Mwakyembe Ataka Mdahalo na akina Rostam

Hizi zote ni kelele tu za kuelekea kwenye majimbo ya uchaguzi hakuna kipya. Nchi kimaadili ya uongozi iko taabani. Nakumbuka wakati taarifa hii (Richmond) inatolewa kwa mara ya kwanza pale bungeni nilijua sasa nchi imeamka ki maadili. Lakini kumbe si lolote si chochote tuko palepale.

Kelele zote tunazopiga ni sawa na za mbwa asiye na kucha wala meno, inashangaza kuona jinsi serikali inavyocheka na wezi huku ikiwa imetumia pesa za walipa kodi wa nchi hii kutafuta habari ambayo baada ya ukweli kujulikana hakuna hatua yoyote iliyo na inayo chukuliwa, huu ni usaliti dhidi ya ustaarabu kimaadili ya uongozi.
 
Wewe muache apige kelele huko mjini,sie tunamsubiri jimboni tumgoee kisawasawa.
 
Hivi jamani naomba kuuliza.... Mbunge ni nani na anapaswa kufanya nini kama mbunge?
 
Rostam hawezi kukubali mdahalo maana anajua kitakachomshukia huko. Atapiga porojo kupitia waandishi wa habari tu, ambao atawapa kodogodogo ili wachapie zaidi story ionekane kumfaa yeye zaidi. Sifa ya ufisadi weacha tu. Wamebobea.

Leka
 

Sweeping statements hazifai! Wapigakura wa Kyela si wote wanaoweza kumwita ama kumwambia 'mpiganaji'/Mbunge wao 'amefulia'. Mwakyembe amedhihirisha kwa vitendo kwamba anao uchungu wa dhati wa nchi yake. Mwakyembe ana guts ambazo wengi humu JF na nje ya JF hatuna. Vile vile naamini kabisa kwamba hata kama Mwakyembe hatakuwa Mbunge, popote atakapokuwa ataendelea kuwa 'mpiganaji' na mkereketwa wa nchi hii.

Laiti mngeliona alivyoshangiliwa na ukumbi mzima pale Karimjee hall wakati anataka huo mdahalo na Rostam mngelijua jinsi ambavyo wananchi wamechoshwa na yote yanayoendelea nchini. Kongamano lililoandaliwa na MNF ni kongamano la aina yake ambalo lilihudhuriwa na watu wa aina zote. Walikuwepo wazee wa nchi hii - akina Job Lusinde, Edwin Mtei, Ndejembi, Mwakawago, vijana akina Nape, Maaskofu, Masheikh, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Maprofesa akina Baregu, Shivji na wasomi kadha wa kadha, viongozi wa Serikali kama Hawa Ghasia aliyeharibu hali ya hewa, Mkuchika naye alihudhuria siku ya mwisho. Walikuwepo wananchi wa kawaida kutoka Dar es Salaam na vitongoji vyake halikadhalika walikuwepo waliosafiri kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania wakiwemo wajasiriamali kutoka maeneo kama Maswa Shinyanga walioamua kuja kwenye Kongamano baada ya kusikia kwenye vyombo vya habari kwamba kuna Kongamano hilo linahusu Mustakabali wa Taifa,n.k, n.k. Watu kutoka makundi yote hayo walipata nafasi ya kuzungumza na wote walizingumzia matatizo ya mmomonyoko wa maadili na kukiukwa kwa misingi mizuri walituwekea waasisi wa taifa hili, Hiyo ilidhihirisha ni jinsi gani wananchi wengi wanaona hali ya nchi yao ilivyo na jinsi walivyochoka kuona hali hiyo ikiendelea.

Kuwakandia wale wanaojaribu kupigania kuinusuru nchi yetu kutokana na janga linalotunyemelea litakaloletwa na mmomonyoko wa maadili, ni sawa na kuisaliti nchi yetu. Whatever the style, kama lengo ni kutaka tufike kule kunakodhamiriwa sioni sababu yoyote ya kuwakatisha tamaa wanaojaribu kuthubutu. Tabia ya kukandia wengine wanaojitokeza kusema haijengi bali inazidi kubomoa na inadhahirisha kwamba hatuna nia ya dhati ya kutaka kurekebisha matatizo yaliyopo nchini.
 

Kwani ni lazima huo mjadala uwe kwenye media?si wakakae huko wabishane?si tunataka kuona ufumbuzi wa tatizo inapatikana na si ushindani wakujenga hoja
 

- Heshima yako mkuu, sina urafiki naye, isipokuwa ninasuuzika sana anapotoa hoja on masilahi ya taifa, kuhusu Kyela labda utuwekee tu mapungufu yake hapa mimi ninamuheshimu sana kwenye masilahi ya taifa tu ya Kyela sijui!

Respect.

FMEs!
 

- Haya ni maneno mazito sana katika kujali masilahi ya taifa, it cool na I am down mkuu!

Respect.


FMEs!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…