Utangulizi
Tafadhalini msiutete uzembe japo unauma ,na ikiwa ni watu wa Jazba hamtafika pahala katika kujadili.
Hivi huyu hakusema kama kuna mambu aliyaweka kando katika taarifa yao,na kama angeyasema basi serikali kwa maana na wengine wangekuwa matatani ?
Ni jambo gani lililompelekea kuwataja akina Lowasa na ufisadi wao na kuwawacha wengine ?
Msiwe mnababaika na viongozi walioficha baadhi na kuyaeleza baadhi.Ni kosa kuwaunga mkono watu wa aina hiyo,kwani hakuitenda katika ripoti yake iwe iwavyo kuwa kina Lowasa wamehusika,sikatai lakini kuna mambu huyu mheshimiwa aliyaficha kwa kauli yake mwenyewe ,hilo ni kosa wakati umeaminiwa au umekabidhiwa tatizo la nchi kulitolea ripoti halafu baada ya ripoti na watu kuekwa kiti moto ,unaruka kama mwanamke alieshikwa mbavu , oo mengine sikuyataja kwa sababu bwamkubwa nae angekuwa matatani . Sasa mtu wa aina hii utamwamini kwa lipi kama si mpika majungu.
Hapa naona mnachanganya mambo,na mnashindwa kupambanua ,mawazo na maoni yenu nimeyaona yote yamebase kwenye kwenye conclusion,kwama Mwakiyembe ni mtu safi & that is wrong , once he is on the side of Rulling party for me ,whatever ni mkweli kiasi gani basi ,sitakiwi kumuunga mkono kwa lolote lile mbele ya macho ya wananchi wapiga kura ni kuchoma na kuchoma tu, mpo ? Kama ni mpinzani wa kweli wa Chama kinachotawala hutakiwi kuwa upande wao hata siku moja ,kwa kila watakalolisema inabidi utafute chochote kile kutoka hicho walicho kisema ili ukifanyie kazi na kukiwekea pingamizi,mfano hata Raisi Kikwete akisema Mji mkuu wa tanzania ni Dodoma ,mimi nitaweka pembeni na kusema hapana Raisi amekosea Mji mkuu wa Tanzania ni Daresalaam na ushahidi nitatoa, hapo ndipo upinzani unaposhamiri na kuweka mikakati dhidi ya watawala.
Mambo ya ukweli upewe haki yake ,mambo hayo hayatakikani kufanyiwa Watawala hasa kwenye mfumo wa vyama vingi na ndio system za Ulaya katika upinzani zinavyofanya kazi ,wapinzani wanatakiwa watoe chochote kutoka kwa watawala na kukipinga kama raisi anavyotoa hotuba ya kila mwisho wa mwezi basi wapinzani walitakiwa na wao waisambaratishe hotuba juu chini,sio kukaa na kupiga makofi bungeni hayo ndio yatatufikisha pa kumuona Mwakiyembe na wengine wote ni watu safi na hivyo akina Mwakiyembe kuufikia umma kiurahisi ya kusema .....si mmeona hata Chadema na CuF na vyama vyengine vinatufagilia..........Amkeni wapinzani msiwe na jazba someni between ze line.
Baada ya Utangulizi.
Kama huyu Mwakiyembe ni hodari kuona kiongozi anakashifu ,atwambie kwa nini hakusimama na kusema Kikwete amekashifu Kiti cha Uraisi wa Tanzania ?
Kama yeye ana ubavu wa kweli kutetea Viongozi kwa nini hakusimamia utekelezwaji wa makubaliano ambao hao hao akina Shamhuna na wenzake waliupiga na chini na kumtoa Muungwana Kapa na kumkatisha matumaini.
Kama kuhatarisha Muungano ,Mwakiyembe angekuwa imara na kusimamia ulinzi wa Muungano pale wahafidhina walipodai warudishiwe ASP yao ,nini maana ya turudishieni ASP yetu na nyie mbakie na Tanu ,alete kina cha maana ya kauli hiyo.
Mwakiyembe alimsikia Shamhuna peke yake ! mbona Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar nae alilonga ,mbona Raza nae anaunguruma na kufika kusema wabunge wa Zanzibar warudi Zanzibar ,hayo Mwakiyembe hakuyaona.
Je Mwakiyembe hakuyasikia waliyosema kuwa wimbo wa Taifa wa Zanzibar ni kama wimbo wa kwaya na serikali yake ni sawa na timu ya mpira,Mwakiembe hakuyaona hayo au angeliwaudhi wenziwe ? Hapa ahkudharauliwa raisi wala waziri kiongozi bali imedharauliwa nchi nzima na ni moja ya sababu ya kuzidisha malumbano na kuchochea ,Mwakiyembe angelisimama na kuwaita hawa kuwa ni wachochezi ,alifika kuwaita kusema hayo ? Au anaficha na akisema wengine watakuwa matatizoni ndio nikasema hafai isipokuwa anapalilia mlo wake au ulaji.
