Mwaka 2023 kuendelea uwe wa madiliko, tutoe ushauri, maoni na maelekezo kuliko kulaumu, kushambulia na kushambuliana

Mwaka 2023 kuendelea uwe wa madiliko, tutoe ushauri, maoni na maelekezo kuliko kulaumu, kushambulia na kushambuliana

HOPEfull

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2021
Posts
1,882
Reaction score
2,313
Salaam great thinkers.

Vurugu zimekuwa nyingi mno kwenye jukwaa au majukwaa.Minyukano mawe mkononi kulaumiana we unajua we hujui kitu maneno makali makali we mpumbavu tu hujui kitu mi ndo najua we hujatembea duniani ngumi mkononi mateke.

Kifupi ni vurugu tupu majukwaani mwisho wa siku tunabaki hoi tumechoka hakuna kitu Cha msingi kilichoonekana kwenye jukwaa au mada yoyote tunabaki tumelala hoi tunakoroma nchi inazidi kuangamia jamii inazidi kupotea na kupata shida.

Great thinkers Kuna Mambo mengi ya msingi sana ya kitaifa yanaletwa humu kujadiliwa lkn badala ya kujadiliwa inakuwa Vita ya wenyewe kwa wenyewe..civil war..mkong'oto mtu hata adui anafurahi Kuona wenyewe kwa wenyewe wanapigana badala ya kumkabili yeye

Matokeo yake inakuwa sifuri.Watu wengi wanatumia nguvu nyingi humu in vain.wengine wanafanya Kama sehemu ya burudani Lakini jf ni jukwaa muhimu Sana .

Waanzilishi wa jukwaa wamefanya kazi kubwa kuanzisha hili jukwaa la kijamii kwa ajili ya kutundisha kuonnya kuekeza n.k. Lkn badala yake imekuwa kinyume.

Great thinkers mwaka 2023 kuendelea uwe wa mabadiliko kusaidia jamii na nchi pamoja na serikali kuishauri na kuiekekeza badala ya kufokeana wenyewe.Tuache kulalamika.

Great thinkers tuwe great pipo kweli kweli.tusaidiane kuelekezana kama mtu hajui au kakosea usimshambulie msaidie mwekekeze.Mara nyingi mada zinakosa nguvu au zinakods kwenda kule ilikokusudiwa kutokana na civil war inayotokea jukwaani.

Uzi utapotea bure dhumuni la uzi linayeyuka na Kama adui basi anaendelea kutesa.

Sasa hivi inchi in matatizo mengi kweli kweli.. Great thinkers ndio sehemu yake ya kuonyesha ukomavu kusaidia nchi na jamii kwa ushauri mawazo na maelekezo.

Pia ningeshauri jf waweke jukwaa maalum la ushauri mawazo maoni na maelekezo ili yasipotee bure tofauti na huku kwenye mijadala ambapo Kila mtu anaandika kivyake.Sasa mfano mtu ameona ushauri Fulani mzuri anajua ataupata sehemu Fulani kwenye mada fulani.

Uzi ni mrefu nitakuja na Part 2.

Poleni Sana na hali tuliyonayo.
 
Unapowaambia jambo great thinkers wa jf jitahidi kufuata alama za uandishi.
Uandishi wako ni mbovu sana, hauna nukta wala koma. Alama za uandishi ni muhimu sana, zinaleta raha ya usomaji, zinatenganisha kati ya jambo na jambo.

Enewei, ushauri wako umepokelewa.
 
Hakikisha unatutenganisha na majizi ya Mali zetu Na Manisha (MACCM)
 
Back
Top Bottom