Mwajiriwa usisahau jambo hili

Mwajiriwa usisahau jambo hili

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Sina maneno mangi naomba niwakumbushe jambo waajiriwa.

Nambari 1: Kama uliweza kuajiriwa ni vyema ukatambua kuwa unaweza kufukuzwa kazi pia.

Nambari 2: Ukifa, ukistaafu, ukiacha kazi, ukihamishwa, ukipunguzwa kazini, ofisi unayofanyia kazi haitafungwa.

Itaendelea kama kawaida na itastawi kama kawaida, hivyo usijidanganye au usidanganywe kuwa wewe ni mtu muhimu hapo ofisini.

Serikali au mkurugenzi mwanzilishi ndio watu muhimu kwenye hiyo ofisi maana hawafukuziki.

Ukizingatia hayo mambo mawili utapata afya katika maisha yako baada ya kazi yako kumalizika hapo ulipoajiriwa.

Stori fupi kidogo

Kuna askari polisi mmoja Kahama aliwasaidia BARRICK (ACACIA) kuokoa Lori la makinikia ambalo watu walikuwa wanalitorosha.

BARRICK wakampa zawadi ya fedha kidogo na kumpa offer ya kumwajiri. Jamaa alipoona mshahara mnono akapiga kalamu chini upolisi na kuwa mlinzi wa mgodi.

Siku moja akiwa main gate, gate number 2 au 3 hivi sikumbuki vizuri ila ni kati ya yale mageti 2 ya katikati ndani ya jengo la utawala. Jamaa alishitakiwa kosa la kukagua vibaya watumishi, ofisi ikamfukuza.

Alilia kama mtoto huku akikumbusha kontena aliloliokoa hata hivyo kilio chake kiligonga mwamba akafukuzwa.

Waajiriwa acheni tabia za uchawa, fanya kazi uliyoajiriwa tu na ile ya ziada uliyopewa na bosi wako.

Kimbelembele kitawaua na pressure mkistaafu.

Nina stori nyingi ila hiyo moja inatosha kwa leo.
 
Story yako imenikumbusha jamaa mmoja alikuwa meneja wa bank nadhan stanbic mwanza,alifahamiana na boss mmoja wa mgodini huko takribani miaka mitatu

Sasa siku moja yule boss alimwambia jamaa anahitaji manager pale mgodini,meneja wa bank akamwambia hata nipo tayar,yule mzungu alifurahi sana kwakuwa anamkubali jamaa wa bank

Basi kwa furaha aliyokuwa nayo akiwa bar anakula ulabu akamwaga mboga kuwa amefanikiwa kumpata meneja wa bank kuwa meneja wake

Wadau huko mgodini wakasema haiwezekani meneja wa bank akubali kuja mgodini huyu lazima atakuwa shushu wa serikali

Maneno yakawa mengi huko mgodini,kumbuka mwamba alikula pakeji kubwa ya mpunga so akaacha kazi bank

Mwisho wa siku boss kubwa akiwa kwa mandela, boss mdogo akamkuta jamaa anapekuwa documents fulani,mzozo ukazuka, mzungu boss mdogo akamtuhumu jamaa kuwa anampeleleza ili apeleke taarifa serikalini

Mwisho wa siku mzozo mkubwa mwamba akaachishwa kazi,nau anajishughulisha na ujasiliamali mdogo mdogo

Somo hapa: usiwe mwepesi wa kuvutiwa na ofa kubwa ambayo haidumu ni bora upate kipato kiasi lkn endelevu
 
Story yako imenikumbusha jamaa mmoja alikuwa meneja wa bank nadhan stanbic mwanza,alifahamiana na boss mmoja wa mgodini huko takribani miaka mitatu

Sasa siku moja yule boss alimwambia jamaa anahitaji manager pale mgodini,meneja wa bank akamwambia hata nipo tayar,yule mzungu alifurahi sana kwakuwa anamkubali jamaa wa bank

Basi kwa furaha aliyokuwa nayo akiwa bar anakula ulabu akamwaga mboga kuwa amefanikiwa kumpata meneja wa bank kuwa meneja wake

Wadau huko mgodini wakasema haiwezekani meneja wa bank akubali kuja mgodini huyu lazima atakuwa shushu wa serikali

Maneno yakawa mengi huko mgodini,kumbuka mwamba alikula pakeji kubwa ya mpunga so akaacha kazi bank

Mwisho wa siku boss kubwa akiwa kwa mandela,boss mdogo akamkuta jamaa anapekuwa documents fulani,mzozo ukazuka,mzangu boss mdogo akamtuhumu jamaa kuwa anampeleleza ili apeleke taarifa serikalini

Mwisho wa siku mzozo mkubwa mwamba akaachishwa kazi,nau anajishughulisha na ujasiliamali mdogo mdogo

Somo hapa: usiwe mwepesi wa kuvutiwa na ofa kubwa ambayo haidumu ni bora upate kipato kiasi lkn endelevu
Hii dunia ina mambo
 
Sina maneno mangi naomba niwakumbushe jambo waajiriwa.

Nambari 1: Kama uliweza kuajiriwa ni vyema ukatambua kuwa unaweza kufukuzwa kazi pia.

Nambari 2: Ukifa, ukistaafu, ukiacha kazi, ukihamishwa, ukipunguzwa kazini, ofisi unayofanyia kazi haitafungwa.

Itaendelea kama kawaida na itastawi kama kawaida, hivyo usijidanganye au usidanganywe kuwa wewe ni mtu muhimu hapo ofisini.

Serikali au mkurugenzi mwanzilishi ndio watu muhimu kwenye hiyo ofisi maana hawafukuziki.

Ukizingatia hayo mambo mawili utapata afya katika maisha yako baada ya kazi yako kumalizika hapo ulipoajiriwa.

Stori fupi kidogo

Kuna askari polisi mmoja Kahama aliwasaidia BARRICK (ACACIA) kuokoa Lori la makinikia ambalo watu walikuwa wanalitorosha.

BARRICK wakampa zawadi ya fedha kidogo na kumpa offer ya kumwajiri. Jamaa alipoona mshahara mnono akapiga kalamu chini upolisi na kuwa mlinzi wa mgodi.

Siku moja akiwa main gate, gate number 2 au 3 hivi sikumbuki vizuri ila ni kati ya yale mageti 2 ya katikati ndani ya jengo la utawala. Jamaa alishitakiwa kosa la kukagua vibaya watumishi, ofisi ikamfukuza.

Alilia kama mtoto huku akikumbusha kontena aliloliokoa hata hivyo kilio chake kiligonga mwamba akafukuzwa.

Waajiriwa acheni tabia za uchawa, fanya kazi uliyoajiriwa tu na ile ya ziada uliyopewa na bosi wako.

Kimbelembele kitawaua na pressure mkistaafu.

Nina stori nyingi ila hiyo moja inatosha kwa leo.
Kwa hiyo tufanyeje sisi! Kama umekosa ajira za serikali shauri yako bwana!
 
Back
Top Bottom