Muungano ni dude liumalo, ambalo badala ya kulikata meno, sisi tumelilea na kulipa kidole liume
 

...Mkuu nashukuru kwa kujitahidi kufuatilia...........karibu kwenye fani......yet still hizo sababu hazijitoshelezi..............check technology investment against quantity.....over a period of time...................na hiyo labour charge unayoizungumza kuwa ni cheap........si kweli kwenye fanii hii....hapo unazungumza na teknolojia Mkuu
 
.. kama ni nchi mbona hawana pasi za kusafiria (passport)? Huyo Rais wao mbona hutumia passport ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania! na wala sio ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar!
 
Kuna haja ya viongozi wetu kujifunza kutoka kwa Joseph Kabila na Vladimir Putin, hawa wakubwa huongea maneno machache sana tena kwa tahadhari kubwa. Ukweli kauli ya mh.Pinda imeleta mtafaruku mkubwa zanzibar, kauli hiyo ilipaswa kutamkwa na jk au ak.

..kwahiyo lile swali angesema anampeleke jk alijibu? au angesema yeye si msemaji wa serikali hivyo wa kulijibu ni jk?

..waliouliza swali walikuwa wanazusha jambo, weshalipata. wahangaike nalo kama wao wanaume/wake kweli!
 

..bila muungano, zanzibar ni nchi ya cuf a.k.a waarabu!

..nyi kuweni watukutu, mtakuwa wana wapotevu siku si nyingi.
 
Wanabodi,

Ile haikuwa kauli ya PINDA yaani toka kichwani mwake isipokuwa KATIBA ya MUUNGANO ndivyo ilivyoandikwa.. Katiba imeeleza wazi kuwa Zanzibar sio Nchi kwa nini mnataka kumlaumu mtu hali makosa sii yake?
Atakuwa mjinga na mpumbavu kama atachukua jinsi anavyofikiria yeye kulihutubia Bunge.. katiba inasema Zanzibar sio NCHI, sasa mlitaka yeye aseme kitu gani?.. Sii Pinda aliyeanzisha ama kutunga sheria za Muungano, kaukuta na yale yaliyokubaliwa ndio somo kwake hawezi kufikiria nje ya kile kilichoandikwa ndani ya Katiba!..
Tatizo hapa ni dogo sana.. Tafsiri ya NCHI na TAIFA kipi kinatangulia.. Ikiwa NCHI ni eneo la ardhi ya Bara na visiwa vyake (Muungano) basi Zanzibar sio NCHI lakini kama NCHI ni eneo la visiwa vya Unguja na Pemba -Zanzibar bila shaka Zanzibar ni NCHI...
 
Huu unaweza ukawa mwanzo wa kuandikwa kwa katiba mpya kama watu watajipanga na haswa wazanzibar kudai haki yao, kwani katiba ya sasa ndivyo inasema kuwa znz sio nchi,na hata rais wake ni mjumbe wa baraza la mawaziri la muungano hivyo Karume hana tofauti na wakina Shamsa,n.k wakati wa vikao vya baraza la mawaziri.
 
Has anyone ever asked themselves what will happen in our next general elections if the majority winner of house of representative and presidency of Zanzibar is not CCM?
 
lakini hao wazanzibari wanachodai ni nchi yao tu, watauona kweli udhaifu huo wa katiba? CCM inaweza kuiogopa hiyo hoja ya katiba kwa kudhani kuwa iwapo itakubalika, watakuwa wamewapa nguvu wapinzani. Siasa hizi ndizo zinazotufanya tushwe kuafanya mambo mengi tu
 
ZNZ wana hoja, kuwa pamoja na kuwa miongoni mwa waanzilishi wa BOT tena walioweka fedha nyingi kuliko Tanganyika kipindi kile ila sheria ya sasa ya BOT haiwatambui kama share holders.

Pili ni kwa nini hawana mamalaka yao ya mapato? Kodi ya mapato na ushuru wa forodha ni miongoni mwa shughuli za Muungano, na mwenye mamlaka ya kutangaza kodi hizo ni waziri wa fedha wa Muungano sasa kama wakipata mafuta itabidi tutangaze sisi wa bara?mbona hawatangazi kodi za dhahabu?
 
