Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametanga siku ya mapumziko leo Ijumaa kwa ajili ya kuwaombea wahudumu wa afya pamoja na familia zilizoathiriwa na virusi vya corona.
Nchi hiyo ya Afrika Mashariki inakabiliwa na wimbi la pili la virusivya corona, jambo lililomsukuma raiskuweka amri ya kutotemebea na kufungwa kwa shughuli’’lickdown’’ mapema mwezi huu.
Bunge la Uganda limefngwa kwa muda kwa wiki mbilihuku maafisa wakisema watu 100 katika bunge hilo walipatakana na maambukizi ya virusi hivyo.
Idadi ya vifo vilivyothibitishwa imeongezeka mara 10 katika kipindi cha siku 14 katika kulingana na wavuti wa Our Word in Data,
Chini ya 2% ya watu ndio waliopokea walau dozi moja ya chanjo ya virusi vya corona.
Wakati haya yakijiri , Uingereza imeiongeza Uganda katika orodha yake ya nchi ambazo raia wake wamezuiwa kusafiri kwenda nchini Ungereza.
Ofisi ya mambo ya kigeni na Jumuiya ya Madola (FCO) imesema kuwa kuanzia Juni30, "Uganda itahamia kwenye orodha nyekundu ya kuingia England ".