Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Juma Chikoka, ameendelea na ziara zake za "Mguu kwa Mguu", akiahidi kufika kila kijiji na mtaa wilayani humo ili kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.
Ziara hizi zinajumuisha ukaguzi wa miradi ya maendeleo, ambapo Chikoka ameeleza dhamira yake ya kutembelea vijiji vyote 68 vya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma pamoja na mitaa yote 73 ya Manispaa ya Musoma.