Binafsi wakuu sioni deal kabisa hapa.. NI Ujinga mtupu kinachofanyika toka pande zote mbili..
Kuelewa kwangu ni swala la NCHI ambalo halina uzito zaidi ya tafsiri ya neno hilo. Zanzibar wanachodai wao ni Zanzibar kuwa NCHI lakini ikiwa ndani ya serikali ya Muungano ambayo ni TAIFA..
Katiba inachosema ni kwamba Zanzibar sio NCHI kwa tafsiri ya kuwa NCHI ni eneo zima la Muungano na kwamba yawezekana kuwa Zanzibar ni TAIFA.. ikiwa na maana TAIFA ni eneo la visiwa hivyo..
Nafikiri ndivyo alivyosema MgonjwaUkimwi kama nilimwelewa vizuri kwamba kinachotangulia ni TAIFA na NCHI ni eneo la Muungano.
Kwa hiyo hata kama tukibadilisha usemi na kusaema Zanzibar ni NCHI bado itakuwa na madaraka yale yale nje ya KITAIFA..
Sheria na uwezo wa Zanzibar kama nchi utakuwa bado umeganda ktk vifungu vinavyoitambua nchi hiyo chini ya Muungano ambao serikali yake ina madakara ya juu zaidi.
 
Muda huu ndio wnatoka nje kwa ajili ya lunch, tunaweza kupata japo nyepesi nini kilikuwa kinazungumzwa na kujadiliwa humo ndani ya kikao...hii ni JF bwana....
 

Bwana Mzee, Shell, StatOil, in addition to hayo uliyoyataja, yaani Petrobras (Brazil) na Dominion (Marekani) ni kampuni ndogo??!! Au hujui kwamba Shell ndiyo wana block pale Mafia??!!
 
..mafuta yakipatikana ktk eneo la ZNZ basi waachiwe 100%.

..yakipatikana ktk mkondo wa bahari tunao-share nao basi iwe 50/50.

..mafuta yakichimbwa, na ZNZ ikiibuka kiuchumi, basi Wabongo ndiyo tutapewa priority kwenda kubeba box, kupiga deki, na kusafisha barabara.
 
A shocking 37 million Americans live in poverty. That is 12.7 per cent of the population - the highest percentage in the developed world. They are found from the hills of Kentucky to Detroit's streets, from the Deep South of Louisiana to the heartland of Oklahoma. Each year since 2001 their number has grown.
 
Sasa baada ya kuchambua sana naona mna jawabu la suali langu Kama Zanzibar si Nchi au Taifa ni nini ?
 
Muda huu ndio wnatoka nje kwa ajili ya lunch, tunaweza kupata japo nyepesi nini kilikuwa kinazungumzwa na kujadiliwa humo ndani ya kikao...hii ni JF bwana....
Kuna wana CCM wametoka kwenye mkutano ,ngoja tusubiri uzushi.
 
Poleni sana ndugu zangu wa Tanganyika mambo ni makali WaZanzibari wanasema Muungano si wa kujadiliwa na CCM na Shingo au Neki yao ,wanazidi kulonga kuwa kama Nec imeshindwa kuwadhibiti mafisadi na kuwawacha wanatembea nchi nzima kifua mbele basi wasijilete Unguja , warudi wakatiane adabu wao kwa wao.
Kama haitoshi wamesema wasichokonoe zaidi kwani ni juzi juzi tu walisikika CCM eti makubaliano ya kamati za CCM na CUF yapelekwe kwa wananchi wakaulizwe ,sasa wanasema na hili nalo wacha CCM wajifungie ndani lakini wakitoka wananchi wanasubiri kuamua hatima ya Nchi yao.
Na wala hili sio suala la CCM hatutaki kusikia Kamati kuu ya CCM ndio inaamua Tunachojua ni kwamba serikali ya ZNZ chini ya Karume ilimkabidhi Nyerere na Tanganyika madaraka ya kuitawala ZNZ.
Kwa hiyo wakuliongelea suala hili ni serikali ya ZNZ na ya Tanganyika , Tanganyika ijivue koti feki la muungano, na ZNZ irudishiwe haki zako zoote. Iko miungano mingi , kuna EAC kuna AU kuna OIC, na kadhalika ,Wazanzibari wataamua wapi wajiunge.
Halafu huyu Mheshimiwa Pinda kama lilivyo jina lake amewapindisha WaTanzania wote kawaondoa kwenye kushughulikia mafisadi na kuwakatisha kona kuelekea kuliko Zanzibar kama ni kijiji au mbuga.
 
Muungano wa Unguja na Pemba ulizaa Zanzibar na kukawa na serikali moja. Hata hivyo muungano wa Tanganyika na Zanzibar ukazaa Tanzania na serikali mbili, DUH
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…