Mwalimu mkuu atunukiwa kinyago cha kutisha baada ya shule yake kushika mkia NECTA

Yes, Why not

wewe mdau kigogo wa NECTA atayepitisha hiyo adhabu kwa viongozi wa elimu ngazi za juu anajiandalia mazingira ya kunyemelewa na "SABBATICAL LEAVE" kama aliyokumbana nayo dr. ndalichako ...kwani kaishia kupoteza tonge mdomoni.... ila ni wazo zuri nafikili wadau husika watalifanyia kazi.
 
Hivi madiwani lazima wavae hiyo mijoho?

Ndiyo coz huo ndo mtoko wao. Akivaa hivyo lazima umuite mheshimiwa .... ole wako ukaidi au upindishe itifaki , waweza kabidhiwa na wewe kinyago chako cha mpapule.
 
Kwa hiyo kinyago kinaondoa matatizo lukuki kama: Upungufu wa walimu, madarasa, vitabu na mazingira duni mashuleni? Pathetic move.
 
Sijaona usirias wa hicho kinachotendeka,unaadhibiwa huku unatabasamu.
 
tena Alitakiwa ampe zawadi huku amenuna, sio wanachekelea
 
kwi kwi kwi kwi kwi kwi nimecheka sana kimoja inabidi akiweke nyumbani kwake ili kiwe kinamkubusha kuwakomalia walimu kumaliza syllabus na kuwapa watoto majaribio ya kutosha sio mwalimu kwa mwezi mnamuona mara moja tu
 
kimoja atengenezewe dhaifu akistaafu tunampa
 
Nakipokea nakiuza kinyago kwa watalii napata hela. Kila mwaka nikipokea nauza.
 
kwi kwi kwi kwi kwi kwi nimecheka sana kimoja inabidi akiweke nyumbani kwake ili kiwe kinamkubusha kuwakomalia walimu kumaliza syllabus na kuwapa watoto majaribio ya kutosha sio mwalimu kwa mwezi mnamuona mara moja tu

Ahahaaa.. kuna siku atakuja kazini kavimba mihasira ya kukitizama hicho kinyago cha mpapule alipokuwa anakunywa chai... ukichanganya na hasira za kugombana na mkewe/ mumewe ndo usiseme
 
Sijaona usirias wa hicho kinachotendeka,unaadhibiwa huku unatabasamu.

Utaona usiriasi wake utapokuwa unawasili shuleni kwako huku ikigongwa kengele ya kukusanya wanafunzi waje waoneshwe zawadi amabyo shule yako imeshinda... kwa mbali umuone ticha flani mkuda ndo utanuna mara buku. usiombe yakukute mkuu.
 
Chanzo: Chimbwara

Lazima kuangalia kwanza sababu za shule hiyo kufanya vibaya. Kama haina walimu wa kutosha na wenye sifa na ikiwa haina vifaa vya kutosha kwaajili ya kufundishia na kujifunza kama madarasa na vitabu, basi serikali ndiyo inayopaswa kupewa kinyago hicho!
 
Najua watakua wanakiangalia na kucheka tu....kipi bora kutoa kinyago ama kurudisha mtihan wa darasa la nne na ule wa lasaba uwe kwa umakini zaidi bila kusahau wastan kidato cha pili usiwe ishirini?kwa staili hyo hadi waziri atapewa kinyago.
 
Hicho anastahili apewe dk JK anapomaliza muda wake
 
Huo mpango nimeupenda sana ila kama ni mimi ningetoa zawadi hiyo kwa mkuu wa shule na viboko kumi kwa waziri wa elimu hadharani mbele ya wanafunzi na wazazi wao bila kusahau waandishi wa habari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…