Muongozo wa Kisheria juu Mtumishi wa Umma kukata rufaa kwa Rais

Muongozo wa Kisheria juu Mtumishi wa Umma kukata rufaa kwa Rais

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Leo mheshimiwa rais Samia amesikika akisema kuwa hataki kuona rufaa ya mtumishi wa umma ikiletwa kwake baada ya kuwa imeshaamuliwa na Tume ya utumishi wa umma.

Ningependa kumkumbusha Rais Samia kuwa, kwa mujibu wa sheria yeye ni mkuu wa utumishi wa umma na pia ni sehemu ya mamlaka ya nidhamu ya watumishi wa Umma na pia ana dhamana na mamlaka ya kusikiliza rufaa za watumishi zilizotolewa rufaa na chombo cha utumishi wa umma.

Kwa mujibu wa muongozo wa mashauri ya watumishi wa mwaka 2011, unaorejea kifungu namba 25(1) cha sheria namba 8 ya mwaka 2002 ikisomwa sambamba na kanuni ya 60(1) ya utumishi wa umma ya mwaka 2003, Rais ndiye mamlaka ya rufaa kwa watumishi ambao mamlaka ya nidhamu ni katibu mkuu kiongozi, Pia kifungu 25(1)(d) cha sheria ya utumishi wa umma namba 8 ya mwaka 2002, Mtumishi au mamlaka za nidhamu zinayo haki ya kukata rufaa kwa rais juu ya maamuzi yaliyotolewa na tume, na maamuzi ya rais yatakuwa ya mwisho!

Tunamtaka mheshimiwa rais atawale kwa mujibu wa sheria, na aache kutoa kauli ama za kutotaka kuwajibika au zinazoweza kuchanganya mamlaka za maamuzi juu ya haki juu ya watumishi wa umma.

Mheshimiwa Rais lazima ajue kuwa suala la ajira za watu na haki zao za kazi ni suala very sensitive, siyo sahihi kutolea kauli za kuchanganya kwa sababu ni suala linalogusa rizki za watu.

Kama mheshimiwa rais hataki kujihusisha na masuala ya watumishi basi huu ni muda muafaa wa yeye kukubali kubadili katiba inayompa mamlaka ya kuwa mkuu wa utumishi wa umma. Ifahamike miongoni mwa mambo ambayo wananchi wanayalalamikia ni mamlaka makubwa ya rais, Sasa ni wakati muafaka kwa Rais Samia kutupa sisi wananchi katiba bora nzuri ili haya anayojaribu kuyakwepa basi yafanywe na taasisi nyingine kikatiba na kisheria badala ya kumtupia rais

Hapa chini ni sehemu ya muongozo wa utumishi wa umma wa mwaka 2011 unaohusu rufaa za watumishi wa umma!

20210608_100453.png
 
Maneno halisi aliyoyasema rais ni yapi?

Kwa muktadha gani?

Kwa mantiki gani?

Kuna video?
 
Dah! Hii nchi ? naomba Mungu nishuhudie mengi ya nchi hii . Sheria vs Matamko?
 
Kwa mwendo huu yaani bado kidogo tu naye atasema akifa ataenda kuwa makamu malaika mkuu .
 
Maneno halisi aliyoyasema rais ni yapi?

Kwa muktadha gani?..
Kauli yoyote ya Rais iwe ya utani au msisitizo au amri tu inayokwenda kinyume cha sheria ni kauli tata na ni hatari maana inaweza kuchanganya wananchi na mamlaka za nidhamu kazini. Rais awe makini na kauli zake
 
Kauli yoyote ya Rais iwe ya utani au msisitizo au amri tu inayokwenda kinyume cha sheria ni kauli tata na ni hatari maana inaweza kuchanganya wananchi na mamlaka za nidhamu kazini. Rais awe makini na kauli zake
Sawa, lakini rais kasema nini?

Kwa sababu mpaka sasa hivi tunaambiwa rais kasema hivi, na watu, hatuna kauli halisi inayonukuu neno kwa neno, hatuna audio, hatuna video.

Ndiyo maana nikauliza, rais kasema nini?

Kwa sababu inawezekana wewe ukawa una misrepresent maneno ya rais, kwa makusudi au kwa kutojua kumsikiliza mtu vizuri.Mtu mwingine akamsikiliza kwa kituo na muktadha akaelewa kwamba amesema tofauti na tafsiri yako.

Nimesema hivi kwa sababu, kuna watu wanabisha kwamba rais hakukataa kusikiliza rufaa, amekataa kusikiliza rufaa ambazo zina abuse nafasi ya rufaa, rufaa ambazo hazina merit, mtu anakata rufaa tu kwa sababu ana nafasi ya kukata rufaa, lakini ukiangalia unakuta hana merit. Kitu ambacho, kama kweli rais kasema hivyo, kasema hatasikiliza rufaa zisizo na merit, mimi sioni tatizo.Kwa sababu rais ana muda adimu na kazi nyingi na anatakiwa achuje rufaa za kusikiliza.

Na hata mahakamani kuna kesi nyingine zinatupiliwa mbali, hazisikilizwi, kwa kukosa merit.

Sasa narudi kwenye swali langu.

Maneno halisi aliyosema rais ni yapi? Kuna video au audio iliyorekodi maneno kwa muktadha na mantiki yote?

Sitapenda kumsema rais vizuri au vibaya kabla ya kujua maneno halisi aliyoyasema ni yapi, kwa sababu kuna upotoshaji mwingi wa kisiasa, na pia kuna watu wana uelewa mdogo wa kuchambua mambo, wanaweza kuichukua kauli nzuri tu, wakaiandika vibaya.

Hivyo basi, kuondoa utata, ningependa kupata maneno halisi aliyotumia rais na muktadha mzima.
 
