Mwaka tangu kustaafu, PSSPF wekeni ukweli na uwazi mbele

Mwaka tangu kustaafu, PSSPF wekeni ukweli na uwazi mbele

MIGNON

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2009
Posts
4,108
Reaction score
5,110
Naandika kwa masikitiko makubwa baada ya kupita mwaka tangu kustaafu. Mawasiliano kati yangu na PSSPF sio mazuri na hayaonyeshi ukweli na dhamira njema.

Ninawaomba PSSPF mtu akishakamilisha kuwasilisha nyaraka zake na mkazihakiki basi angalau mpeni muda ambao ataweza kupata mafao yake. Kuwaweka watu katika "uncertainty' si jambo jema, linaumiza mno.

Wekeni tu wazi hata mkisema kuwa "mafao yako utapata baada ya miaka miwili"inatosha kwani mtu atajipanga.
 
Nimekuonea huruma mkuu, pole sana. Pesa yako mwenyewe lakini unaisotea.
 
Kati ya mambo yanayowatesa watumishi wa Serikali baada ya kustaafu ni mafao yao halali kupatikana kwa wakati.

Hiki kitu hakieleweki hata kwa wale walioko kazini hivi sasa, kama wangejua wangetengeneza mazingira mazuri mapema Ili wastaafu kwa heshima.

Ushahidi nilionao unaonyesha watumishi wengi waliostaafu kusota hadi kujifia mapema wakati siku si zao. Wanaonufaika kwenye mpango huu kwa kweli ni wastaafu kwenye ngazi za juu Rais, mawaziri wabunge na wakuu wa idara. Waliobaki ni akili kichwani au vilio na kusaga meno.
 
Naandika kwa masikitikito makubwa baada ya kupita mwaka tangu kustaafu. Mawasiliano kati yangu na PSSPF sio mazuri na hayaonyeshi ukweli na dhamira njema....
Pole sana mstaafu.

Naamini mawaziri wanao husika na mambo haya ni waiziri Jenista na naibu wake Katambi.

Kwakweli kuwatesa na kuwasumbua wastaafu ni kujitafutia lawama.
 
Pssf ni wasumbufu sana. Unakamilisha taratibu zote, lakini bado unacheleweshewa stahiki zako.

Sijui hela za wanufaika wanaziweka kwanza fixed account ili kupata faida!! Au sijui wanakopeshana!! Moja ya taasisi mbovu na ya kibabaishaji nchini, ni hii ya PSSSF.
 
pole sana mstaafu.

naamini mawaziri wanao husika na mambo haya ni waiziri Jenista na naibu wake Katambi.

kwakweli kuwatesa na kuwasumbua wastaafu ni kujitafutia lawama.
Inatakiwa UVCCM waangalie kero kama hizi kwenye jamii, na kuishauri serikali. Hapo Wananchi wataona umuhimu wa UVCCM au hata UWT. Wako tayari tu kujibishana na Vyama vya upinzani.

Kuna fao la KUJITOA NSSF sekta binafsi, watu wote walipwe FAO LA KUJITOA

Psssf mafao yalipwe kwa wakati
 
Kuna shida kubwa sana kwenye Organiasational culture Tanzania; kotekote kwa mashirika ya umma na mashirika binafsi vilevile

Unaweza kushangaa tunalalamikia custumercare mbaya hapa jamiiforums lakini na sisi tukiwa kwenye nafasi zetu tunafanya hayohayo

Tunahitaji kubadilika ili tuweze kubadilisha!
 
Kuna shida kubwa sana kwenye Organiasational culture Tanzania; kotekote kwa mashirika ya umma na mashirika binafsi vilevile

Unaweza kushangaa tunalalamikia custumercare mbaya hapa jamiiforums lakini na sisi tukiwa kwenye nafasi zetu tunafanya hayohayo

Tunahitaji kubadilika ili tuweze kubadilisha!
Ni wazo zuri, je ni nani atangulie kwa customer care ili wengine wafuate mfano bora?

Inatakiwa walio juu waanze, na Haki za wafanyakazi zizingatiwe.

Ofisi ya waziri utumishi kwa Raisi

Ofisi ya Waziri Mkuu

Na matatizo ya wafanyakazi kuzingatiwa.

Kuna thread iko active inajadili kuhusu manyanyaso ya PSSSF kuchelewesha mafao

Kuna hot topic ya FAO LA KUJITOA NSSF...wale skilled labor hawalipwi FAO LA KUJITOA
 
Ni wazo zuri, je ni nani atangulie kwa customer care ili wengine wafuate mfano bora?

Inatakiwa walio juu waanze, na Haki za wafanyakazi zizingatiwe.

Ofisi ya waziri utumishi kwa Raisi

Ofisi ya Waziri Mkuu

Na matatizo ya wafanyakazi kuzingatiwa.

