Elections 2010 Mwakalebela aiteka kampeni ya JK Iringa

Elections 2010 Mwakalebela aiteka kampeni ya JK Iringa

Mlachake

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2009
Posts
4,437
Reaction score
4,618
Fidelis butahe, Iringa

ALIYEKUWA mshindi katika kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Fredrick Mwakalebela jana alikuwa kivutio na kufunika mkutano wa kampeni wa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, Jakaya Kikwete baada ya kutakiwa kupanda jukwaani.

Katika mkutano huo uliofanyika katika uwanja wa Samora mjini hapa, wananchi walililipuka kwa shangwe na vigeregere huku wakimtaja jina lake mpaka mgombea huyo alipopanda jukwaani.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwakalebela aliwaomba wanachama wa CCM wa Iringa Mjini kuvunja makundi, kwani anaamini kuwa bado chama hicho kina nafasi.

"Wana Iringa kila kitu tunachokiona hapa kimeletwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete, wabunge na madiwani wa CCM. Napenda kuchua fursa hii kuhakikisha chama chetu kinashinda Iringa..."

"Napenda kusema mbele ya Rais Jakaya Kikwete tukiunge mkono chama chetu, kwani tulikuwa watu 12, lakini sasa tuwe kundi moja. Natangaza kuvunja makundi, wapinzani wasitutumie kama mtaji," alisema Mwakalebela huku wananchi wakishangilia na kelele za sauti ya juu.

Baada ya kumaliza kuzungumza na kushuka jukwaani, Mwakalebela alikumbatiana na Kikwete na kisha kushikwa mkono na mgombea huyo wa urais hadi jukwaani tena na kuonyeshwa kwa wananchi.

"Mmemuona Mwakalebela?" alihoji Kikwete mbele ya umati wa wananchi waliofurika katika mkutano huo, wananchi walijibu 'tumemuona" huku wakiendelea kushangilia na kumkumbatia tena Mwakalebela akiwa naye jukwaani.

Kabla ya Mwakalebela kuzungumza Mwenyekiti wa CCM wilayani humo, Deo Sanga 'Jah peaple' aliwaita wagombea wanne waliokuwa katika kinyanganyiro cha kura za maoni ambapo kwa nyakati tofauti walieleza kuvunja kambi zao na kuumuunga mkono mgombea alisimamishwa kwa tiketi ya chama hicho, Monica Mbega.

Awali, mgombea ubunge katika jimbo la Iringa Mjini, Monica Mbega, aliwaomba wananchi kuwachagua wagombea wa CCM, kwani chama hicho kimeweza kutekeleza sehemu kubwa ya ahadi walizozitoa miaka mitano iliyopita.

Mgombea huyo alipoitwa jukwaani na Kikwete hakushangiliwa kama ilivyokuwa kwa Mwakalebela na hata alipoanza kuzungumza baadhi ya watu katika uwanja huo walianza kuondoka.

Mwakalebela ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) alishinda nafasi ya kugombea ubunge Iringa Mjini kwa kupata kura 3,897 dhidi ya Mbunge aliyepita, Monica Mbega aliyepata kura 2,989 katika matokeo ya kura za maoni CCM.

Mwakalebela alitumia dakika tatu kuzungumza na wananchi waliofurika katika uwanja huo huku sauti yake ikisikika kwa shida kutokana na shangwe na kelele kutoka kwa wananchi hao.

Akizungumza na wananchi uwanjani hao Kikwete alisema hospitali ya mkoa huo itaboreshwa pamoja na kujenga maabara.

"Hospitali ya mkoa iendelee kuwa ya mkoa, ya wilaya itajengwa na kuongezwa kwa vituo vya afya ili watu wasijazane katika hospitali hizi" alisema Kikwete.

Akijinadi kutetea kiti chake katika Jimbo la Kalenga, Rais Kikwete aliwataka wanawake nchini kutokuwa na hofu na kwamba katika serikali ijayo ya miaka mitano itaendelea kuwapa kipaumbele katika nafasi za uongozi mbalimbali
SOURCE: MWANANCH
 
Siasa za kinafiki CCM ndo penyewe....
 
haya acha waendelee kuwasomba wanafunzi mashuleni kuudhuria mikutano yao huku utafiti ukionesha wanafunzi haohao kufelu kwa 50%.........kikwete anadhambi
 
Mwakalebela hana jinsi ya kufanya zaidi ya kujipendekeza kupita kiasi ili kuweka mazingira ya yeye kukumbukwa kwenye ufalme wa Kikwete!(its just like he is undressing and bowing)!huh!.............Kwa hali hiyo he might be considered!
 
