Pre GE2025 Mwaka 2025 mageuzi ni lazima: Dorothy Semu awataka Wanawake kusimama imara

Pre GE2025 Mwaka 2025 mageuzi ni lazima: Dorothy Semu awataka Wanawake kusimama imara

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kiongozi wa ACT Wazalendo, Dorothy Semu, amesisitiza kuwa mwaka 2025 ni mwaka wa mageuzi na wanawake hawatarudi nyuma katika mapambano ya kudai haki zao. Akizungumza katika Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani jijini Dar es Salaam, Semu ameeleza kuwa hali ya kisiasa nchini imezidi kuwa ngumu, huku wanawake wakiendelea kukumbwa na changamoto za kiuchumi, kijamii, na kisiasa.

IMG_3440.jpeg
Amesema licha ya matumaini yaliyokuwepo kwa uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, wanawake bado wanakabiliwa na ukandamizaji, ukosefu wa huduma bora za afya, elimu, na ajira. Semu amewahimiza wanawake kuungana kudai tume huru ya uchaguzi, katiba mpya, na mageuzi ya kiuchumi yanayolenga ustawi wa wanawake na jamii kwa ujumla.

IMG_3441.jpeg
Akitaja ajenda za Wanawake 2025, amesisitiza kuwa ACT Wazalendo itaendelea kuwa bega kwa bega na wanawake katika kupigania haki zao. Amehitimisha kwa kuwataka wanawake wa Tanzania kuwa mstari wa mbele katika mageuzi ya kisiasa na kijamii, akisisitiza kuwa hakuna taifa linaloweza kukombolewa bila nguvu ya wanawake.

IMG_3442.jpeg

Soma, Pia: Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Dorothy Semu atangaza nia ya kuwania Urais mwaka 2025
 

Attachments

Tuungane sote kupambana na mfumo kandamizi wa ccm
 
Back
Top Bottom