Mwakiyembe inaonyesha ni mgeni wa demokrasia na hafahamu haswa maana halisi ya demokrasia ,hivi na afike Uingereza kuna uwanja unakwenda unasema na kusema mpaka tosha yako ,kama unaponda basi huna mipaka utamponda kila unaemuona hafai.
Na hapa Tz ikiwa tumeamua kufuata demokrasia basi isiwe vibaya kumkosoa mtu na ndio neno alilotumia Mwakiyembe ,sasa alitaka watu wanyamaze kimya,kumnyooshea mtu kidole na kusema aadhibiwe hilo ni kosa hasa kwa kiongozi ,watu wanasema na wamesema mengi kuhusiana na hili la Zanzibar ni nchi au si nchi ,ikiwa Katiba mbili kila moja inasema kivyake sasa ulitegemea kuwa Shamhuna au wengine wamesema uwongo,ikiwa Pinda ametegemea Katiba ya Muungano wao wanosema Zanzibar ni Nchi wametegemea katiba yao Kosa lipo wapi la kuadhibiwa mtu.
Naona Mwakiyembe hakuwa shupavu kumueleza Pinda kuwa kusema mambo anayarudisha CCM sio sahihi wakati hili si jambo la CCM ,au Mwakiyembe alinyanyua mdomo kumwambia Pinda kuwa umetenda kosa kusema hivyo ,Mwakiyembe ni mwoga anaogopa kusema kwani hao ndio wenzake au sivyo ?
Mwakiyembe anaogopa Raisi kunyooshewa kidole machoni (anaogopa kusema kutiwa kidole machoni maana ndio lugha sahihi ya msemo huo) ,sasa kama raisi hajaelezewa hajanyooshewa kidole wakati yeye ndio mhusika mkuu wa taifa hili nani mwengine ambae ataweza kusikia au kusikiliza,tumewaona wanafunzi,walimu na wengine wote wanalia na Raisi ,Mwakiyembe hafahamu kama huku ni kunyooshewa kidole kwa Raisi,kelele za kuwafikisha mafisadi mahakamani ,hizi zote anaelekezewa kidole Raisi ,je Mwakiyembe hayaoni haya.
Kusema nina chuki binafsi na Mwakyembe hilo sikubaliani nalo wala mimi si mfuasi wa Shamhuna ,lakini Mwakiyembe amekwenda mbali na hili analolifanya ni kuhimiza udikteta ambao ulikuwa siri ndani ya Chama cha CCM lakini sasa subira zimewashinda wanawindana mchana kweupe ,zamani wakiitana kwa vikao vya ndani na kupeana mawaidha wengine wakikaripiwa kama wanavyosema wengine wakiambiwa wajiuzulu na kikao baada ya kumalizika wengine hushikwa na magonjwa na kufa.
-------------------------------------
Alisema endapo Waziri Mkuu ambaye ndiye kiongozi wa Baraza la Mawaziri akiamua jambo na kulitolea ufafanuzi, hairuhusiwi kwa waziri yoyote kupinga maamuzi hayo, kwani kwa kufanya hivyo ni kutoheshimu kiongozi huyo na ni utovu wa nidhamu.
------------------------------------------
Sasa nini faida ya watu hawa ikiwa kupinga maamuzi ni utovu wa nidamu ?
Hayo hapo juu ni maneno ya Mwakiyembe yaliopo kwenye gazeti ,hivi hivyo ndivyo inavyoendeshwa serikali ,heshima hiyo ndio iliyowapa ruhusa akina Mwakiyembe kuwapandisha mkenge wenzao maana kuuliza,kuhoji na kupinga ni utovu wa nidhamu ? Hivi kama hivyo ndivyo anavyoona Mwakiyembe hamwoni kama akina Lowasa walizulumiwa. Maana ni utovu wa nidhamu kwa aliechini kusikika akipaza sauti kupinga akina Mwakiyembe na wenziwe walishindwa kutumia aidha wakiogopa kuwa watovu wa nidhamu.na Kumwacha Waziri Mkuu Lowasa atumbukie,na ndio hawahawa akina mwakiyembe wanaogopa kumshauri au kumpinga Raisi kwa kuwa watakuwa watovu wa nidhamu na hawana adabu ,hivyo hata wakimuona Raisi anatumbukia kwenye shimo ,WaTanzania wasitegemee kuwa Raisi wao atasshauriwa vilivyo ili kuepuka mradi raisi kasema haya twendeni basi watakwenda wanaogopa kumvunjia heshima raisi ,wanaogopa kumshauri raisi,wanaogopa kumhoji Raisi wanaogopa kumuelekeza Raisi ,sasa nini faida ya akina Mwakiyembe ? Jawabu ni kusinzia kwenye vikao wakishituliwa na makofi na wao wanaamka na kupiga makofi hata hawajui kinachozungumzwa.