mwalimu daraja "A" maana yake nini?

Marire

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2012
Posts
12,333
Reaction score
5,292
salaam wana.jf
kuna mtu wangu wa karibu kaletewa cheti cha ualimu ila kimeandikwa daraja A. je,hilo daraja ndio linafaa kufundishia au nini?
__anaweza kuajiriwa ualimu?
na je waalimu wanaajiriwa na nani?
 
ticha ticha saidie mimi
 
salaam wana.jf
kuna mtu wangu wa karibu kaletewa cheti cha ualimu ila kimeandikwa daraja A. je,hilo daraja ndio linafaa kufundishia au nini?
__anaweza kuajiriwa ualimu?
na je waalimu wanaajiriwa na nani?

Mtu wako wa karibu ndiyo nini? Sema kama ni demu wako. Haya, Mwalimu daraja "A" ni yule aliyemaliza kidato cha 4 na kusoma Astashahada ya Ualimu (Certificate in Teaching) Kwa mujibu wa Sera ya Elimu na Mafunzo (Education and Training Policy) ya mwaka 1995, mwalimu wa daraja "A" anaruhusiwa kufundisha katika shule za msingi tu.

Anaweza kuajiriwa na serikali au wenye shule binafsi kama sio kilaza.

Walimu wana waajiri wengi, Serikali ya Tanzania (kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mamlaka za Serikali za Mitaa,Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto nk), mashirika ya dini, watu binafsi nk
 

mke wangu mkuu.
sasa kama anataka kuomba kufundisha ataambatanisha na matokeo ya mtiani wa chuo?
 
Nnavyo faham, hizi grade za ualimu zilikuja enzi za UPE (sina hakika sana), hawa walimu walikuwa wanatofautiana kiwango cha elimu japokuwa wote wanafundisha shule ya msingi,
1: kuna wale walim ambao wamemaliza darasa la saba, na kusomea ualim wao walipewa daraja B (grade B)
2: kuna wale wa darasa la nne na kusomea ualim, wao walipewa daraja C (grade c).
3: Yule aliefika darasa la kumi na mbili na kusomea ualim, alipewa daraja A (grade A).

Kwa hivi sasa hao waalimu wa grade B and C almost kama wameisha, hivi sasa walio baki ni hao wa grade A peke yake.

Kwa taratibu za sasa walim huajiriwa na serikali moja kwa moja, labda atake kwenda kuajiriwa shule za private
 
kwa hiyo wakuu
ni taratibu gani za kufuata ili kupata ajira?
 
kwa hiyo wakuu
ni taratibu gani za kufuata ili kupata ajira?

Ajira serikalini atapangiwa moja kwa moja (kama amemaliza mwaka jana) na kama ni private aandike barua shule husika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…