Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,019
- 579
Sijui kama hapa ni mahali pake, lakini najua wanajamii forum wengi sana watahusika na habari hizi.
Mwalimu Anganile Mpeta ametuaga duniani tangu jana kunako saa 12.00 jioni baada ya kubanwa pumzi ghafla akiwa nyumbani kwake Rujewa Mbarali Mbeya. Alipelekwa hospitalini haraka na baada ya kama dakika 15 aliaga dunia. Niandikapo hivi, mwili wa marehemu Anganile Mpeta unafanyiwa taratibu za kuagwa pale Rujewa na kisha kupelekwa IWAMBI SEKONDARI mjini Mbeya ambako alikuwa Mkuu wa Shule ya Sekondari moja karibu na Ivumwe ili nao wakamuage na kisha apelekwe kijijini alikozaliwa Mbigili Rungwe East kwa maziko kesho.
Marehemu Anganile Mpeta alisoma Mwakaleli Middle School kunako 1971, akasoma Sekondari hadi Kidato cha Sita ambapo alikwenda Mujibu JKT na kushiriki vita ya Iddi Amin kule Kagera 1979. Kutoka hapo alijiunga na chuo cha Ualimu Chang'ombe DSM miaka 2, akapangiwa kazi Masasi Girls Secondary School Mtwara akiwa na Diploma.
Baadaye alijiunga Chuo Kikuu cha DSM akapata Degree ya kwanza ya (Uchumi), kisha akapangiwa kazi Minaki Sekondari ambako alifundisha kwa kutoa As nyingi sana za Economics (EGM), akateuliwa kuwa Discipline Master wa Shule na baadaye Mkuu Msaidizi wa Minaki Sekondari kwa miaka kadhaa. Kisha alihamishiwa Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya kufungua Kyela Secondary School kama Mkuu wa Shule, ambapo baada ya miaka kadhaa alihamishiwa Rujewa Sekondary School kama Mkuu wa Shule wa kwanza kuifungua shule hiyo. Mwaka jana alihamishiwa shule ya mjini Mbeya (IWAMBI) ambako aliendelea kuwa Mkuu wa shule hiyo hadi umauti ulipomfika.
Marehemu Anganile Mpeta atakumbukwa kwa mambo mengi na wanafunzi wake na wafanyakazi wenzake hata majirani kwa kutokuwa mwongeaji sana na kufuata sana utaratibu uliowekwa. Alikuwa kama hataki kukifanya kitu anakuambia waziwazi pasipo kusubiri.
Aliaza kusumbuliwa na tatizo la moyo ambalo kidogo limuwahishe miaka michache iliyopita kama daktari maarufu Dr Mabula wa Hospitali ya Rufaa Mbeya asingeingilia kati, akarudi katika afya ya kawaida na kunawiri sana hata kuacha vyote alivyoagizwa kuachana navyo ili kutoathiri matibabu, mtoto wa kwanza kwa baba yake Mchungaji Mstaafu wa KKKKT Dayosisi ya Konde, Mch. Anganile Mwakapola (Mwaipwisi) ameacha mke na watoto wawili.
Hayo ni maelezo machache sana yamhusuyo mwanataaluma wetu aliyetupotea, ili angalau wawili watatu waweze kukumkuka kwa kuwa picha haijapatikana mara moja. Ni maelezo ambayo huenda yanaweza kusahihishwa kidogo hapa na pale, lakini kimsingi
Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema sana peponi, Amin.
Mwalimu Anganile Mpeta ametuaga duniani tangu jana kunako saa 12.00 jioni baada ya kubanwa pumzi ghafla akiwa nyumbani kwake Rujewa Mbarali Mbeya. Alipelekwa hospitalini haraka na baada ya kama dakika 15 aliaga dunia. Niandikapo hivi, mwili wa marehemu Anganile Mpeta unafanyiwa taratibu za kuagwa pale Rujewa na kisha kupelekwa IWAMBI SEKONDARI mjini Mbeya ambako alikuwa Mkuu wa Shule ya Sekondari moja karibu na Ivumwe ili nao wakamuage na kisha apelekwe kijijini alikozaliwa Mbigili Rungwe East kwa maziko kesho.
Marehemu Anganile Mpeta alisoma Mwakaleli Middle School kunako 1971, akasoma Sekondari hadi Kidato cha Sita ambapo alikwenda Mujibu JKT na kushiriki vita ya Iddi Amin kule Kagera 1979. Kutoka hapo alijiunga na chuo cha Ualimu Chang'ombe DSM miaka 2, akapangiwa kazi Masasi Girls Secondary School Mtwara akiwa na Diploma.
Baadaye alijiunga Chuo Kikuu cha DSM akapata Degree ya kwanza ya (Uchumi), kisha akapangiwa kazi Minaki Sekondari ambako alifundisha kwa kutoa As nyingi sana za Economics (EGM), akateuliwa kuwa Discipline Master wa Shule na baadaye Mkuu Msaidizi wa Minaki Sekondari kwa miaka kadhaa. Kisha alihamishiwa Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya kufungua Kyela Secondary School kama Mkuu wa Shule, ambapo baada ya miaka kadhaa alihamishiwa Rujewa Sekondary School kama Mkuu wa Shule wa kwanza kuifungua shule hiyo. Mwaka jana alihamishiwa shule ya mjini Mbeya (IWAMBI) ambako aliendelea kuwa Mkuu wa shule hiyo hadi umauti ulipomfika.
Marehemu Anganile Mpeta atakumbukwa kwa mambo mengi na wanafunzi wake na wafanyakazi wenzake hata majirani kwa kutokuwa mwongeaji sana na kufuata sana utaratibu uliowekwa. Alikuwa kama hataki kukifanya kitu anakuambia waziwazi pasipo kusubiri.
Aliaza kusumbuliwa na tatizo la moyo ambalo kidogo limuwahishe miaka michache iliyopita kama daktari maarufu Dr Mabula wa Hospitali ya Rufaa Mbeya asingeingilia kati, akarudi katika afya ya kawaida na kunawiri sana hata kuacha vyote alivyoagizwa kuachana navyo ili kutoathiri matibabu, mtoto wa kwanza kwa baba yake Mchungaji Mstaafu wa KKKKT Dayosisi ya Konde, Mch. Anganile Mwakapola (Mwaipwisi) ameacha mke na watoto wawili.
Hayo ni maelezo machache sana yamhusuyo mwanataaluma wetu aliyetupotea, ili angalau wawili watatu waweze kukumkuka kwa kuwa picha haijapatikana mara moja. Ni maelezo ambayo huenda yanaweza kusahihishwa kidogo hapa na pale, lakini kimsingi
Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema sana peponi, Amin.