CCM ni chama cha wanafiki hata ungekuwa wewe ndio Mwakalebela ungefanya hivyo hivyo ili hiyo kesi iliyopo mahakamani ifutwe!! Sasa ngojea huyo mzee wa kikikuyu wa huko Mufindi nae atafanya hivyo hivyo ili kujipendekeza!! Jamaa hawa hawajui maana ya binadamu kuwa na hadhi yake; Shellukindo alionyesha intergrity yake kule Bumbulu kwa kutokubaliana na huu ushenzi!! Hata hivyo nadhani hawa wanyalukolo wamemchuuza tu huyu mkwere come october hawamchagui huyo Monica mbega kwani hana jipya na wamemchoka!!
 
Hizi siasa za Tanzania nisiseme Tanzania ngoja niseme Africa maana we are almost practicing the same thing, Na ilikuwa lazima JKamuite Mwakalebela kwa kuwa inaonyesha kabisa huyu jamaa alifanyiwa mizengwe lakini ukiangalia kwa ndani zaidi wanajitahidi kumpoza jamaa inawezekana huko mbeleni akapata cheo fulani
 
Ndugu Mwakalebela pole sana, maana inaonekana unakubalika kwa wananchi kuliko huyo waliyempitisha. Nadhani watakupoza kwa madaraka fulani
 
Nilifurahi sana coz Wananchi wa iringa walimdhibitishia JK uzuzu wa akina Makamba and Co. kwa kumtema mwakalebela.
 
Unaambiwa hata Orijinal Komedi hawakushangiliwa kama ilivyokua kwa Mwakalebela.
 
Mwakalebela alipigwa bit asipomsupport Mama Mbega basi na Kesi yake na PCCB haita isha,sasa afanyeje jamani?
Kijana ikabidi atii amri vinginevyo kesi ingeendelea.
Ila kazi anayo Mama Mbega manake hana mvuto na hakuna cha maana alichofanya
 
Mwakalebela alipigwa bit asipomsupport Mama Mbega basi na Kesi yake na PCCB haita isha,sasa afanyeje jamani?
Kijana ikabidi atii amri vinginevyo kesi ingeendelea.
Ila kazi anayo Mama Mbega manake hana mvuto na hakuna cha maana alichofanya

Mkuu Katika pita pita zangu zote. sijawahi kusikia sehemu/kijiwe chochote aanapopewa support mama Mbega.
Jana mama Mbega aliingia katika hoteli moja hapa Iringa wananchi walimzomea sana. Then gari ya Mgombea wa Chadema akipaki Nje ya hiyo hoteli na Kuporomosha Kampeni.
 
Mwakalebela alipigwa bit asipomsupport Mama Mbega basi na Kesi yake na PCCB haita isha,sasa afanyeje jamani?
Kijana ikabidi atii amri vinginevyo kesi ingeendelea.
Ila kazi anayo Mama Mbega manake hana mvuto na hakuna cha maana alichofanya

ni kweli kabisa mkuu...! bila kesi jamaa angekuwa amevaa kombati za ukombozi..i mean za CHADEMA
 
nilifurahi sana coz wananchi wa iringa walimdhibitishia jk uzuzu wa akina makamba and co. Kwa kumtema mwakalebela.

call a spade a spade. Kwani vikao vya kumtema mwakalebela viliongozwa na nani? Na anayewanadi akina mrammba na lowassa ni nani?
 
Mwakalebela aliposhuka Jukwaani. wananchi walianza kusambaa. Kikwete wakati anaongea watu wanasukumana getini kutoka nje. what a shame!!!
 
Mpiganaji hakutakiwa kuogopa kesi. Leo hii angekuwa Chadema, kesi angeshinda na Ubunge angepata. Amewaangusha sana wana-Iringa.
 
Aliyeshangiliwa ni mwanachama wa CCM. Kashangiliwa kwenye mkutano wa kampeni ya mgombea wa CCM. Nyie kelele kama wendawazimu za nini?
 
Back
Top Bottom