Muungano wa serikali tatu hauna nafasi duniani

Muungano wa serikali tatu hauna nafasi duniani

josias

Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
47
Reaction score
34
Nina sikitishwa na baadhi ya mawazo ya baadhi ya watu wanao jiita wana harakati na wasomi katika nchi hii, ni suala la ajabu sana kwa mtu mwenye uelewa mzuri kutetea uwepo wa serikali mbili au tatu.Nina penda kuuliza, endapo kila nchi zilizofanya muungano duniani zingekua na serikali kulingana na idadi ya majimbo au nchi zilizo ungana ingekuaje? Chukulia mfano rahisi wa nchi ya Marekani ambayo ni muunganiko wa serikali za majimbo(nchi) 52 zingekua na rais kutoka kila jimbo ingekuaje? Itakua kazi ngumu sana kuchukua maamuzi kwa nchi yenye muundo wa serikali 3 kwani kutakua na uhitaji wa kuzishawishi serikali shirika ili kufikia uamzi wa pamoja.

Serikali ya jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ingechukua maamzi mazito ya kubain udhaifu wa muungano uliopo kisha wakafanya maboresho ya muungano huu kwa kuondoa serikali ya Tanzania bara na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kisha kukawa na serikali moja ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania(Re-birth of the union) make sidhani kuwa misingi aliyoiacha muasisi wa muungano hayahitaji maboresho.
Kama muungano utashindwa kuwa wa serikali 1 basi zanzibar iachwe iwe nchi huru yenye serikali yake na bara kuwe na serikali yake huru yanye mamraka yake.
 
Nina sikitishwa na baadhi ya mawazo ya baadhi ya watu wanao jiita wana harakati na wasomi katika nchi hii, ni suala la ajabu sana kwa mtu mwenye uelewa mzuri kutetea uwepo wa serikali mbili au tatu.Nina penda kuuliza, endapo kila nchi zilizofanya muungano duniani zingekua na serikali kulingana na idadi ya majimbo au nchi zilizo ungana ingekuaje? Chukulia mfano rahisi wa nchi ya Marekani ambayo ni muunganiko wa serikali za majimbo(nchi) 52 zingekua na rais kutoka kila jimbo ingekuaje? Itakua kazi ngumu sana kuchukua maamuzi kwa nchi yenye muundo wa serikali 3 kwani kutakua na uhitaji wa kuzishawishi serikali shirika ili kufikia uamzi wa pamoja.

Serikali ya jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ingechukua maamzi mazito ya kubain udhaifu wa muungano uliopo kisha wakafanya maboresho ya muungano huu kwa kuondoa serikali ya Tanzania bara na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kisha kukawa na serikali moja ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania(Re-birth of the union) make sidhani kuwa misingi aliyoiacha muasisi wa muungano hayahitaji maboresho.
Kama muungano utashindwa kuwa wa serikali 1 basi zanzibar iachwe iwe nchi huru yenye serikali yake na bara kuwe na serikali yake huru yanye mamraka yake.

Muungano wa serikali moja ni mujarab! Tatizo ni kwamba Zanzibar imeshajiundia serikali yake na bado inapigania kuwa nchi huru zaidi...jambo hilo ndilo linahalalisha uwepo wa serikali tatu, kwa vile kwa deko na ung'ang'anizi wa wazanzibar, si rahisi kwao kugeuka nyuma baada ya 'uhaini' walioufanya wa kuvunja katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.
 
Kwa taarifa yako majimbo yote ya Marekani yana serikali zao chini ya Magavanor. Kila jimbo lina mahakama na sheria zake kwa mambo yasiyohusu serikali kuu.
 
Na jee duniani kuna Muungano wa serikali 2?
...
Kwa chuki zilizopo sasa, serikali moja haiwezekani!
Mi nahisi kama mtu anataka muungano, serikali 3 ndio suluhisho! Kwanza ndio mawazo ya wengi!
 
Naamin we pia ulitakiwa kuiita Tanganyika bila kuongeza neno bara maana kabla ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ilfahamika hivo....Nimeiita Tanzania bara baada ya kuelewa kuwa hadi sasa kuna pande mbili za muungano yaan bara na visiwani....... kikubwa naamini nimeeleweka wakuu.
 
Kwa taarifa yako majimbo yote ya Marekani yana serikali zao chini ya Magavanor. Kila jimbo lina mahakama na sheria zake kwa mambo yasiyohusu serikali kuu.

hata sisi bado tuna weza kuifanya Tanzania nchi moja yenye majimbo au mikoa tofaut tofauti, yaan zanzibar inaweza kugawanywa katika majimbo au mikoa na ikawa na link na serikali kuu.... Naamin hata Marekan magavanor wana wajibu sawa na wakuu wa mikoa huku masenator wakiwa na majukum kama ya wabunge
 
wewe sema Tanganyika bara ndo au Tanzania bara ndo nchi gani

Naamin we pia ulitakiwa kuiita Tanganyika bila kuongeza neno bara maana kabla ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ilfahamika hivo....Nimeiita Tanzania bara baada ya kuelewa kuwa hadi sasa kuna pande mbili za muungano yaan bara na visiwani....... kikubwa naamini nimeeleweka wakuu.
 
Methali: KILA PENYE ZANZIBAR PANA TANGANYIKA - Aidha kiwaziwazi au kiwiziwizi.
 
Tatizo wazanzibar walishachemka sasa wabara wamebaki kuumiza vichwa juu ya muundo wa muungano,very simple let them go!
 
Back
Top Bottom