Uchaguzi 2020 Muungano wa CHADEMA na ACT, utaifaidisha zaidi ACT-Wazalendo

Uchaguzi 2020 Muungano wa CHADEMA na ACT, utaifaidisha zaidi ACT-Wazalendo

Lord Diplock MR

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2015
Posts
1,393
Reaction score
3,237
Tuweni wakweli sababu hasa ya Zitto Kabwe kutaka hasa muungano wa vyama vya upinzani ni kwa kuwa muungano huo utawafaidisha zaidi ACT na siyo kwamba ana nia ya dhati kuona upinzani ukifanya vizuri.

Ikumbukwe kuwa mwaka 2015 pamoja na kwamba vyama vya upinzani viliungana na kusimamisha mgombea mmoja lakini ACT Wazalendo walisimamisha mgombea wao peke yao Mh. Anna Mghwila.

ACT inakubalika kidogo mno Tanzania Bara, ila upande wa Zanzibar ina nafasi nzuri kwa influence ya Maalim Seif. Kwa mfano mkoa wa Kigoma CHADEMA ina ushawishi kuliko ACT japo ACT ndiyo mkoa wanaoutegemea. ACT kwa Bara inakubalika kidogo mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara, hata hivyo ukubalikaji huo siyo wa kiasi kile kiasi kwamba kama CHADEMA ikisimamisha wagombea kwenye majimbo husika basi ACT haiwezi kupata wabunge katika mikoa hiyo.

Kiujumla kwa upande wa bara ACT Wazalendo bila kuachiwa majimbo na CHADEMA inaweza kupata jimbo moja tu la Zitto Kabwe peke yake.

Hivyo basi katika muungano wa CHADEMA na ACT, CHADEMA haitabenefit sana kwani maeneo ambayo CHADEMA ina nguvu kama DSM, Arusha, Mbeya, Songwe, Kilimanjaro, Mara nk ACT haina nguvu yoyote ile. Ila katika maeneo yote ACT inayokubalika ukiondoa Zanzibar CHADEMA pia ina nguvu na pengine zaidi ya ACT mfano Kigoma.

Zitto Kabwe anajua tayari Zanzibar chama chake kina ushawishi, hivyo anahitaji angalau apate majimbo mawili matatu kwa kupitia mgongo wa ushirikiano na CHADEMA ili wamuongezee viti maalumu. Hii ndiyo sababu ya kulilia zaidi muungano wa vyama.

Kinachofanyika sasa ni Zitto Kabwe kuiblackmail CHADEMA kwa kumchukua Membe anajua CHADEMA itaogopa Membe kugombea ACT kwa hofu ya kugawa kura. Hivyo anajua kwa vyovyote vile CHADEMA itamtafuta Zitto Kabwe ili washirikiane kuepuka Membe kugawa kura za Urais.
 
Tuweni wakweli sababu hasa ya Zitto Kabwe kutaka hasa muungano wa vyama vya upinzani ni kwa kuwa muungano huo utawafaidisha zaidi ACT na siyo kwamba ana nia ya dhati kuona upinzani ukifanya vizuri.
Sasa ACT ikifanya vizuri si ndiyo upinzani unafanya vizuri? Au ACT imhashajiunga na chama tawala? Wewe unataka chama kipi cha upinzani kifanye vizuri ndiyo ukubali kuwa upinzani umefanya vizuri? Zitto kuna mambo ambayo unaweza ukamkosoa, mengi tu ila kwa hili la chama chake chake cha ACT, sioni mahali ambapo unaweza ukamkosoa kwa sasa. Sana sana waanaomkosoa Zitto kwenye maswal haya ya chana chake, mimi naona kama wana nia ya kuwasahaulisha wagombea wa CCM wajisahau, halafu aje awapige mabao kirahisi wakati wa uchaguzi, hasa upande wa Zanizbar
 
Politics is the art of the impossible. Swali la msingi si nani atapoteza bali muungano huo utawapa nguvu zaidi na je sera zao zinaendana?
 
Ni vizuri upinzani ukaungana. Kwa mfano CCM na TLP zimeungana na mgombea wao ni mmoja. CHADEMA na ACT ni muhimu kuungana na kugawana majimbo, kwa mfano Kanda yote ya kusini iachiwe ACT na baadhi ya mikoa katika kanda zingine. ACT au CDM ikipewa kanda iachiwe pia nafasi zote za ubunge na udiwani. CDM wasiweke mgombea urais Zanzibar na ACT wasiweke mgombea Urais Bara, Member ni mtaji mkubwa wa kwa wapinzani. Membe should work together with Lissu.
 
Wataofaidi ni watanzania kwa kukombolewa kutoka kwenye makucha ya Simba aliyewatafuna miaka 60 bila haha kuwaachia.
Kwani kukombolewa ni mpaka vyama viungane? Si wachague tu kimoja wanachokitaka kati ya CHADEMA, ACT, CUF au NCCR?

Tshisekedi mpinzani alishinda DRC bila muungano kwa 38 mwingine 33 na zingine kwa chama tawala.

Watanzania wakimtaka mtu hawahitaji muungano wa vyama.
 
Kwani kukombolewa ni mpaka vyama viungane? Si wachague tu kimoja wanachokitaka kati ya CHADEMA, ACT, CUF au NCCR?

Tshisekedi mpinzani alishinda DRC bila muungano kwa 38 mwingine 33 na zingine kwa chama tawala.

