Muwasho

gpblaze

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2011
Posts
304
Reaction score
14
Nisaidieni napata muwasho sana baada ya kuoga.yani nawashwa sana.
 
mwili mzima au eneo fulani. Na je huna allergy yeyote. na kwenye familia yenu kuna mtu mwenye asthma, yaani upande wa baba na mama pamoja na bibi zako.
 
mwili mzima au eneo fulani. Na je huna allergy yeyote. Na kwenye familia yenu kuna mtu mwenye asthma, yaani upande wa baba na mama pamoja na bibi zako.

muwasho ni mwili mzima.na wenye asthma wapo.hata mimi ninayo ila miaka inapozidi kwenda nayo inapungua.naweya kukaa miaka hata miwili bila kubanwa.
 
mwili mzima au eneo fulani. Na je huna allergy yeyote. Na kwenye familia yenu kuna mtu mwenye asthma, yaani upande wa baba na mama pamoja na bibi zako.

allergy ninayo ya kula mayai-nikila natapika sana-tokea nikiwa mdogo
 
hilo ni janga la watu wengi....hata mimi nnako hako katatizo mkuu...tusubiri. wataalamu wakuje .
 
allergy ninayo ya kula mayai-nikila natapika sana-tokea nikiwa mdogo
umejibu vema, sasa hii tunaita ATOPIC DERMATITIS, au wengine huita asthma ya ngozi. Hii inarithiwa kama inavyorithiwa asthma. Na ugonjwa huu huwa unaendana sana na allergic to animal protein yaani protein ya wanyama wote. Sasa bahati mbaya au sijui nzuri kwamba wewe umerithi hizi zote. Sasa kwa mfano ukila nyama au protein ambyo unaallergy nayo kwanza automatically utawashwa na kuongeza unyeunyevu utaongeza zaidi muwasho hivyo ndo maana ukioga au ukiwa na jasho utapata muwasho zaidi. Mambo ya kuzingatia ukiwa na ugonjwa huu.1. Pamoja na kuwa na allergy to animal protein lakini si animal protein zote, namna ya kujua ni kuwa unatakiwa kula moja baada ya nyingine na itakayo kuwasha au kukuletea shida kama ulivyoelezea kwenye mayai basi hivi vinavyokusumbua uviache kabisa katika maisha yako yote. Mfano wa animal protein nyama, samaki, dagaa, mayai, maziwa, senene, n.k2. Mtu mwenye asthma ya ngozi anashauriwa kuacha kutumia sabuni au mafuta yenye harufu au chemicals. Unashauriwa kutumia sabuni ya kipande hasa mbuni au kodry au jamaa. Mafuta anashauriwa atumie yasiyona harufu, mfano vestiline ya watoto.3. Unashauriwa kutumia nguo za pamba coz hizi zinanyonya jasho hivyo kupunguza muwasho. Kama unanguo yako isiyo ya pamba tanguliza tshirt au shumizi ndani ya pamba. 4. Kufua unashauriwa utumie sabuni ya kipande kuliko ya unga coz ya vumbi ya sabuni hasa ya unga. Hii ni applicable hata kwa asthmatic pt. Hata ukitumia sabuni ya unga basi nguo suuza kwa maji mengi na mara nyingi. Coz hili vumbi likigusa ngozi chemicals zake zinawasha lakini kwa asthma inasababisha chocking na hivyo inaweza kusababisha asthmatic attack.Kumbuka ALLERGY HAINA TIBA, tiba zote zinazotolewa ni za kutuliza tu matibabu pekee (definitive treatment) ni kuepukana na vile vinavyokusumbua, pia wakati wa kuoga usipende kutumia plastic kujisugulia bali tumia kitambaa laini cha pamba.Ukiwa unapata muwasho uwe unaneglect itaisha ukiona inazidi waweza tumia dawa za kuzuia kuwasha kama Prednisolone kama unawashwa mwili mzima au hydrocortisone cream kama unawashwa maeneo eneo au meza cetirizine. Ntumia simu hivyo naweza nisieleweke vema ila naamini itakusaidia na wale ambao wanahusika. Nakutakia pasaka njema.
 
nashukuru jf jaman namm ninatatizo hili duu mungu awabarik wanajamvi wote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…