Mwalimu afungwa miaka 30 kwa kumlawiti mwanafunzi

Mwalimu afungwa miaka 30 kwa kumlawiti mwanafunzi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma mkoani Mara, imemuhukumu kwenda jela miaka 30 mwalimu Idrisa Athumani (29) wa shule ya Msingi Kyawazaru iliyopo wilayani Butiama baada ya kukutwa na hatia ya kumlawiti mwanafunzi wake

Hukumu hiyo imetolewa leo Septemba 16,2022 ikiwa ni siku mbili tu tangu mwalimu huyo kuhukumiwa kifungo cha maisha jela na Mahakama ya Wilaya ya Musoma baada ya kupatikana na hatia ya kulawiti mwanafunzi mwingine.

Akisoma hukumu hiyo leo, Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, Erick Marley amesema kuwa mahakama hiyo imejiridhisha pasi na shaka kuwa mwalimu huyo aliyeajiriwa Desemba mwaka 2020 na kuanza kazi shuleni hapo Januari, 2021 alitenda kosa hilo kutokana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo.

"Mahakama hii inakutia hatiani kutokana na kosa uliloshtakiwa nalo na ili iwe mfano kwako wewe na wengine wenye tabia kama yako ukizingatia kuwa umekabidhiwa watoto ili kuwatunza na hili suala ni kinyume na tamaduni zetu, halitakiwi wala kuruhusiwa nakuhukumu kwenda jela miaka 30" amesema

mwalimu.jpg

PICHA: Mwalimu Idrisa Athumani Najela
 
Musoma. Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma mkoani Mara, imemuhukumu kwenda jela miaka 30 mwalimu Idrisa Athumani (29) wa shule ya Msingi Kyawazaru iliyopo wilayani Butiama baada ya kukutwa na hatia ya kumlawiti mwanafunzi wake

Hukumu hiyo imetolewa leo Septemba 16,2022 ikiwa ni siku mbili tu tangu mwalimu huyo kuhukumiwa kifungo cha maisha jela na Mahakama ya Wilaya ya Musoma baada ya kupatikana na hatia ya kulawiti mwanafunzi mwingine.

Akisoma hukumu hiyo leo, Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, Erick Marley amesema kuwa mahakama hiyo imejiridhisha pasi na shaka kuwa mwalimu huyo aliyeajiriwa Desemba mwaka 2020 na kuanza kazi shuleni hapo Januari, 2021 alitenda kosa hilo kutokana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo.

"Mahakama hii inakutia hatiani kutokana na kosa uliloshtakiwa nalo na ili iwe mfano kwako wewe na wengine wenye tabia kama yako ukizingatia kuwa umekabidhiwa watoto ili kuwatunza na hili suala ni kinyume na tamaduni zetu, halitakiwi wala kuruhusiwa nakuhukumu kwenda jela miaka 30" amesema

Akisoma maelezo ya shtaka hilo, hakimu Marley amesema kuwa mwalimu huyo alishtakiwa Julai 20, 2022 kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wake wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 12.

" Tukio lilifanyika tarehe ambayo bado haujajulikana Mei mwaka huu majira ya saa nane mchana baada ya mshtakiwa kumuita mwanafunzi wake akiwa na nia ya kutenda kosa hili" amesema

Amesema kuwa siku ya tukio mwalimu huyo alimuita mwanafunzi huyo kisha kumtaka avue nguo agizo ambalo mwanafunzi huyo aligoma kutekeleza kisha mwalimu kumshika kwa nguvu na kumvua nguo kisha kumuinamisha na kutenda kosa hilo.

Alipotakiwa kujitetea mwalimu huyo ambaye ni mwalimu wa nidhamu shuleni kwake ameiomba mahakama hiyo kumpa adhabu ndogo kwani yeye ni baba wa familia mwenye mke mmoja na watoto wawili hivyo familia yake inamtegemea.
 
Ticha anaenda kukutana na njemba ambazo zikiona mng'ao kina diki wanasimama
 
Back
Top Bottom