Watanzania wakimtaka mtu hawahitaji muungano wa vyama.
Kwa hiyo unaamini kabisa wakongo walimtaka Tshisekedi?
 
Muungano wowote ule utamnufaisha zaidi Zitto. Hata huyo Membe anataka kutumiwa tu kumsogeza Zitto kuwa kiongozi wa KUB. Sijawahi ona “shushushu mbobezi” mbumbumbu kama huyu
 
ACT wakisimamisha mgombea wao BM msilalamike wanatumika na CCM kugawa kura za CHADEMA maana nyinyi jamaa ni wabinafsi sana lakini upenda kuwavalisha sifa ya ubinafsi watu wengine,na hii ndiyo tabia ya wabinafsi wote duniani.
 
Muungano wowote ule utamnufaisha zaidi Zitto. Hata huyo Membe anataka kutumiwa tu kumsogeza Zitto kuwa kiongozi wa KUB. Sijawahi ona “shushushu mbobezi” mbumbumbu kama huyu

Pengine Membe amehamua kukiimarisha ACT kwa kugombea 2020,2025 na 2030.

CHADEMA, CCM,ACT nk ni vyama vilianzishwa ili kushika Dola hivyo kila haki ya kujiimarisha ili kushika Dola.
 
Ni sawa na wewe una mtaji wa Tshs Mil 3 then Laiser akubali kuungana na wewe kibiashara!!
 
Membe kama Membe hatakuwa na nguvu yoyote ya kisiasa (impact); wanasema mtaji wa maskini huwa ni nguvu zake na MTAJI wa mwanasiasa yeyote asiye na dola ni WAFUASI.... Sasa kama anakwenda upinzani na wafuasi walau 1000 wenye ushawishi majimboni na wilayani sawa huu ni mtaji otherwise hamna jipya ni yale yale.

Jeshi la mtu mmoja si Jeshi ndugu; Maalim yupo tofauti kabisa na ndiyo maana ana nguvu kubwa sababu wanaofuata nyuma ni maelfu kwa maelfu.
 
Ni vizuri upinzani ukaungana. Kwa mfano CCM na TLP zimeungana na mgombea wao ni mmoja. CHADEMA na ACT ni muhimu kuungana na kugawana majimbo, kwa mfano Kanda yote ya kusini iachiwe ACT na baadhi ya mikoa katika kanda zingine. ACT au CDM ikipewa kanda iachiwe pia nafasi zote za ubunge na udiwani. CDM wasiweke mgombea urais Zanzibar na ACT wasiweke mgombea Urais Bara, Member ni mtaji mkubwa wa kwa wapinzani. Membe should work together with Lissu.

Mkuu umenena vyema. Zaidi sana na katika yote, wachawi wabobezi hawapendi kabisa kulisikia hili:

"Membe should work together with Lissu."

Katika hao baba lao ni jiwe mwenyewe!
 
Tuweni wakweli sababu hasa ya Zitto Kabwe kutaka hasa muungano wa vyama vya upinzani ni kwa kuwa muungano huo utawafaidisha zaidi ACT na siyo kwamba ana nia ya dhati kuona upinzani ukifanya vizuri.

Ikumbukwe kuwa mwaka 2015 pamoja na kwamba vyama vya upinzani viliungana na kusimamisha mgombea mmoja lakini ACT Wazalendo walisimamisha mgombea wao peke yao Mh. Anna Mghwila.

ACT inakubalika kidogo mno Tanzania Bara, ila upande wa Zanzibar ina nafasi nzuri kwa influence ya Maalim Seif. Kwa mfano mkoa wa Kigoma CHADEMA ina ushawishi kuliko ACT japo ACT ndiyo mkoa wanaoutegemea. ACT kwa Bara inakubalika kidogo mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara, hata hivyo ukubalikaji huo siyo wa kiasi kile kiasi kwamba kama CHADEMA ikisimamisha wagombea kwenye majimbo husika basi ACT haiwezi kupata wabunge katika mikoa hiyo.

Kiujumla kwa upande wa bara ACT Wazalendo bila kuachiwa majimbo na CHADEMA inaweza kupata jimbo moja tu la Zitto Kabwe peke yake.

Hivyo basi katika muungano wa CHADEMA na ACT, CHADEMA haitabenefit sana kwani maeneo ambayo CHADEMA ina nguvu kama DSM, Arusha, Mbeya, Songwe, Kilimanjaro, Mara nk ACT haina nguvu yoyote ile. Ila katika maeneo yote ACT inayokubalika ukiondoa Zanzibar CHADEMA pia ina nguvu na pengine zaidi ya ACT mfano Kigoma.

Zitto Kabwe anajua tayari Zanzibar chama chake kina ushawishi, hivyo anahitaji angalau apate majimbo mawili matatu kwa kupitia mgongo wa ushirikiano na CHADEMA ili wamuongezee viti maalumu. Hii ndiyo sababu ya kulilia zaidi muungano wa vyama.

Kinachofanyika sasa ni Zitto Kabwe kuiblackmail CHADEMA kwa kumchukua Membe anajua CHADEMA itaogopa Membe kugombea ACT kwa hofu ya kugawa kura. Hivyo anajua kwa vyovyote vile CHADEMA itamtafuta Zitto Kabwe ili washirikiane kuepuka Membe kugawa kura za Urais.
Juhudi za wagawanye uwatawale zinaendelea. Wapumbavu ndio wataingia mtego huu.
 
Back
Top Bottom