Mwakyembe ameishindwa tazara?

Mwakyembe ameishindwa tazara?

kanewi

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
298
Reaction score
200
post hii naileta hapa kwenye jukwaa la sheria nikiwa na matumaini kwa wanajamvi pamoja na mengine kunisaidia masuala ya kisheria imekaaje,.mimi ni mtumishi wa MAMLAKA YA RELI YA TANZANIA NA ZAMBIA TAZARA tangu mwaka huu wa 2013 uanze hatujawahi kupata mshahara,leo hii tunazungumzia ni mwisho wa mwezi wa tatu,.Waziri amekuwa anapita na ahadi za uongo kuhusu masuala mbali mbali ya shirika lkn tunaona kama kuna DUDU kali ndani ya IKULU linalo zuia utekelezaji wa mikakati kabambe ya utendaji,.juzi alipata taharifa za mabehewa kubeba mikaa na mbao suala ambalo alilipa uzito wa kisiasa kuliko pelekea kuja na waandishi wa habari usiku wa manane kuonyesha kuwa ni mtendaji lkn ni porojo tu,.suala la mishahara kwa wafanyakazi analipata kila kukicha tunaona analikwepa tu na ilidiriki mtu mmoja kumuambia siku alipokuja tazara akiongozana na waziri wa miundo mbinu wa zambia kuwa,.namnukuu,''mweshimiwa unatuambia treni hii ya jiji tusiisimashishe tuiache itembee lkn unajua kuwa wanayoiendesha hawana mishahara ya miezi mnne?,wewe sizani kama dereva wako akiwa amelewa unaweza kumruhusu akuendeshe sasa sisi tumelewa pombe mbaya sana,tumelewa njaa ya miezi minne na hapo unatusihi tuendeshe treni sasa huoni unahatarisha maisha ya watu hawa kwa kuendeshwa na watu wenye mawazo ya watoto wao kula nini,kutibiwaje,kusomaje,kulala nje ya majumba baada ya kufukuzwa kodi?''mwisho wa kunukuu,.waziri akaleta majibu ya siasa,.sasa ikaja wakakutana tena Lusaka zambia kwa suala la TAZARA ila WAZAMBIA wako COMMITED sana tatizo ni hapa kwetu,.najua kuna watu wa karibu wanapita humu nawaomba wamfikishie ujumbe huu maana njia zote tumetumia imeshindikana pia kwa kutumia TRAWU hasikii na wafanyakazi wenyewe nao wapi basi wanajukwaa wa karibu yake waongee nae,.na naomba usheuri wa nini kifantike ili kulinusuru shirika hili la TAZARA.:attention::attention:
 
Wengine hapo Tazara mumeingia kwa vyeti vya wizi sasa mnapata malipo ya udanganyifu, kama wewe ni Mfanyakazi wa serikali huwezi kukosa mshahara miezi minne,mtakuwa nyie ndo mnatusumbua hapa TAZARA kwa kusafirisha nyara za Serikali kila kukicha,Halafu mkitoka hapo mnajiita Chadema na kuiponda serikali hiyohiyo kwa kusema imeshindwa kazi, nyambaf,Jirekebisheni. BIG UP MWAKYEMBE endelea kuwabana hivyohivyo mpaka kieleweke,
 
Ndg Kanewi nimekusoma, kwa kweli tatizo la TAZARA ni la muda mrefu sana. njia pekee ya kulinusuru shirika hilo ni kubadilisha muundo wa TZR. Kuanzia Collective agreement ya uanzishaji wa TZR ili shirika lijiendeshe kibiashara lisiingiliwe na siasa. Mfano waondoe kifungu Managing Director lazima atoke Zambia. ukiitangaza nafasi hii utapata waendeshaji competent amabo wataweza kufufua utendaji wa shirika. waje hata Wazungu mambo yataenda kuliko wababaishaji hao akina Ndum....o. TAZARA ina madeni mengi sana. NSSF hawajapeleka tangu 1997 je fikiria ni pesa kiasi gani kinadaiwa. hapo ni uozo mtupu. Ndio maana wafanyakazi wanadiriki kupakia mkaa na mbao ili waweze kujikimu....maana hakuna salaries hapo. tangu Dec 2012 hawajalipwa unategemea kuwepo na ufanisi hapo?
 
....Pamoja na hivi karibuni kumwondoa MD Mzee Lewanika lakini najua dhahiri shahiri hiyo sio tiba kwani Serikali ya zambia itateua MD mwinngine kuja kuendesha. hapo ni kama shamba la bini wanakuja kujichumia tu wanaondoka kumbuka alikuja MKANDAWILE wafanyakazi wakashangilia wamepata mkombozi alichowatenda ilikuwa balaa walimfukuza kwa kelele na kumrushia mawe. MKANDAWILE akawa yeye ndio kila kitu..Director of finance, chief engineer, Director of HR, Cashier etc kulikuwa hakuna invoice inalipwa bila ya yeye kuiona hata kama ni ya elf 50. ikawa pesa yote iko kwenye mamlaka yake. Wastaafu hawakulipwa na mpaka sasa nina uhakika kuna malimbikizo mengi sana ya wastaafu sijui ni lini watalipwa.
 
Tazara ni shirika la kipuuzi kweli kwenye menejimenti yake. Lilinishinda nikachapa mwendo. Shirika haliongozwi kwa kufuata sheria. Tazara kila mtu bosi kuanzia station foreman. Shirika limejaa miungu watu. Wanasiasa nao ndo wanalitumia kujinufaisha. Mwakyembe haiwezi Tazara. Tazara inatakiwa ibadilishiwe kwanza sheria yake, kisha muundo halafu top management yote ibadilishwe. Vinginevyo mtalia njaa kila siku. TRAWU nayo magumashi tu. Anzisheni chama kingine cha wafanyakazi.
 
Back
Top Bottom