Uchaguzi 2020 Mwaka huu kama umegombea CCM, ukikatwa jina lako huna mbadala, majina yote kutolewa siku ya mwisho na NEC

Uchaguzi 2020 Mwaka huu kama umegombea CCM, ukikatwa jina lako huna mbadala, majina yote kutolewa siku ya mwisho na NEC

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Mwaka huu kama umegombea kwenye kura za maoni, ukashinda halafu kamati kuu au wenye chama wakakata jina lako huna mbadala kama iliyokuwepo siku za nyuma, kwamba utakimbilia upinzani ugombee.

Kama mnavyosikia, alisema Polepole na jana pia amesema Waziri Mkuu kuwa kura za maoni hazikua na maana yoyote, maamuzi yote yako kamati kuu, wao ndio watarudisha jina la Mgombea hata kama ukiwa wa mwisho na kura 0 bado unaweza kurudishwa kua mgombea. Na akamhakikishia shehe majini kua atakua mgombea kule Handeni.

Kinachofanyika mwaka huu, kamati kuu ya CCM itapeleka majina ya Wagombea wa majimbo yote Tume ya Uchaguzi kimia kimia. Ikishafika siku ya mwisho ya kurudisha form ya kuomba kuteuliwa na Tume kwa vyama vya siasa basi Tume itatangaza majina ya wagombea wote hivyo kama ulikatwa unakua huna nafasi ya kuhamia chama kingine kwa sababu muda unakua umeshapita.

CCM wanahofia kua wakitoa majina mapema wale ambao hawatakubaliana na maamuzi ya kamati kuu ya chama au maamuzi ya wenye chama basi wanaweza kukimbilia upinzani na hatimae wakapata nafasi ya kugombea na kushinda uchaguzi.

Hivyo kama uligombea kwenye kura za maoni ukawa mshindi kwa kura nyingi, wenye chama wasipokutaka huna mahala pa kukimbilia. Hivyo wagombea wote jiandaeni na matokeo yoyote yatakayokuja.
 
CCM wanahofia kua wakitoa majina mapema wale ambao hawatakubaliana na maamuzi ya kamati kuu ya chama au maamuzi ya wenye chama basi wanaweza kukimbilia upinzani na hatimae wakapata nafasi ya kugombea na kushinda uchaguzi.


Wakimkata kwa staili hiyo, akaamua kumpigia kampeni mgombea wa upinzani ili kutimiza msemo wa tukose wote, hiyo nayo wameiwekea mkakati upi?
 
What if Kama nina mtu pale NEC akanimegea za chini ya kapeti?
Unamtaftia huyo mtu matatizo. Watajiuliza amejuaje, wanafukuza watu wote pale nec waliobahatika kuiona hiyo document ya majina.
 
Mwaka huu kama umegombea kwenye kura za maoni, ukashinda halafu kamati kuu au wenye chama wakakata jina lako huna mbadala kama iliyokuwepo siku za nyuma, kwamba utakimbilia upinzani ugombee.

Kama mnavyosikia, alisema Polepole na jana pia amesema waziri mkuu kua kura za maoni hazikua na maana yoyote, maamuzi yote yako kamati kuu, wao ndio watarudisha jina la mgombea hata kama ukiwa wa mwisho na kura 0 bado unaweza kurudishwa kua mgombea. Na akamhakikishia shehe majini kua atakua mgombea kule Handeni.
Kuna kila dalili ya kukomoana hapa.
 
Takataka kabisa. Ni siasa za hovyo.

Lakini hili linachangiwa na wanachama wengi kua wajinga.

Haiwezekani sisi wanachama tumchague mgombea tunaemtaka halafu nyie huko juu mumkatae na bado mtuletee mtu wenu tumkubali.
Kama mgombea huyo alitumia njia ya rushwa kupata ushindi huo, unafikiri wakati wa uchaguzi mkuu chama kitakuwa katika hali nzuri ya kumuuza kwa wananchi jimboni?

Maana chama hakitakuwa tayari kutoka hadharani na kumnadi mgombea ambaye si muadilifu, mtoa rushwa na mla rushwa. Sifa kuu ya kiongozi anayetokana na CCM ni lazima achukie rushwa na aoneshe kuwa anaichukia kwa vitendo, kwa maana rushwa ni adui wa haki.

Kiongozi anayetoa na kupokea rushwa hawezi kuongoza kwa haki!
 
Kama mgombea huyo alitumia njia ya rushwa kupata ushindi huo, unafikiri wakati wa uchaguzi mkuu chama kitakuwa katika hali nzuri ya kumuuza kwa wananchi jimboni? Maana chama hakitakuwa tayari kutoka hadharani na kumnadi mgombea ambaye si muadilifu, mtoa rushwa na mla rushwa. Sifa kuu ya kiongozi anayetokana na CCM ni lazima achukie rushwa na aoneshe kuwa anaichukia kwa vitendo, kwa maana rushwa ni adui wa haki. Kiongozi anayetoa na kupokea rushwa hawezi kuongoza kwa haki!
Hivi Chenge hua anagombea chama gani?
 
Kama mgombea huyo alitumia njia ya rushwa kupata ushindi huo, unafikiri wakati wa uchaguzi mkuu chama kitakuwa katika hali nzuri ya kumuuza kwa wananchi jimboni? Maana chama hakitakuwa tayari kutoka hadharani na kumnadi mgombea ambaye si muadilifu, mtoa rushwa na mla rushwa. Sifa kuu ya kiongozi anayetokana na CCM ni lazima achukie rushwa na aoneshe kuwa anaichukia kwa vitendo, kwa maana rushwa ni adui wa haki. Kiongozi anayetoa na kupokea rushwa hawezi kuongoza kwa haki!
Huko ccm nani ambae hatoi rushwa?!
 
Back
Top Bottom