Mvinyo ........... wine............. Karibu

Mamndenyi

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
43,242
Reaction score
60,939
Mods, chonde chonde, huu uzi nakuombeni muuache hapa hapa.

Leo tutengeneze mvinyo wa rozela; Kutengeneza mvinyo wa rozela .......... lita 20.

Viambaupishi;
rozela gramu 200;
sukari kilo 12;
chungwa 2
limao 1
hamira vijiko vidogo 6
sufuria,
ndoo ya lita 20
dumu la lita 20
air lock 1
mwiko 1
jiko na mkaa au kuni


NAMNA YA KUTENGENEZA

1. chemsha maji pamoja na rozela, chuja weka kwenye ndoo, ikianza kupoa weka sukari, juisi ya chungwa, limao juisi yake pamoja
na maganda ya nje yaparue (hii ni kwa ajili ya fleva), hamira, koroga funika vizuri.
2. koroga kila siku mara moja kwa muda wa siku sita
3. siku ya saba chuja, tia kwenye dumu la lita ishirini, weka air lock ikiwa na maji ndani (kama huna air lock unaweza
kutumia mrija ambao utauingiza kwenye chombo chenye maji) hii ni kwa ajili ya kutoa hewa ndani ya mvinyo wako;
4. Mvinyo mzuri ni ule uliosindikwa ukakaa muda wa kutosha ....... miezi sita na kuendelea.
5. baada ya miezi sita unaweza kufunga tayari kwa kuuza; ukitaka chupa, lebo, sili unaweza kuniuliza zaidi.

Karibuni kwa maswali maoni na ushauri.

Nawakilisha.
 
Upo juu mam embu tuambie najinsi ya kuandaa mbege a.k.a wari
 
Poa,
Kama uko bongo
niambie tu nikuelekeza mtaa,
naona kuna vichupa vichache vimesalia hapa.

hee kweli hii kali jamani
hivi kuna mvinyo wa Rozella?
nilikuwa sijui na sijawahi kunywa
nije kuchukua kwako bestito Mamndenyi ?
 
Nakuja niunywe usiku , afu mi nikilewa hua sioni njia .
Si utani dischurge hata usubui ?
Kuna tatizo ?
 
Hahaaaa mchanganyo huu nahisi unaweza ukalala siku tatu,sasa Mamndenyi mchanganyo aina ya air lock 1 kwangu mtihani ujue Lol!
 
Nakuja niunywe usiku , afu mi nikilewa hua sioni njia .
Si utani dischurge hata usubui ?
Kuna tatizo ?

Heee fomula hiyo katengeneze mwenyewe unywe ikishuka chini mkeo awe karibu.
 
Hahaaaa mchanganyo huu nahisi unaweza ukalala siku tatu,sasa Mamndenyi mchanganyo aina ya air lock 1 kwangu mtihani ujue Lol!

Rudia kusoma ukiwa umetulia utaelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…