Kuna thread iko active inajadili kuhusu manyanyaso ya PSSSF kuchelewesha mafao

Kuna hot topic ya FAO LA KUJITOA NSSF...wale skilled labor hawalipwi FAO LA KUJITOA



Mimi naona kuna shida mbili kubwa kwa hili la mafao, haswa fao la kujitoa na kwingine kote kwenye public na private sectors

1 Ya kwanza ni tatizo la sera
- ambapo hakuna uwazi au miongozo kwenye nini kifanyike na kisipofanyika nani awajibike

2 Tatizo la pili ni mfumo
- hakuna taratibu zilizo wazi katika kutoa kushughulikia wateja, kukiwa na taratibu zilizo wazi na muda unaojulikana wa kutatua kila tasks/application/complains kwa wateja, pamoja na upimaji wa performance na uwajibishwaji kwa watoa huduma tutaona mabadiliko haya yakifanyika
 
Nimemzika Rafiki yangu mwezi uliopita, amefuatiliia mafao yake hajapata. Mke wake ni mjamzito kafuatilia nae hadi sasa wanamhangaisha
Kuna jamaa yangu kafariki mwaka jana, familia ikampitisha mkewe asimamie mirathi,toka mwaka july mwaka jana hadi hii leo wanamzungusha tu,ada ya Watoto ishaanza kusumbua huku haki ya Baba yao wajinga wanaichelewesha maksudi!
 
Pesa imefuatiliwa kwa zaidi ya miaka minne.

Na bado hamna dalili ya hiyo pesa kulipwa.

Upuuzi tu huu. Ndiyo maana watumishi wa umma wanakua wezi wezi kwakua wanahakikisha kujilimbikizia pesa kuepuka mambo kama haya.
 
Kuna jamaa yangu kafariki mwaka jana,familia ikampitisha mkewe asimamie mirathi,toka mwaka july mwaka jana hadi hii leo wanamzungusha tu,ada ya Watoto ishaanza kusumbua huku haki ya Baba yao wajinga wanaichelewesha maksudi!
Tangu mwaka jana bado sana aisee
 
Mimi naona kuna shida mbili kubwa kwa hili la mafao, haswa fao la kujitoa na kwingine kote kwenye public na private sectors

1 Ya kwanza ni tatizo la sera
- ambapo hakuna uwazi au miongozo kwenye nini kifanyike na kisipofanyika nani awajibike

2 Tatizo la pili ni mfumo
- hakuna taratibu zilizo wazi katika kutoa kushughulikia wateja, kukiwa na taratibu zilizo wazi na muda unaojulikana wa kutatua kila tasks/application/complains kwa wateja, pamoja na upimaji wa performance na uwajibishwaji kwa watoa huduma tutaona mabadiliko
Uko sahihi kabisa Mkuu

Waziri wa utumishi Ofisi ya Raisi, ashughulikie hili..

Na Waziri wa Kazi na ajira, Jenista Mhagama, waangalie sera za mafao

Kuwanyima skilled labor mafao, ni kuzuia intellectual investment katika Nchi. Watu wenye weledi wakilipwa mafao yao, watafungua biashara, makampuni na viwanda. Maana Wana elimu na ujuzi. Kuwalazimisha watafute ajira miaka yao yote, ili waje kupata mafao sio sahihi.

Fao la KUJITOA NSSF lirejeshwe
 
Kati ya mambo yanayowatesa watumishi wa Serikali baada ya kustaafu ni mafao yao halali kupatikana kwa wakati.

Hiki kitu hakieleweki hata kwa wale walioko kazini hivi sasa, kama wangejua wangetengeneza mazingira mazuri mapema Ili wastaafu kwa heshima.

Ushahidi nilionao unaonyesha watumishi wengi waliostaafu kusota hadi kujifia mapema wakati siku si zao. Wanaonufaika kwenye mpango huu kwa kweli ni wastaafu kwenye ngazi za juu Rais, mawaziri wabunge na wakuu wa idara. Waliobaki ni akili kichwani au vilio na kusaga me
 
Uko sahihi kabisa Mkuu

Waziri wa utumishi Ofisi ya Raisi, ashughulikie hili..

Na Waziri wa Kazi na ajira, Jenista Mhagama, waangalie sera za mafao

Kuwanyima skilled labor mafao, ni kuzuia intellectual investment katika Nchi. Watu wenye weledi wakilipwa mafao yao, watafungua biashara, makampuni na viwanda. Maana Wana elimu na ujuzi. Kuwalazimisha watafute ajira miaka yao yote, ili waje kupata mafao sio sahihi.

Fao la KUJITOA NSSF lirejeshwe

MPadmire 📍🔨
 
Naandika kwa masikitikito makubwa baada ya kupita mwaka tangu kustaafu. Mawasiliano kati yangu na PSSPF sio mazuri na hayaonyeshi ukweli na dhamira njema.

Ninawaomba PSSPF mtu akishakamilisha kuwasilisha nyaraka zake na mkazihakiki basi angalau mpeni muda ambao ataweza kupata mafao yake. Kuwaweka watu katika "uncertainty' si jambo jema, linaumiza mno.

Wekeni tu wazi hata mkisema kuwa "mafao yako utapata baada ya miaka miwili"inatosha kwani mtu atajipanga.
Mimi ilichukuwa miaka miwili baada ya kustaafu ndiyo nikapata hayo mafao. Vumilia tu one day yes.
 
Back
Top Bottom