Muonekano rasmi wa Tuzo za Muziki Tanzania 2024

Muonekano rasmi wa Tuzo za Muziki Tanzania 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Hadithi ya Tuzo za Muziki Tanzania (TMA) inazidi kupamba moto, na sasa tumebakiza siku tisa tu hadi wasanii wetu wapate fursa ya kutunukiwa heshima kuu kwa kazi zao za ubunifu. Tuzo hizi hazina maana tu ya kusherehekea ushindi, bali zinawakilisha moyo wa kujituma, ubora na vipaji ambavyo vinaibua ari ya ushindani mzuri katika tasnia ya muziki nchini.
Screenshot 2024-10-10 165515.png
Leo hii, Oktoba 10, 2024, jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma, anayefahamika na wengi kama Mwana FA, akiwa mbele ya waandishi wa habari waliokusanyika kwa shauku, alionyesha rasmi muonekano wa Tuzo za Muziki Tanzania (TMA), akitoa ahadi kwamba serikali imejipanga kuhakikisha viwango vya juu vya tuzo hizi vinaimarika kila mwaka.

"Sisi wasaidizi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tunaona mapenzi ya dhati ya mama yetu kuhusiana na michezo, sanaa na utamaduni wa nchi hii, hivyo hatuwezi kufanya vitu chini ya kiwango, ndio maana tuzo hizi zilikuwa zinaendelea kuhakikiwa" amesema Mwinjuma.
Screenshot 2024-10-10 165418.png
Kwa upande wake, Katibu wa Baraza la Sanaa la Taifa, Dkt. Kedmon Mapana, amesema: "Mwaka huu tumepokea kazi zaidi ya 1440, ikilinganishwa na mwaka jana, katika vipengele 36 vinavyoshindaniwa."
Screenshot 2024-10-10 165353.png
Soma: Vipengele vya Tuzo za Muziki za TMA 2024 ni Pamoto
 
Mbona sijaona alama yoyote inayohusiana na Muziki hapo? Yani kama hujaambiwa unaeza hisi ni Tuzo la LoyoTua.
Lakini pia hivi hii nchi haliwez tendeka jambo lolote bila kutukuzwa kwa huyu Mama?
 
teh hadi aliezishika ni mjanja ila kaonekana mshamba 😆 😆 😆
Tuzo ana design mtoto wa fulani ndugu yetu, mbayaa, utadhani za hali ya hewa, au mazingira
 
Back
Top Bottom