Mwadhama Polcarp Kadinali Pengo amewamwagia sifa Wachagga

Mtambachuo

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2023
Posts
1,907
Reaction score
3,560
Leo Jimbo Katoliki Moshi lilikuwa na Upadrisho wa mashemasi 18 katika Ibada ya misa hiyo ambayo iliiongozwa Askofu Mkuu huyo mstaafu wa wa Jimbo kuu Katoliki la Dar es Salaam.

Mwisho wa Ibada hiyo Askofu wa Jimbo Katoliki Moshi Ludovic Joseph Minde alimpa nafasi Kadinali Pengo kutoa salamu na alisema kuwa Wachagga sio wezi kama inavyosemwa na watu kwani yeye amefanya kazi nao akiwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam na walimsaidia sana kwenye kujenga kanisa na maendeleo yalionekana kwenye nafasi waliozopata katika kulijenga kanisa. Aliongeza kwa kusema kama ni tabia ya udokozi ya mtu sio kwa Wachagga tu pia wapo Wasukuma, Wafipa ma wengine wenye tabia hiyo.

Hivyo nyie mnaopenda kueneza propaganda kuwa Wachagga ni wezi ili wasipate uhalali wa kuongoza acheni hiyo tabia.
 
Mwadhama abarikiwe sana kwa kusema ukweli mtupu.
 
Nahisi kuna maneno yameachwa. Yaani from nowhere, baada ya kupewa nafasi ya kutoa salamu, akaanza kuwaongelea Wachaga kama siyo wezi!! It doesn't make sense.
 
Ni kweli ,ni watu waadilifu sana na wachapa kazi,ikitokea mchaga akawa mwizi ujue atakuwa mwizi kweli au ikitokea akawa Malaya ujue atakuwa Malaya kweli.mchaga alilifanya jambo lolote chini ya jua hulifanya kwa weledi mkubwa sana.sio watu wanapenda unafiki unafiki sana kama
Makabila mengine.wanaongoza sana kwa kuchukiwa na makabila mengine lakini wao hata hawajali kuhusu Hilo ni mwendo wa kazi tuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…