna vidume havina aibu na vinaweza ku flirt kiutani na mke akachukulia utani kumbe ndio vinafanya kweli! No sio mapema tena amechelewa sana! Amani yako moyo ni muhimu na hao mke na mtoto wala hawana habari na kinachokusibu; TAKE ACTION mamii
hhehehehe!hapa nilijua tu hommie langu lazima lichangie tu!
ai miin YUU HAS TU SEI SAMSINGI HIA BANA!
Wapendwa nina rafiki ambae pia ni jirani yangu. Urafiki ulianzia kwa mtoto wao wa miaka 4, tukafahamiana na mama wa mtoto na tukawa marafiki na hatimae nikatambulishwa kwa baba wa mtoto ambae pia ni mume wa huyu rafiki yangu. Tulipoonana mara ya kwanza akadai nafanana sana na dada mmoja na haamini kama hatuna undugu na huyo dada - mke wake hamfahamu huyo mdada ninaefananishwa nae nami simfahamu pia.
Toka siku hiyo kila tunapoonana amekuwa hakosi cha kusema juu yangu, mara nina macho ya uhamasishaji, lips sijui za kufanyaje.... umbo la kampeni... nk nk. Amekuwa akiyasema hayo mbele ya mke wake na rafiki zake. Sijamzoea wala sina utani nae, na nimeweka wazi kwamba sifurahii anachokifanya lakini ni kama hanielewi. Leo asubuhi tumekutana akiwa na mke wake wanaelekea kazini, mke wake akaja kunisalimia na kunihug, mume nae akaja akafanya kama mke wake hii ni mara ya kwanza kwa yeye kunihug, akashtuka kama kapigwa shoti na akasema nina ngozi laini hajapata kuona! Nilijisikia vibaya na niliona mke wake pia amekosa amani. Sijui kilichoendelea baada ya kuachana nao. Nimebaki na maswali mengi na sijui ana maana gani kwa anayoyafanya lakini naona anavuka mipaka. Nilikuwa na imani mke wake atachukua hatua na kumkanya, sijui kama amefanya hivyo.
Wapendwa mnalionaje hili?
Annina
Nipo kwenye serious mahusiano na huyu mume wa rafiki yangu anafahamu hilo, Sijazungumza nae, sababu mume wake huwa anasema mbele yake - niliamini katika hali ya kawaida angechukua hatua, Sina hisia zozote kwake
...........mhhhhhhhhhhh!!Njia nzuri hapo ni kuwaepuka wote huyo rafiki yako na mume wake usiwe close nao. Bila hivyo mtakuja kukorofishana na huyo rafiki yako kwa ajili ya mume wake. Ninavyosema hivi mimi mwenyewe yalishanikuta kama hayo, hivyo hivyo mume wa rafiki kutwa kunisifia hadi mkewe ambaye ni rafiki yangu wivu ukamwingia na kuhisi namchukulia mumewe kumbe mumewe alikuwa limbukeni tu.Halafu mbaya zaidi anakusifia vitu ambavyo mkewe hana hapo ndio kasheshe kweli kweli.
Dada...kwani wewe mananihino umeyaelewaje? Unaweza ukaninon'goneza pembeni kama hutajali.....(nami nipate kukukumbatia nii-feel hiyo ngozi yako laini...shhhhhh)
ooh no.. I knew it!!!
anina ......
I miss u so........
Hujambo?
Kuhusu huyo jamaa,unahitaji a man around,ili amfumue mangumi siku moja ndo aelewe...
Ngoja nije huko.........