Muundo wa serikali ya Tanzania

nicholau

Senior Member
Joined
Feb 20, 2013
Posts
133
Reaction score
49
Ndugu wadau, mimi naomba nichokoze hoja ya muundo wa serikali ya Tanzania. Napendekeza iwe na serikali moja na wala si mbili wala tatu. Tumeona jinsi kero za muungano wa Jamhuri wa Tanzania zilivyowashinda aliyekuwa waziri Mkuu na waziri Kiongozi. Na baadaye akakabidhiwa makamu wa rais naye ameshindwa. Kwa hiyo binafsi napendekeza serikali moja t ambayo itakuwa na waziri Mkuu na kwa znibar atakuwa waziri Kiongozi. Hii inamaana kuwa seriali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar zitaongozwa na mawaziri. Kwa Tanganyika atakuwa Waziri Mkuu na kwa Zanzibari atakuwa waziri Kiongozi.

Kwa hiyo swala la serikali mbili au tatu litakufa kifo cha mende. Nimemsikiliza Dr. Shein wakati akifungua madhimisho ya miaka 50 ya Muungano akiwa zanzibari, akawa anajiumauma. Anasema kero za muungano zitatatuliwa. Na nani na lini? Wakati tumeshawatumia Makamu wote wawili na mawaziri Mkuu na Kiongozi na wote wameshindwa kutatua kero hizo za Muungano. Mimi nadhani ili kuepuka mkanganyiko huo, kwanza tujindae kuwa na serikali moja na zanzibari ikubali kuwa sehemu ya jamhuri wa Tanzana na Tanganyia irudi. Hivyo ni lazima katiba ya zanzibari ifumuliwe na katiba ya Tanganyika iandikwe kwanza.
Nawasilisha
 

Mbona mlolongo utakuwa mrefu sana,kwa nini tena Tanganyika irudi? ama katiba ya Zanzibar ifumuliwe, na Katiba ya Tanganyika iandikwe - ili hali umesema tunatakiwa kuwa na serikali moja = katiba moja au sijakuelewa?hivi kwa katiba ya 1977 kulikuwa na katiba ngapi?
 
Huyu sheni ni mamluki na nikibarak tuu!..

Nduguu kwa nini usifikirie kila sehemu kuwa na nchi yake bila ya kuwapo huo muungano, naona ndio hizo kero zitakufa kabisaaa mana kila mtu atakuwa na kwake!.
 
Huyu sheni ni mamluki na nikibarak tuu!..

Nduguu kwa nini usifikirie kila sehemu kuwa na nchi yake bila ya kuwapo huo muungano, naona ndio hizo kero zitakufa kabisaaa mana kila mtu atakuwa na kwake!.

Ni kweli Shein ni mamluki. Kwani anajua kitu gani serikali ya Mapinduzi inataka. Akija kwenye kikao anasema muungano uwepo. Unaweza kutafakari jinsi waziri wa sheria wa zanzibari ( yule aliyemvua nguo Mbunge Ole Sendeka) hata kama anatoka chama cha CAF anavyotaka serikali tatu harafu aendelee kuwa madarakani? Huyu ni sawa na mtangulizi wake. Kwa hiyo napendekeza serikali moja, Nchi moja ya Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…