Muziki uliokawia wa Omari Kungubaya

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MUZIKI ULIOCHELEWA WA OMARI KUNGUBAYA

Omari Kungu Baya alikuwa mpiga guitar maarufu katika miaka ya 1970.

Nyimbo yake, "Salaam za Wagonjwa," ilikuwa ikifungua kipindi cha Radio Tanzania Dar es Salaam, chenye jina kama hilo.

Alikuwa akipiga mziki wake Manzese kwa Mama Mary sasa kunaitwa Uwanja wa Fisi.

Ukitembelea sehemu hizo nyakati za jioni miaka hiyo hutoweza kukosa kusikia muziki wake.

Upigaji wa guitar wa staili wa Kungubaya haukuwa maarufu sana Tanganyika ulishika sana Kenya na pakawa na wapigaji wengi kama George Mukabi na Daud Kabaka.

Bahati mbaya sana Kungubaya alipiga muziki wa aina hii wa guitar moja wakati wake ukiwa ushapita sana.

Muziki huu wa guitar moja na chupa ikigongwa uliingizwa Tanganyika mwanzoni miaka ya 1950 Radio Dar es Salaam ilipoanzishwa mwaka wa 1952.

Huu ndiyo wakati Frank na Dada Zake walipoanza muziki wao uliokuwa maarufu sana.

Lakini Frank Humplink hakudumu sana katika upigaji huu wa guitar moja Peter Colmore alimchukua Nairobi katika bendi ya Jambo Boys iliyokuwa na wanamuziki kama Edward Masengo, Fundi Konde na Fadhili William.

Nyimbo za kwanza kusikika za mtindo huu katika Sauti ya Dar es Salaam zilikuwa za Mwenda Jean Bosco ambazo alirekodi Hugh Tracey na santuri zake kutengenezwa Afrika ya Kusini na kampuni ya Gallatone.

Bahati mbaya Omari Kungubaya amefariki bila kuacha nyimbo zilizorekodiwa kama hii ya wagonjwa.







 
Naukumbuka wimbo huo hapa; inabidi uufungue ukiwa YouTube.
 
Xah

Mzee umenirudisha kihesaaaaa
 
Mohamed Said, Kichuguu, Retired, Nguruvi3, Pascal Mayalla,

..kaka zangu hapo juu, au mwana-JF, yeyote naomba msaada kuhusu jina la wimbo unaopigwa ktk background ya hiyo video hapo chini.


JK,
Hii nyimbo ilipigwa na kurekodiwa Uholanzi katika miaka ya 1960 na aliyeimba hii nyimbo ni kijana wa Kitanzania ambae baadae alikuja kuwa waziri katika serikali ya Tanzania.

Bahati mbaya huyu bwana jina lake silikumbuki.

Lakini naamini Masud Masud atakuwa ana historia kamili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…