Sawa, lakini rais kasema nini?

Kwa sababu mpaka sasa hivi tunaambiwa rais kasema hivi, na watu, hatuna kauli halisi inayonukuu neno kwa neno, hatuna audio, hatuna video...
Hiyo hoja ya kukataa kusikiliza rufaa kwa hoha kuwa hazina merit ni tatizo kubwa zaidi, wa nini usiipokee kwanza na kuisikiliza ili ujue ina merit au la?, Utajuaje kuwa haina merit wakati hujaipa nafasi ya kuisikiliza?
 
Hiyo hoja ya kukataa kusikiliza rufaa kwa hoha kuwa hazina merit ni tatizo kubwa zaidi, wa nini usiipokee kwanza na kuisikiliza ili ujue ina merit au la?, Utajuaje kuwa haina merit wakati hujaipa nafasi ya kuisikiliza?
Mkuu, weka maneno halisi (verbatim) ya rais hapa tujadili vizuri.

Maana naona hata maneno yangu ninayoyaandika hapa tu huelewi, sasa napata shaka kama umeelewa maneno ya rais na unayaelezea vizuri.

Sijasema habari ya rais kukataa kusikiliza rufaa kwa kuwa hazina merit. Hilo neno lina maana kuwa rais hatasikiliza rufaa zote kwa sababu hazina merit, kitu ambacho hawezi kujua kabla ya kuzipata hizo rufaa.

Nimeongelea suala la kwamba, kwa kuwa rais ana muda mchache na kazi nyingi, ofisi yake inaweza kupokea rufaa zote, ikazichuja, zisizo na merit zikatupiliwa mbali, rais akasikiliza chache zenye merit. Wasaidizi wake watamsaidia kuchuja.

Kwangu mimi ninaweza kumuelewa rais anayesema hatasikiliza rufaa zisizo na merit.

Kwa sababu, kauli hiyo tu itamfanya mtu anayetaka kukata rufaa ajifikirie mara mbili kuihakiki rufaa yake kama ina merit.

Na kama anaona haina merit ajiongeze na kuacha kukata rufaa mwenyewe.

Au wewe unataka rais ahangaike na maelfu ya rufaa zisizo na merit?

Na kwenye kujua rufaa haina merit, kimantiki rufaa zote zitapokelewa na Ikulu na kuhakikiwa na watumishi wa rais, wao ndio watahakikisha rufaa zinazomfikia rais zina merit, rufaa za figisu zitatupwa, halafu mtu mwenye rufaa ya figisu asilalamike, kwa sababu rais alishasema rufaa zisizo na merit hatazisikiliza.

Na mtu kama anaona ana rufaa yenye merit ofisi ya rais imeitupa, anaweza kukata rufaa kwa bosi wa rais.

Anaweza kukata rufaa kwa wananchi wa Tanzania kwa kupiga kampeni against Rais, kusema ameonewa na kakata rufaa mpaka kwa rais rais hataki kumsikiliza.

Watanzania wataamua kwenye kupiga kura au kumuondoa rais vingine kisheria.

Ukikataa rais kukataa ruifaa zisizo na merit maana yake nini?

Unataka rais ahangaike na rufaa zisizo na merit?
 
Kwangu mimi ninaweza kumuelewa rais anayesema hatasikiliza rufaa zisizo na merit.

Kwa sababu, kauli hiyo tu itamfanya mtu anayetaka kukata rufaa ajifikirie mara mbili kuihakiki rufaa yake kama ina merit...
Rufaa ni haki ya mtu, kuwa na merit au kutokuwa na merit kutategemea na hoja zitakazojibiwa shaurini.

Huwezi kukataa shauri in the first place bila kujipa time kusikiliza upande unaokata rufaa. kazi/ajira ya mtu ni suala nyeti sana linalohotaji kuchukuliwa kwa uzito mkubwa sana, Kazi ni uhai
 
Rufaa ni haki ya mtu, kuwa na merit au kutokuwa na merit kutategemea na hoja zitakazojibiwa shaurini.
Huwezi kukataa shauri in the first place wakati kazi/ajira ya mtu ni suala nyeti sana linalohotaji kuchukuliwa kwa uzito mkubwa, kazi ni uhai
Nimekwambia hivi, weka maneno halisi ya rais hapa tuyajadili.

Haki hata kupiga kura una haki ya kupiga kura, lakini kama kura yako haina merit, mfano umeiharibu, haki yako ya kupiga kura haifanyi kura yako ihesabiwe.

Weka maneno halisi ya rais tuyajadili.Tuchambue mbivu na mbichi.Kwa kuangalia maneno halisi ya rais, si tafsiri yako ya maneno ya rais, tafsiri ambayo inaweza kuwa sawa au potofu.

Inawezekana kabisa kila rufaa ikasikilizwa na ofisi ya rais, wasaidizi wa rais wakachuja rufaa zisizo na merit zisimpotezee muda rais.

Rais akapata rufaa chache zenye merit ya kusikilizwa na rais.

Na ndiyo maana rais akawa kasema hatasikiliza rufaa zisizo na merit, zitafika ofisi ya rais na kuchujwa kabla hazijamfikia.

Sasa ikiwa rais kasema hivyo, utamlaumu kwa lipi?
 
Siyo sahihi rais kutoa kauli tata zinazotuma conflicting message kwa watumishi na mamlaka za maamuzi ya mashauri ya wafanyakazi.

Kiufupi rais hatakiwi kuhint hata kwa bahati mbaya kuwa eti asipelekewe rufaa ya mtumishi!. Kwaksuli hii watu hawatapeleka kweli wakati kumbe wanayohaki na wangeweza kuipata kwake kwa sababu yeye ni mamlaka halali ya kisheria ya rufaa
 
Back
Top Bottom